iPhone ni kama gereza la kifahari. Ni kwajili ya fasheni tu, hutaweza kufanya vitu muhimu vifuatavyo...

Siyo kweli app karibu zote kubwa zimeanzia iPhone ndo zikaja android. App nyingi sana zimeanzia iOS kuanzia whatsapp, instagram (ios imeanza toka 2010 wakati android version imetolewa 2012), snapchat imeanzia ios mwaka 2011, app maarufu unazojua wewe asilimia 80% zimeanzia ios taja yoyote achana na hizi app ambazo ni ndogo ndogo au anazotengeneza google mwenyewe lakini maarufu zimeanzia iOS.
Mimi nimeahamia samsung siyo kwasababu yaapp yoyote maarufu ni kwasababu ya app mahusui kwa kazi ninayofanya na wala hutoikuta playstore maana si kwa ajili ya public use.
Kuweka app app store ni ngumu kuliko play store hata malipo ni makubwa ndiyo maana utakuta kuna apps nyigni za kipuuzi playstore kwakuwa anyone anaweza weka vitu huko na ndiyo maana inaongoza kuwa na app nyingi lakini nyingine za kipuuzi na hazifanyi kile utakachosoma kwenye review. Mtu anatengeneza ki app anaweka maelezo ya uongo ili mradi tu mtu akidownload apate matangazo avute ela.
 
Kuna iphone haters wengi sana humu na Tz kwa jumla. Ni kama haters wavijana wanaomiliki magari..huwezi kuta mtu wa iphone anatoka povu la omo kuhusu simu zingine au anafungua uzi kuponda simu za android na zingine, sijui ni wivu au chuki tu! Dah...
 
Samsung au Huawei kuuza simu nyingi zinakusaidiaje wewe mteja??
Mwambie ni sawa na update za vingamuzi Tu user hufaidi chochote hahaaaaaaa😁😁😁 natengua kauli ninakuja IOS nikipata hela
 
Iphones generation nzuri inaanzia Iphone 8 kwenda mbele baadhi ya faida

1.Zinakaa na chaji hadi siku 2

2.Mtu akiiba atalitupa au auze screpa

3.Haiwezi haribika ikiguswa na maji hata kama utazimisha kwenye mtungi.


Mwisho kila mtu anatumia anchotaka
 
Kuna iphone haters wengi sana humu na Tz kwa jumla. Ni kama haters wavijana wanaomiliki magari..huwezi kuta mtu wa iphone anatoka povu la omo kuhusu simu zingine au anafungua uzi kuponda simu za android na zingine, sijui ni wivu au chuki tu! Dah...
inategemea ni iphone ipi 7 kushuka chini ni tecno tu.

ndio wanatusumbua kitaa.

kwanza zinauzwa mpaka laki 3 bei ya infinix kabisa hii.
 
Zinauzwa wapi kwa hapo Dar es Salaam ? Nikanununr hata kama 1 mill.. maisha yenyewe ndio haya haya
 
Zinauzwa wapi kwa hapo Dar es Salaam ? Nikanununr hata kama 1 mill.. maisha yenyewe ndio haya haya
Sehemu nyingi tu mkuu hata maduka yao yaliyosajiliwa hata pale mlimani city na shopers utapata japo hao bei yao siyo rafiki
 
Android users sababu zao za kitoto sana, Mwingine analilia kubadilisha Fonts. Yaani unamkuta mtu ana wallpapers hadi kwenye keyboard.
Na wengi hawanunui flagships.

Wananunua models za mwisho kabisa ndo wanaanza kelele.

Apple hana models za kijinga.
 
inategemea ni iphone ipi 7 kushuka chini ni tecno tu.

ndio wanatusumbua kitaa.

kwanza zinauzwa mpaka laki 3 bei ya infinix kabisa hii.
Laki 3 ni refub halafu used hapa bongo.
 
Na wengi hawanunui flagships.

Wananunua models za mwisho kabisa ndo wanaanza kelele.

Apple hana models za kijinga.
Mkuu bila hizi simu za laki za android ukoo hapa bongo wenye simu za bei wangebaki wachache tu.

Shukuru kwamba android wana simu hata za laki siku hizi hata watu wameongezeka wanaoweza kuanzisha ama kuchangia maada humu jamii forums zenye misaada, Hata huku whatsapp kumenoga zaidi pale hata wenzetu wenye vipato vya chini wanapoweza kujiunga whatsapp.

Ni kushukuru android kwa kufabikisha haya hapa Tanzania simu zimefanya tuishi kama kijiji kupitia social media, Kutumiana documents, taarifa muhimu, n.k

Android swala la bajeti si kikwazo, utapata simu ya laki hadi huko milioni 3 kama upo vizuri.

Apple huku bajeti walau uwe na milioni kama utahitaji simu dukani ukiachana na hizi za mitumba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…