Tanzania ni miongoni mwa nchi ambayo fertility rate iko juu sana. Kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2012 kila familia ilikisiwa kuwa na average ya watoto 5.
Takwimu za kiuchumi mara nyingi zimeonya ongezeko la watu nchini haliendani sawa na ukuaji wa uchumi wetu na kusihi mamlaka husika kuchukua hatua mjarabu.
Ziko Sababu nyingi zinazohusishwa kwa nini waafrika wengi hupenda familia kubwa zikiwemo sababu kama watoto ni rasilimali, gharama nafuu ya kuwakuza, na fahari ya uanaume.
Unakuta mzee kazaa watoto zaidi ya 10, huku hali yake ya uchumi hawezi hata kuwahudumia watoto 2, hali inayopelekea watoto kuishi bila msingi mzuri wa malezi.
Na Kutokana na msingi mbovu alioandaliwa na yeye anakuja kupitia hali ile ile na kusababisha kile kinachoitwa vicious circle of poverty.
Kwa msingi huu naona ni Wakati muafaka wa kuja na Sheria ya kudhibiti idadi ya watoto. Mtu ambaye hana akiba ya kutosha ya malezi asiruhusiwe kufyatua tu na kuja kuwapa wengine mzigo wa malezi.
Watu wote wanaolia na umasikini uliokithiri ni waanga wa kutowajibika kwa wazazi wao.
Sent using Jamii Forums mobile app
Takwimu za kiuchumi mara nyingi zimeonya ongezeko la watu nchini haliendani sawa na ukuaji wa uchumi wetu na kusihi mamlaka husika kuchukua hatua mjarabu.
Ziko Sababu nyingi zinazohusishwa kwa nini waafrika wengi hupenda familia kubwa zikiwemo sababu kama watoto ni rasilimali, gharama nafuu ya kuwakuza, na fahari ya uanaume.
Unakuta mzee kazaa watoto zaidi ya 10, huku hali yake ya uchumi hawezi hata kuwahudumia watoto 2, hali inayopelekea watoto kuishi bila msingi mzuri wa malezi.
Na Kutokana na msingi mbovu alioandaliwa na yeye anakuja kupitia hali ile ile na kusababisha kile kinachoitwa vicious circle of poverty.
Kwa msingi huu naona ni Wakati muafaka wa kuja na Sheria ya kudhibiti idadi ya watoto. Mtu ambaye hana akiba ya kutosha ya malezi asiruhusiwe kufyatua tu na kuja kuwapa wengine mzigo wa malezi.
Watu wote wanaolia na umasikini uliokithiri ni waanga wa kutowajibika kwa wazazi wao.
Sent using Jamii Forums mobile app