Kwani makonda ndiye mkuu wa divisheni/idara zote za serikali? Huko wanakofanya kazi hawo watumishi wa umma hakuna wakuu wao wanaowaongoza kutimiza majukumu yao au unataka kusema nini mkuu?Duh! Kwa hiyo,wafanyakazi serikalini wabembelezwe kufanya kazi zao? Wakijisikia walale,mwisho wa mwezi walipwe.
Kwa nini wafanye kazi kwa woga? Wakitimiza wajibu wao,nani atawafatilia kuwawajibisha!?
Hili nililisema tangu zamani kwamba Makonda ni timu Sukuma Gang na kwamba baada ya kupenya kuingia uongozini, ataanza mchakato wa kumuangusha mama kupitia chawa wengi wa kundi hili waliomo serikalini. Ikifika 2025 tayari kundi hili litakuwa limeota mizizi ya kutosha. Halitaweza kurudishwa nyuma wala kutishwa kwa vyovyote vile na timu ya mama.
Sasa ni wakati muafaka timu ya mama imshughulikie mapema kiongozi huyu wa Sukuma Gang kabla hajaleta madhara kwa chama, serikali na kundi la mama. Wasipoziba ufa mapema, watakuja kujenga ukuta.
Safi sana alikuwa akimjibu Makonda.
Tupe mfano, mipango ya serikali ujadiliwa kwenye baraza la mawaziri, je mwenezi uwepo?Haujui unachokitaka: unampinga mwenezi halafu unamalizia kuomba utatuzi wa anayoyapigania mwenezi!
Kwahiyo unashauri amwachie Makonda 2025?Tatizo mnapingana na ukweli, Magufuli ndiye aliyeleta uhai wa chama na kazi yake imeonekana. Fikiria mtu yupo kaburini ila bado anawapa shida nyie mlio hai.
Mama hana cha kutuambia, amepwaya sana na hakubaliki.
Rais anahitaji msaada gani?! Huyo Makonda sasa anatoa msaada gani Kwa Rais?Mkiongozwa na chuki Makonda atawanyoosha kwelikweli...
Tatizo ninaloliona hapa kuna watu walitamani kumpamgia raisi, nani ashirikiane naye na nani amwache...
Kitu unachopaswa kujua nyinyi mungekuwa na uwezo wa kumsaidia raisi, angewateua nyinyi badala ya huyo munayemchukia ...
Kutokuteuliwa ninyi ni ishara kwamba hamuna uwezo wowote wa kumsaidia raisi na hamkubaliki kwa wananchi...
1. Mimi nimeongelea aliesema woga wa wafanyakazi kuwajibishwa.Kwani makonda ndiye mkuu wa divisheni/idara zote za serikali? Huko wanakofanya kazi hawo watumishi wa umma hakuna wakuu wao wanaowaongoza kutimiza majukumu yao au unataka kusema nini mkuu?
Kabeeesa. Time is the best answer
Huyu ndiyo tunamtaka kwasasa na si kesho. Anayemchukia ni mjinga na mwenye ajenda zake za siri. Unamchukia vipi mtu, tena kiongozi wa chama tu aliyejitoa kutetea na kutatua kero za wananchi, tena wanyonge. Rais kashindwa, makamu kashindwa, waziri mkuu kashindwa, naibu waziri mkuu kashindwa, mawaziri wameshindwa, naibu waziri wameshindwa, wakuu wa mikoa wameshindwa, wakuu wa wilaya wameshindwa, RAS, DAS hovyo tu. Usidhani kama sisi ni wajinga kujaa kwenye mikutano yake. Ana kitu huyu kijana na anafaa kwasasa kwani amesaidia watu wengi mno. Vipi kama angekuwa na mamlaka ya kikatiba sasa? Go Makonda gooooo!Lakin saa inakuja,nayo sasa ipo,ambapo mtavuna mnachokipanda, kwa jicho la mbali mnamuona kama anakijenga chama, katika jicho la upeo wa roho anadhoofisha chama, bosi wake na Viongozi wakuu wengne na kujijenga yeye.
Anajisafisha na kujitanabaisha alikuwa ni mtu mwema, kiongozi shupavu na jasiri. Mpaka sasa anamuheshimu mwendazake na ndiye bosi wake wa moyo wa mda wote. Ndo mana anaishi falsafa zake na ndio anazohubiri, falsafa hizo zinalengo la kuwaibua wale walompenda na kufanya aonekane yeye ndo mrithi sahihi, Wale walompenda Mwendazake sasa watampenda huyu kwa heshima na kweli na watamuimba kama shujaa wao na hakuna atakae weza kuzuia.
Mama Falsafa yako ilitanabaisha watumishi wa serikali wasifanye kazi kwa woga, bali kwa weledi na nidhamu,ila falsafa inayohubiria majukwaani kwa sasa ni hofu na umaarufu wa mtu.kwa vile watumishi wengi wa serikali ni waoga, wamejengwa kuogopa wanasiasa,zile zama za woga zinarudi, na hakika watumishi na wateule wako wote wanamuogopa huyu kuliko kiongozi yeyote ktkt taifa hili, huku akijijenga kwa wale wananchi mnaowaita walalahoi na wanyonge wamuone ndiye kiongozi pekee mwenye udhubutu na kukemea maovu.
Hakika nakwambia ,watanzania wanataka kiongozi anayesema na kutenda, anayeonya na kukemea kweli kweli, anayewajibisha watumishi wa umma wazembe na wabadhirifu wa mali za umma na hii ndio beat anayotembea nayo Mwenezi.
Asipofundwa vizuri atakufarakanisha na wale uliokuwa umeanza kupatana nao,haki uliyoitengeneza na kuipigania itapotea. Mhe raisi binafsi naamini unafanya kazi nzuri sana na nakupenda kwa dhati kwa sababu unapenda haki na usawa kwa wote lakin nakuomba usiamni sana hawa wasaidizi wako,wengi wao wanaangalia vyeo na matumbo yao,usiwakumbatie sana kana kwamba bila wao nchi haitaenda,kuna wateule wako wanakuharbia halafu wanakusifia wakiamn utafurahishwa na hizo sifa.maagizo yako hawayatekelezi kabisa na wanafanya yao kwa mgongo wako.
Ole wenu msipotafta namna ya kumfunda, ipo siku yaja hamtaweza kuyazuia mafuriko, Kama lengo ni kumjenga kuwa kiongozi basi ni vema mkamjenga sawasawa kwa sababu kama atabadilika ni kiongozi mwenye udhubutu na huenda akaleta Mabadiliko katika nchi, anahulka ya kupenda Maisha ya kifahari lakini anachukia wengine wanaoyaishi, anapenda mamlka na kuamuru lkn hapendi anayemzidi mamlaka, anapenda kusaidia watu na anataka ajitanabaishe ni yeye pekee mwenye huruma na moyo wa kusidia watu, anapenda kuonekana ni mcha Mungu kuliko wanaosimama madhabahuni.
Maisha yameguwa magumu sana mtaani,Mama sekta bnafsi zinazofanya kazi na serikali hasa zinazolipwa na pesa kutoka HAZINA hazilipwi kwa wakati na kusababisha baadhi kuzorota au kufa hasa za wazawa,umeme umekuwa ni tatizo na kero kubwa sana kwa wananchi,watu wanategemea umeme kufanya shughuli zao zinazowaingizia kipato na kuendesha Maisha yao lkn umeme umekuwa ukikatika kila uchao jambo linalowafanya wananchi kuanza kuchukia serikali.zaidi Viongozi wa serikali wengi hasa wateule wako wanaishi Maisha ya kifahari na bila shaka kero ya umeme kwao haiwapati
Iwe jumapili njema kwenu,Maandiko yanasema ‘basi sasa msiwe watu wa kudharau,vifungo vyenu msije vikakazwa,maana nimeskia kwa Bwana,Bwana wa majeshi,Habari ya hukumu itakayotimizwa,nayo imekusudiwa.
mnailazimisha furaha, ingawa moyoni mna majonzi na hakuna wa kuwafuta machozi...
Anaharibu wapi, acheni kudanganya watu nyie... Msimtishe Mh Rais wetu bila sababu. Mnadhani wenyewe hamjui vizuri. Tatizo, bana, mafisadi yakishaona kuna hali ya hatari, yanaanza kujitengenezea barrier ya kutoguswa. Hata kama anatembelea nyota na Magufuli, kuna tatizo gani? Wakati katika nyota ile, hata mama yetu Dr SSH alikuwemo. Mmeshaona chama kinajirekebisha na kuwa kikali, mmeanza kulialia. Wacha watu wachape kazi, iwe lolote lakini wananchi wanahitaji matokeo: maji, umeme, bei nafuu, mfumuko wa bei chini, mafuta chini, sukari chini, n.k. Sijui unaelewa. Hayo mengine ni propaganda zako za kutunga.
Hivi huu ni mgao kukatika katika hovyo kwa umeme?Hiyo falsafa ya mama ya kubembelezana ndio imetuzalishia mgao wa umeme uliovunja rekodi kwa kuwepo muda mrefu.
Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Hakuwa anazungumzia issue za Makonda bana...mbona kwa Makonda alijibu vizuri..acheni kugombanisha