Ipi njia sahihi ya kushukuru (kutoa shukrani)

Ipi njia sahihi ya kushukuru (kutoa shukrani)

Mla Bata

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2013
Posts
7,841
Reaction score
17,491
Wasalaam,

Hakika Mungu wetu ni mwema nyakati zote, niseme tu mimi Mla Bata si miongoni mwa wafia dini yeyote, wala mwenye kuyajua mengi yahusuyo dini hizi mbili za (ukristo & uislamu), lakini ni mwenye imani ya kuamini kuna nguvu kubwa inayozidi nguvu zote, viumbe vyote na yote yaliyomo ndani na nje ya ulimwengu.

kipindi cha karibuni nilikumbwa na changamoto fulani fulani za kimaisha ziluzonifanya niache kila kitu na nikae chini kusema na nguvu hii kubwa yenye kutawala ulimwengu (Mungu), imani huponya! Mungu amejibu karibia yote niliyomuomba tena kwa kipindi kifupi sana, hivyo kuufanya moyo wangu na nafsi yangu kutamani kufanya jambo kubwa la shukrani litakalofanya niwe na amani,

Nimeshajaribu kwenda kutoa sadaka sehemu za ibada kutoka katika yale niyapatayo kwenye utafutaji wangu, nishatoa kwa wenye uhitaji ikiwemo ndugu na jamaa wa karibu, lakini nafsi yangu haina amani, kila nikikaa nahisi Mungu ananidai shukrani kwa yale aliyonitendea.

Je ni jambo gani la shukrani lenye nguvu linalopaswa kufanywa kama sehemu ya kumshukuru Mungu kwa wema na matendo yake? Kama nilivyosema awali si muumini wa hizi dini mbili za (ukristo na uislamu) lakini naamini kwenye uwepo wa Mungu mmoja mwenye nguvu na mamlaka na ulimwengu na vilivyomo ndani yake, natanguliza shukrani kwa wale wote wenye michango ya kujenga.


Wasalam,

"Everything is possible for those who believe" lets meet at the top, cheers 🥂.

Mla bata

München, Deutschland 🇩🇪.
 
Ninaweza kuwa mmoja wapo wenye mafanikio makubwa zaidi kuliko wewe unavyoona ila siamini chochote kutoka kwa Mungu kama nadharia , hilo unalizungumzia vip🤔
 
Mkuu wasiidie wasio jiwezi
Yatima
Wagonjwa ambao hawana ndugu na hawana pesa ya Tiba hasa pale muhimbili.

Ila katika kutoa kwako TOa ukiweka Nia kuwa nashukuru Sana Mungu Kwa kila jambo NATOa msaada huu kama shukrani kwako.


Mimi nimewai kuwa muislamu pia nimewai kuwa mkristo
Ila naona Dini ni sehemu za watu kupiga pesa tu...!

Mungu yupo Ila Dini ni njia na Sio kila njia ni sahihi na unaweza kufika popote Kwa kutumia njia zako
 
Ninaweza kuwa mmoja wapo wenye mafanikio makubwa zaidi kuliko wewe unavyoona ila siamini chochote kutoka kwa Mungu kama nadharia , hilo unalizungumzia vip🤔
I agree to disagree & i got no comment on that. 🙏🏽
 
Wasalaam,

Hakika Mungu wetu ni mwema nyakati zote, niseme tu mimi Mla Bata si miongoni mwa wafia dini yeyote, wala mwenye kuyajua mengi yahusuyo dini hizi mbili za (ukristo & uislamu), lakini ni mwenye imani ya kuamini kuna nguvu kubwa inayozidi nguvu zote, viumbe vyote na yote yaliyomo ndani na nje ya ulimwengu.

kipindi cha karibuni nilikumbwa na changamoto fulani fulani za kimaisha ziluzonifanya niache kila kitu na nikae chini kusema na nguvu hii kubwa yenye kutawala ulimwengu (Mungu), imani huponya! Mungu amejibu karibia yote niliyomuomba tena kwa kipindi kifupi sana, hivyo kuufanya moyo wangu na nafsi yangu kutamani kufanya jambo kubwa la shukrani,

litakalofanya niwe na amani, nimeshajaribu kwenda kutoa sadaka sehemu za ibada kutoka katika yale niyapatayo kwenye utafutaji wangu, nishatoa kwa wenye uhitaji ikiwemo ndugu na jamaa wa karibu, lakini nafsi yangu haina amani, kila nikikaa nahisi Mungu ananidai shukrani kwa yale aliyonitendea.

Je ni jambo gani la shukrani lenye nguvu linalopaswa kufanywa kama sehemu ya kumshukuru Mungu kwa wema na matendo yake? Kama nilivyosema awali si muumini wa hizi dini mbili za (ukristo na uislamu) lakini naamini kwenye uwepo wa Mungu mmoja mwenye nguvu na mamlaka na ulimwengu na vilivyomo ndani yake, natanguliza shukrani kwa wale wote wenye michango ya kujenga.


Wasalam,

Mla bata.
Uza mali zako zote kawagawie masikini
NAWASILISHA
 
Wasalaam,

Hakika Mungu wetu ni mwema nyakati zote, niseme tu mimi Mla Bata si miongoni mwa wafia dini yeyote, wala mwenye kuyajua mengi yahusuyo dini hizi mbili za (ukristo & uislamu), lakini ni mwenye imani ya kuamini kuna nguvu kubwa inayozidi nguvu zote, viumbe vyote na yote yaliyomo ndani na nje ya ulimwengu.

kipindi cha karibuni nilikumbwa na changamoto fulani fulani za kimaisha ziluzonifanya niache kila kitu na nikae chini kusema na nguvu hii kubwa yenye kutawala ulimwengu (Mungu), imani huponya! Mungu amejibu karibia yote niliyomuomba tena kwa kipindi kifupi sana, hivyo kuufanya moyo wangu na nafsi yangu kutamani kufanya jambo kubwa la shukrani litakalofanya niwe na amani,

Nimeshajaribu kwenda kutoa sadaka sehemu za ibada kutoka katika yale niyapatayo kwenye utafutaji wangu, nishatoa kwa wenye uhitaji ikiwemo ndugu na jamaa wa karibu, lakini nafsi yangu haina amani, kila nikikaa nahisi Mungu ananidai shukrani kwa yale aliyonitendea.

Je ni jambo gani la shukrani lenye nguvu linalopaswa kufanywa kama sehemu ya kumshukuru Mungu kwa wema na matendo yake? Kama nilivyosema awali si muumini wa hizi dini mbili za (ukristo na uislamu) lakini naamini kwenye uwepo wa Mungu mmoja mwenye nguvu na mamlaka na ulimwengu na vilivyomo ndani yake, natanguliza shukrani kwa wale wote wenye michango ya kujenga.


Wasalam,

Mla bata.
Happy to see again na hongera kwa kuzivuka changamoto .. Pitia huu uzi
 
Back
Top Bottom