Ipo changamoto katika mamlaka ya Uteuzi

Ipo changamoto katika mamlaka ya Uteuzi

Dr Restart

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
4,949
Reaction score
24,046
Wasalaam.

Baada ya sintofahamu ya baadhi ya Wateule kukataa kuapishwa katika nafasi waliyoteuliwa, kumezuka na maswali na minong'ono mingi isiyo na sababu.

Lakini, yote haya yamesababishwa na kuwepo kwa mawasiliano hafifu baina ya upande wa uteuzi na yule aliyeteuliwa. Kwa akili zangu, nilidhani mhusika hujulishwa kupata nafasi hiyo kabla ya majina kutangazwa hadharani.

Kinachoonekana ni kuwa, mamlaka ya uteuzi yamejitwisha haki ya kuamua hatma ya mteuliwa. Wamesahau kuwa watu wana mipango yao mingi, majukumu yao na wengine hawana mpango wa kushikilia wadhifa za aina hiyo.

Lakini pia, aina hiyo ya uteuzi pasipo kushirikisha pande zote mbili kunaaibisha mamlaka haswa ofisi ya Rais. Mtu kukataa nafasi ya uteuzi ni kuonesha kutokuwa makini kwa wale wote wanaohusika na uteuzi. Na kwa kuwa wateuliwa waliteuliwa na Mh Rais, basi inayoaibika ni ofisi husika.

Kukataa pia nafasi ya uteuzi si jambo geni. Ilishatokea na itatokea tena. Polisi na mamlaka zingine ziheshimu maamuzi ya mtu kwa hiyari. Kuwakamata na kuwahoji kisa tu wamekataa uteuzi, huku wakijua wazi kuwa mhusika ana nafasi nyingine ni kutompa mtu haki ya kujiamulia mambo yake.

Wasaidizi wa Rais kwa hapa wamefeli kwa kiwango kikubwa. Na ingelikuwa vema kama watareconcile na upande mwingine kabla ya kufikia maamuzi ya kuteua.

Nawasilisha.
 
Wapo waliomkatalia Nyerere, Mwinyi, Kikwete na hata Mkapa. Iwe Magufuli?

Uamuzi wa mtu uheshimike endapo atatoa sababu zenye logic.
Na hata hofu au uoga wa kutumikia cheo ni sababu tosha kuikataa nafasi
 
Nafikiria Kwa sauti Kama uteuzi angeufanya hayati Dr Magufuli wangekataa?
Wakati wa Magufuli yule alikuwa mfano wa kichaa so alikuwa anaogopwa na kila mtumishi na hii ilikuwa inawarahisishia wateuliwa ktk utendaji wao ila leo mtu anateuliwa kwenda kusimamia watu waliokaa kipigaji pigaji anajua kabisa hataheshimika maana wameshindwa kumuheshimu kiongozi wao mkuu mwisho mteuliwa anatupwa nje ya ulingo kwa aibu kisa kushindwa kusimamia watu walioshauriwa na boss wao kula kwa urefu wa kamba zao.

Teuzi za kiserikali bongo bora mtu ukawe winga Kariakoo una uhakika wa kuamka na kazi yako asubuhi siyo huu ujinga wa kupewa vyeo.
 
Wasalaam.

Baada ya sintofahamu ya baadhi ya Wateule kukataa kuapishwa katika nafasi waliyoteuliwa, kumezuka na maswali na minong'ono mingi isiyo na sababu.

Lakini, yote haya yamesababishwa na kuwepo kwa mawasiliano hafifu baina ya upande wa uteuzi na yule aliyeteuliwa. Kwa akili zangu, nilidhani mhusika hujulishwa kupata nafasi hiyo kabla ya majina kutangazwa hadharani.

Kinachoonekana ni kuwa, mamlaka ya uteuzi yamejitwisha haki ya kuamua hatma ya mteuliwa. Wamesahau kuwa watu wana mipango yao mingi, majukumu yao na wengine hawana mpango wa kushikilia wadhifa za aina hiyo.

Lakini pia, aina hiyo ya uteuzi pasipo kushirikisha pande zote mbili kunaaibisha mamlaka haswa ofisi ya Rais. Mtu kukataa nafasi ya uteuzi ni kuonesha kutokuwa makini kwa wale wote wanaohusika na uteuzi. Na kwa kuwa wateuliwa waliteuliwa na Mh Rais, basi inayoaibika ni ofisi husika.

Kukataa pia nafasi ya uteuzi si jambo geni. Ilishatokea na itatokea tena. Polisi na mamlaka zingine ziheshimu maamuzi ya mtu kwa hiyari. Kuwakamata na kuwahoji kisa tu wamekataa uteuzi, huku wakijua wazi kuwa mhusika ana nafasi nyingine ni kutompa mtu haki ya kujiamulia mambo yake.

Wasaidizi wa Rais kwa hapa wamefeli kwa kiwango kikubwa. Na ingelikuwa vema kama watareconcile na upande mwingine kabla ya kufikia maamuzi ya kuteua.

Nawasilisha.
Sisiemu ya samia imejaa upumbavu mtupu unampaje mtu uongozi pasipo kutaka au yeye mwenyewe kuona ana weza kuongoza au samia anadhani kuwa kiongozi ni kujaza vyoo tu
 
Kuna mwamba alimkatalia Magufuli
☝🏾
Wakati wa Magufuli yule alikuwa mfano wa kichaa so alikuwa anaogopwa na kila mtumishi na hii ilikuwa inawarahisishia wateuliwa ktk utendaji wao ila leo mtu anateuliwa kwenda kusimamia watu waliokaa kipigaji pigaji anajua kabisa hataheshimika maana wameshindwa kumuheshimu kiongozi wao mkuu mwisho mteuliwa anatupwa nje ya ulingo kwa aibu kisa kushindwa kusimamia watu walioshauriwa na boss wao kula kwa urefu wa kamba zao.

Teuzi za kiserikali bongo bora mtu ukawe winga Kariakoo una uhakika wa kuamka na kazi yako asubuhi siyo huu ujinga wa kupewa vyeo.
 
Back
Top Bottom