Ipi ni kesho ya Taifa katika ukuaji wa Sayansi na teknolojia?

Ipi ni kesho ya Taifa katika ukuaji wa Sayansi na teknolojia?

TheForgotten Genious

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2014
Posts
2,087
Reaction score
3,156
Kenya kesho wanazindua na kurusha Satellite yao walioipa jina Taifa-1 na ikumbukwe Kenya wana Laptops na desktops zao zinaitwa taifa.

Tanzania haieleweki katika uga wa elimu,katika ukuaji wa sayansi na teknolojia ndio kama mfu,hawana mpango maalumu wakuvumbua vipaji bunifu katika teknolojia na kuvikuza,ile tume ya sayansi na teknolojia ipo kama mshenga tuhaina mchango wowote ule.

Utazungumziaje maendeleo ya kiuchumi leo halafu ukajitenga na maendeleo ya sayansi na teknolojia?

Nchi imeshindwa kuwapa nafasi watu kubuni hata sakiti ya subwoofer ambayo ni logic ndogo tu,nimeshuhudia mawazo bunifu ya kiteknolojia yaliyogunduliwa na vijana wa kitanzania lakini serikali haijayapa kipaumbele ni kama hawaelewi faida yake,,wenye uwezo wamediriki mawazo yao kuyauza mbali ili hali ingekuwa ni credit kwa taifa endapo ingewezesha.

Kichwa cha mwendawazimu.
 
Back
Top Bottom