Pre GE2025 Ipo siku yaja kwa huyu mwenezi msipomfunda CCM na Rais Samia mtavuna mabua

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Duh sasa nijisikie amani kujiita mtanzania kwa lipi mkuu katika hii nchi?
 
Duh! Kwa hiyo,wafanyakazi serikalini wabembelezwe kufanya kazi zao? Wakijisikia walale,mwisho wa mwezi walipwe.
Kwa nini wafanye kazi kwa woga? Wakitimiza wajibu wao,nani atawafatilia kuwawajibisha!?
Suala la nidhamu ya hiari limefeli sasa si bora wawe na nidhamu ya uoga tu.
 
Sidhani kama ulimaanisha
Tuombe Mungu,na iwe hivo kama ulvotolea huo mfano.
 
hawa ni watu wawili tofauti
falsafa mbili tofauti
 
Sidhan, mwenezi hafanyi Kwa ajil ya hilo gang, he is working for His own empire.
 
Haujui unachokitaka: unampinga mwenezi halafu unamalizia kuomba utatuzi wa anayoyapigania mwenezi!

Hakika,Inabidi tumpe mamlaka kamili
 
Makonda kaachiwa nchi Mama anaswampa ughaibuni akirudi anakuwa kizi city na kuondokea huko kurudi ughaibuni.....nchi haina mwenye uchungu nayo....Jeshi linalalamika Rais analalamika....mamlaka zinalalamika wana chi wanalia na kulalamika
 
Naunga Mkono hoja....

Kwa kweli akisimama 2025, CCM watakuwa na kazi nyepesi sana maana Watanzania wengi (ukiondoa mafisadi wachache na yenye nguvu ya fedha), tunawapenda watu kama Paul C. Makonda.

Hii ni kwa kuwa watendaji wetu hawana uzalendo wala uadilifu wa kufanya pasipo kusimamiwa.
Makonda ni msimiaji mzuri sana.

Kama hatokuwa Rais 2025, basi apewe hata Uwaziri Mkuu.
Naiona Tanzania mpya chini ya Makonda..
 
Hata Kama ni mtu Miaka 64 ni Mingi Hata akili Itakuwa imeanza kuchoka na kupungua uwezo wa kufikiria na kukabili changamoto .
Miaka 62 sio mingi au hapo akili itakuwa haijanza kupungua na kuchoka?Najua unajua namzungumzia nani.Au kipimo hicho ni baadhi ya watu tu?

Ingekuwa kisayansi uwezo wa akili unapungua tusingekuwa na viongozi wenye umri zaidi ya huo duniani.
 
Hakuwa anazungumzia issue za Makonda bana...mbona kwa Makonda alijibu vizuri..acheni kugombanisha
Hiyo ni clip ya muda mrefu kuhusu bei elekezi ya mazao.Haina uhusiano wowote na ziara ya Makonda.Ukiona watu wameanza kutetemeka jua kuna linalowatetemesha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…