Ipi sababu ya Kenya kupendwa kuliko Tanzania licha ya kuwapita utajiri wa utamaduni?

Ipi sababu ya Kenya kupendwa kuliko Tanzania licha ya kuwapita utajiri wa utamaduni?

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Nilikuwa naangalia video flani YouTube inahusu capital city za nchi 54 za Africa. Sasa nikaenda sehemu ya comments kusoma nikajionea watu wengi kutoka mataifa mbalimbali dunia wakiisifia Kenya kuwa ndo favourite country yao lakini kiuhalisia ni dhahiri tumewazidi vivutio (Sina haja ya kuvitaja vinajulikana) pamoja na utamaduni tuna makabila mengi ambayo wazungu labda wangetamani kuja kwetu kujifunza Mila za makabila pia tuna amani hatuna historia mbaya ya kumwagana damu kugombana kubwa zaidi tuna eneo kubwa la ardhi mapori yasiyofanyiwa chochote yameachwa tu hivyo ni rahisi kuwekeza tofauti na Kenya ambapo ardhi inashikiliwa na wachache.

Sielewi kwanini wazungu waipende kenya tukisema kwamba sababu ni ina maendeleo sio kweli maana hata kwao ulaya huko wako vizuri tu hawawezi kuja kushangaa magorofa ya Nairobi hapo na hata hivyo kama kutupita kiuchumi hawajatupita sana ni gap fulani la kawaida.

Ingawa pia nilianza kuhisi labda comments hizo zaweza kuwa ni za Wakenya wenyewe wameamua tu kujimwambafy; si mnajua walivyo makanjanja kwenye kujipaisha.

Video yenyewe iko hapo chini search YouTube nenda upande wa comments.

Screenshot_20220202-000036.jpg
 
Lugha inawabeba wenzetu sana ni Wakati sasa wa kuanza kufundisha Lugha ya Dunia kuanzia Primary mpaka Chuo kikuu, Hili Swala la kukumbatia kiswahili tu. Kwa kweli linatukosesha Kuwa linked na Ulimwengu tembea hata Platform nyingi uone wakenya wanavyo ji brand ila sisi watz tunakwama kwa ajili ya Lugha pia
 
Siyo kwamba Kenya inapendwa ni kuwa Tanzania hatujitangaza vyakutosha licha ya kuwa vivutio vingi.

Ukiwa huko majuu ukijitambulisha kama mtanzania, utashangaa kuullzwa kuwa;

Is Tanzania Nigeria, South Africa or Kenya?

Kwa maswali kama hayo unapata picha kuwa nchi wenzetu wanajua umuhimu wa kujitangaza kimkakati duniani kote.
 
Lugha ndio imewabeba, Leo hii wakenya wengi ndio wanafundisha lugha ya kiswahili huko marekani na ulaya na sasa wanaitwa afrika kusini kufundisha huku sisi ambao tumebobea kiswahili wanatukwepa kwasababu hata lugha ya kuwasiliana na wanafunzi kwa kiingereza ni tatizo.

Huku kwetu lugha ya kiingereza haipewi thamani matokeo yake tunaongea ze ze ze what izi, yani tukatia aibu mpaka ile siku yule mkalimani pale uwanjani ambae kabobea kabisa kibongo bongo alichapia tafsiri 😂😂 , hebu vuta picha tu yule waziri wa elimu alipata A masomo yote ikiwemo kiingereza naskia lakini kiingereza anachoongea ni broken si mchezo, nae Marehemu Magu aliweza kusoma hadi phd ila lugha ilimpa tabu, hata Kikwete tunaemsifia anajua kiingereza no vile tu ni kibongo bongo lakini nae kiukweli bado, nae rais wa sasa Anaweza kuwa vizuri kwenye kiingereza cha kusoma speech ambazo zimeshaandikwa lakini akihutubia ama akiongea kivyake vyake kama yeye hapo huwa ni tatizo kubwa

Watanzania wengi lugha ya kiingereza wanaiweza kwenye kuandika, yani ukikuta mtanzania ameandika kiingereza huko kwenye status unaweza kudhani ni nect level, haya sasa uje kwenye kiingereza cha kuongea 😂😂😂 utacheka mpaka basi, pia kiingereza wengi hata kuelewana na wazungu huwa inakua taabu maana wazungu wana lafudhi yao ya kumungunya maneno sio hii ya ze ze ze 😂😂.

Wakenya kiingereza kimeqaunganisha na dunia sana, Leo hii maparachichi nchi inayoongozea kuuza ni Kenya lakini yanatokea huku na hii ni kwasababu wao wanaweza lugha kuuza huko nje.

Lugha!! Lugha!! Lugha!!
 
Utajiri wa utamaduni upi.? Au ndo mambo ya kuwafanya wamasai na mila zao waonekane kama kivutio.?
Ndugu yangu siku hizi kuna kitu kinaitwa 'cultural tourism' have you ever heard about it? Hii ni muhimu sana na inaleta pesa nyingi sana kwa wamasai.

Pia Kuna sex tourism wenzetu hapo Lamu na Malindi imeshamiri sana beach boys wanakula wamama wa kizungu kwa malipo naona Zanzibar imeanza hii.

Kuna agricultural tourism etc yani Ile sabasaba day inatakiwa wageni wajae Tanzania kuja kuangalia what do we in the market!

Kuna vitu tumezubaa ndio maana wenzetu wanatupiga bao sehemu ndogo sana.

Sisi tuna vivutio vingi zaidi Ila hatujajiongeza kuvifanya viafahamike kwamba tunavyo ili tuexplore hizo fursa.

Wakisema wanazo fursa tunaanza kukasirika all we have to offer is Kilimanjaro and Serengeti huu no ujinga wakenya hata Kilimanjaro wameacha kuitaja siku hizi.

We have to be proactive.
 
...pamoja na utamaduni tuna makabila mengi ambayo wazungu labda wangetamani kuja kwetu pia tuna amani na eneo kubwa. nashindwa kuelewa kwani je wazungu waipende kenya kisa Ina maendeleo wakati hata kwao wako vizuri tu na Kama kutupita kiuchumi hawajatupita Sana NI gape fulani la kawaida.
BET Awards Red Carpet...
BET.png

Pamoja na mambo mengine, usikute Diamond hapo alidhani alikuwa anaitangaza Tanzania lakini kwa wale ambao ilikuwa ndo mara yao ya kwanza kumuona/kumsikia basi, kwa hiyo dressing code, majority aliwaaminisha yeye ni Mkenya!!

Nini hiyo dressing code, hata Kiswahili huko mbele majority wanadhani Kenya ndo "wenyewe"!!

Ingawaje kwa mbaaaaaaali hivi sasa kidogo inapungua lakini zamani kuitambulisha Tanzania ipo wapi ilikuwa ni kazi ngumu kweli kweli hususani kama HUTAKI kuitaja Kenya kwa sababu the only way kuitambulisha kirahisi ilikuwa uitaje Kenya manake hata ukitaja Mt Kilimanjaro, usishangae ukaambiwa "Oh! So, you mean it's Kenya"!

Bila shaka hapo utakuwa umepata jibu!!

In short, Ujamaa wa Mwalimu ulitufanya Watanzania kuwa mazombi and less aggressive! Na vile hatutaki hata kuwashtua CCM physically, ndo kabisa coz' in Africa, if you don't have something good to showcase, just showcase your unpleasant side!
 
Kungreza tuuu ndicho kinawabeba hata huko ndani ndani mdhungu anaweza wasiliana na yeyote.
 
Biashara matangazo, tena ya akili. Sasa Kigwangala anamchukua Ebitoke akatangaze utalii unategemea nini?
 
Lugha inawabeba wenzetu sana ni Wakati sasa wa kuanza kufundisha Lugha ya Dunia kuanzia Primary mpaka Chuo kikuu, Hili Swala la kukumbatia kiswahili tu. Kwa kweli linatukosesha Kuwa linked na Ulimwengu tembea hata Platform nyingi uone wakenya wanavyo ji brand ila sisi watz tunakwama kwa ajili ya Lugha pia
Sio lugha pekee Bali na uzembe unachangia
 
Natoka kidooog nje ya maada, nataka kuwakumbusha WAHENGA wenzangu humu; miaka ya katikati ya 80 hasa mwaka 1987 wakati ccm inatimiza miaka 10 ilimletaga mwana muziki wa Kikongo bwana Tabu Ley akiwa na mkewe wa mkataba bibi Mbilia Bel wakiwa ndio wametoka kufunga ndoa yao ndani ya ndege kule Paris France, baada ya hapo band nyingi kutoka Congo/Zaire zilianza kuja kwa wingi nchini mwetu, Pepe Kalle, mzee wa Nzawisa, Kanda Bongoman, Bokilo nk; nakumbuka radio by that time ilikuaga moja tu, RTD (sasa TBC taifa ) na swali ambalo lilikua pendwa sana la waandishi wa habari by that time kwa hawa wana music wa nje lilikua hili, "je umewahi kuusikia music wa Tanzania kabla ya kuja hapa"?

Majibu yao yalikua yanafana; kwamba HAPANA sijawahi kuusikia. Binafsi nilikua najiuliza sana why? Wahenga mtakumbuka pia kipindi hicho hicho uliwahi kutokea mgogoro mkubwa sana band ya DDC Mlimani park na radio Tanzania hasa mara baada ya Sikinde kumrudisha mwana music wao kaka Benno Villa Anthon na Maximillian Bushoke kwenye kundi kwamba kazi zao zinauzwa hadi Ujerumani na wao hawapati chochote, ndipo ulipoanza mgogor wa kuto kurekodi pale RTD na badala yake wakaanza kwenda Kenya kabla ya studio ya Don Bosco chini ya MAroon Linje kuanza.

Now coming back to the question which to me will continue to associate with music industry; nimekua mpenzi sana wa nyimbo hizo za Wakongo to date, nasikiliza sana kwa youtube, nasikiliza utunzi wa manguli wa Bongo kina Muhidin Maalimu Gurumo, Bushoke, Hassan rehani Bichuka na solo gita za kina Kassim Mponda, Babu Seya, na yule mashoto wa Ndekule halafu nalinganisha na kina Diblo, Dally Kimoko etc; nakaa najiuliza, why music wetu haukujulikana kama wa Wacokongo/Wazaire those days?

Jibu langu ni rahisi tu, urasimu wa ujamaa na kujitegemea, haukutaka kutangaza chochote nje ya Bongo, tulitaka watu wajue kwa jitihada zao wenyewe which didn't waork out, same same na kwenye UTALII, Kenya inajulikana zaidi kuliko Tanzania ilhali Tanzania kuna vingi kuliko Kenya, makabila as well kama mleta UZI anavyosema, in fact we have a lot compared with Kenya.

Tizama hata sasa hivi Kagame anavyoitangaza Rwanda huko majuu; sasa hvi Rwanda inajulikana zaidi kuliko Tanzania; mwanzoni mwa miaka ya 2000 ulikua ukiwa huko nje na kusema unatokea Tanzania, unawaambiwa wenyeji wako kwamba ile nchi ambayo Osama alipiga ubalozi wa Marekani ndio wanaelekewa, nao imeishapita zaidi ya miaka 20, kizazi kipya kimeingia ambacho wala hakikumbuki about that story of Osama in 1998.

Tatizo bado tunao watu wenye mentality zile zile za kijamaa todate kwenye ulimwengu wa kibepari, angalia hata maofisini kwetu, linganisha utendaji kazi wa Wakenya na sisi, tofauti kabisa. So shida iko hapo kwenye utendaji wetu na kubadirika kulingana na muda, hiyo ndio shida; Kenya ataendelea kusumbua while he/she has nothing comparing with us
 
Ndugu yangu siku hizi kuna kitu kinaitwa 'cultural tourism' have you ever heard about it? Hii ni muhimu sana na inaleta pesa nyingi sana kwa wamasai.

Pia Kuna sex tourism wenzetu hapo Lamu na Malindi imeshamiri sana beach boys wanakula wamama wa kizungu kwa malipo naona Zanzibar imeanza hii.

Kuna agricultural tourism etc yani Ile sabasaba day inatakiwa wageni wajae Tanzania kuja kuangalia what do we in the market!

Kuna vitu tumezubaa ndio maana wenzetu wanatupiga bao sehemu ndogo sana.

Sisi tuna vivutio vingi zaidi Ila hatujajiongeza kuvifanya viafahamike kwamba tunavyo ili tuexplore hizo fursa.

Wakisema wanazo fursa tunaanza kukasirika all we have to offer is Kilimanjaro and Serengeti huu no ujinga wakenya hata Kilimanjaro wameacha kuitaja siku hizi.

We have to be proactive.
❤️
 
Wengi wamekujibu lakini hawajakutendea haki kabisa...

Swali lako inabidi uelewe history ya dunia ilivyokuwa..

Hata Tanzania ilikuwa maarufu Sana Ila kisiaasa na ilikuwa maarufu kwa nchi ambazo zina mlengo mmoja wa kisiaasa..

Kenya walikuwa na siasa za kibepari ambazo Africa hazikupendwa enzi hizo

Tanzania actually ilikuwa na influence Africa nzima na hata nje ya Africa..kwa siasa

Kenya walikuwa wanapendwa na West

USA na UK kwa siasa za kuwaunga mkono nchi hizo ...na kwakuwa Kenya alikuwa almost peke yake ..alipendwa zaidi ..Kenya walikuwa pamoja na South Africa ya makaburu kuunga mkono kila kitu cha West..

Watalii wakawa wanaenda Kenya zaidi..na ikatangazwa zaidi .

Most important ikawa head quarter ya media za West...zote kwa Africa

Hata mashirika ya kimataifa yote yakaweka office Nairobi kwa Africa..by the time dunia inabadilika kisiasa na kuwafata west tayari Sisi tuliokuwa tunafata East ambako ni China na Ussr tushachelewa...sasa hata China anafuata west..
 
Back
Top Bottom