Ipi bora: Madirisha ya vioo vya ku slide ama ya mbao kwa marembo ya nondo

FORWARD

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2014
Posts
740
Reaction score
293
Habari wadau, miaka ya hivi karibuni nyumba nyingi za hapa jijini Dsm zimekuwa zikiwekewa madirisha ya vioo vya ku slide na kuyapa kisogo madirisha ya mbao kwa marembo ya nondo, Je Tukizingingatia maswala ya fashion na hali ya hewa la jiji la Dsm , aina gani ya madirisha yanafaa zaidi?
 
.... Je Tukizingingatia maswala ya fashion na hali ya hewa la jiji la Dsm , aina gani ya madirisha yanafaa zaidi?
Hali ya hewa ya DSM ipoje?
 
Mtoa mada hujui unachokitaka

Mimi najua nacho kitaka swala linalokuja hapo ni ushawishi wa watu wa pembeni + je kuna umuhimu gani kukubaliana nao na kuacha lile nalofikiri ni sahihi kwangu.
 
Watu wanapenda aluminium sababu yanaonekana ndiyo yanakwenda na wakati, na kama unatumia AC muda mwingi na muunekano unavutia. Aluminium yanaongeza joto.

Lakini kwa hali ya Dar ya joto, kwa kweli mbao ni nzuri zaidi na ukipata fundi mzuri utayapenda. mimi niliweka aluminium ,rafiki yangu akaweka mbao kwakweli nimemtamani.
Sema kama unataka kwenda na wakati aluminium sawa lakini mbao ni best ila yawe makubwa yanakuwa na mvuto yaidi
 
Tunaweka aluminium kwa kipindi hiki kwa sababu ya uhaba wa mbao. Kama ukipata mbao nzuri za kutosha ya mbao ndio yanaendana na majengo yetu. Madirisha ya kuslide sio mazuri labda yawe makubwa ya kutosha kwani yanapunguza eneo la kupitisha hewa ya kutosha! Unaweza ukaweka madirisha ya aluminium ya kufunguka vilevile.
 

Hivi una akili ya kuslide ni digitally na ya mbao ni analogue utachekwa mkuu
 
Hivi una akili ya kuslide ni digitally na ya mbao ni analogue utachekwa mkuu

Akili ipi unayoizungumzia hapo? Kipi hasa kimesababisha iyo ya ku slide kuwa bora? Maana kama hauna Ac ni sawa na kufunga vioo vya dsm la mbagala mwenge saa saba mchana wa jua kali. Kifasheni ni mazur ila yanatesa kwa joto la dsm.
 

Nakubaliana na wewe.
 

Kwa kweli umenipa majibu nayoyatafuta.
 
Inategemea na Architectural specification...
 
kwa gharama ya aluminum ni zaidi maana lazima uweke na grill juu yake!

kaka it depends na aina ya mbao unayotaka kutumia. kama unatumia gravellia au pine, sawa.. but if you are going for prime quality muninga au mkongo.. it is very very expensive
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…