Ipi ni bora kati ya Subaru forester (Isiyo na turbo) na Volkswagen Tiguan, zote za 2010?

Socw

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2016
Posts
1,329
Reaction score
2,644
Habari wakuu,

Utamshauri mtu anunue gari ipi kati ya gari hizo mbili kwa kuzingatia vigezo vya mazingira ya miundombinu ya barabara zetu, hali ya kiuchumi (kipato cha kati) na upatikanaji wa mafundi wa kueleweka na vipuri.


Subaru forester



Volkswagen tiguan​
 
T
Technical issues muwe mnafafanua. Mi hapo sielewi kitu yaani!
Hiyo ni dual clutch gearbox sio CVT au auto za kawaida ambazo zipo kwenye gali nyingi za mjapan. Hii inafanya inachanganya faster faster kutafuta speed ya juu na ndiyo maana unakuta gari zao zina top speed mpaka 240.

Subaru ina CVT transmission haiko sporty,ipo slow lakini hauta shindwa garage kwa fundi maiko kwa matengenezo kila siku 🤗.
 
Technical issues muwe mnafafanua. Mi hapo sielewi kitu yaani!
Angalia jinsi Volkswagen gear level yake inavyokuwa Kwanza ina option ya manual na automatically pia ina sport mode hii ni technology ambayo mjapan hawezi kufanya kwenye gear box moja(dual clutch plates)...
Kama mnafukuzana na Volkswagen dhidi ya Subaru basi tambua kuwa Volkswagen atakuwa anaovertake sehemu ambazo wewe hautaweza huyu mwenzio anaweza akavuka magari Hadi 4 Kwa sekunde 10 Tu.

Hayo magari ya kijerumani usifananishe na wajapan wameachwa mbali Sana kwenye performance
 
Asante mkuu kwa kuchukua muda wako kufafanua. Nimepata mwanga.
 
Mzee chukua Tiguan hutojuta, Volkswagen inamuacha Subaru ktk nyanja zote. Chukua mjerumani halisi VW

Usimdanganye mwenzio, mwambie ni maeneo tiguan inaizidi forester, ila si yote. Mfano tu kwenye suala la off-road ability, tiguan haiwezi kuifuata forester.
Reliability ni eneo jingine Subaru ni afadhali kuliko Tiguan.
Space ndani ya gari na boot, Forester ni zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…