Tetesi: Iran na uturuki kuungana kukabiliana na vikwazo vya marekani

Tetesi: Iran na uturuki kuungana kukabiliana na vikwazo vya marekani

kimsboy

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
9,846
Reaction score
20,319
Iran na Uturuki zahimizwa kuunganisha nguvu zao kupambana na Marekani
Mkuu wa chama cha Vatan cha Uturuki amesema kwamba kuna wajibu kwa Ankara na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuunganisha pamoja nguvu zao kupambana na vikwazo vya Marekani dhidi ya nchi hizo mbili.
Dogu Perinçek amesema hayo leo na kuongeza kuwa, Iran ni mshirika wa kiistratijia na ni jirani mwaminifu kama ambavyo ndiyo nchi inayoidhaminia Uturuki sehemu kubwa ya mahitaji yake ya nishati na ni kwa sababu hiyo ndio maana ushirikiano wa Ankara na Tehran ukawa ni jambo la dharura na muhimu sana katika kukabiliana na ubeberu wa Marekani.
Mkuu huyo wa chama cha Vatan cha Uturuki ameongeza kuwa, ushirikiano wa kiistratijia baina ya Tehran na Ankara na ushirikiano mzuri wa nchi hizo mbili katika suala la Syria, bila ya shaka yoyote ni jibu thabiti kwa vitisho vya Marekani.
Vile vile amesema, serikali ya Uturuki inapaswa kuachana mara moja na siasa za kuipiga vita Syria na badala yake ifanye juhudi za kurejea uhusiano na kutoa mkono wa urafiki kwa Damascus kama njia ya kuimarisha ushirikiano uliopo hivi sasa baina ya China, Russia na Iran.
Hivi karibuni Marekani iliziwekea vikwazo vya kidhulma Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki ikiwa ni kuzidi kuwathibitishia walimwengu ubeberu wake.


MY TAKE: NAONA UTURUKI ASHAANZA KUJITOA TARATIBU UPANDE WA MAGHARIBI JUZI KAOMBA AUNGWE KWENYE KUNDI LA BRICS
4bn2bd80ebc216wpr9_800C450.jpg
 
Mturuki ni m-lofa na mpumbavu kama anataka nchi yake igawanyike mara 100 irudi Anatolia, Seljuk, Byzantine na nyinginezo yeye aleta ujinga tu.

Kosa lake alitungua ndege ya mrusi, mrusi akambinye pumbuz na plies akaenda kwa mrusi sasa Trump anamuonyesha kazi huwezi kumkimbia baba yako ukalelewe na baba wa kambo na anajichanganya zaidi anapoenda kwa Iran. Wakati wa vita ya pili aliunda urafiki na Hitler lakini tunajua yaliyompata. Inabidi mturuki asicheze na moto au tushuhudie Iraq nyingine na syria nyingine uturuki

Mimi namuonea huruma jiwe na reli yake ya sgr hewa maana erdogan anakamuliwa mavi bado yeye jiwe atanyonywa mkojo na Trump kwa vikwazo. Ila ndo hivyo jiwe hana bahati poor kiongozi mtarajiwa wa malaika
 
Ni wakati sasa wa mataifa mengine kuungana dhidi ya kitisho kutoka Marekani
 
Trump nimshamba wa madaraka ndio tabu kumpa mtu uongozi wa nchi wakati hata uongozi ngazi za chini hajawahi,nchi akipishana nayo kidogo vikwazo hata bush hakuwa hv.
 
uturuki wa walimdaka yule pastor ili kumtumia kama kadi ya kumpata gullen ila kwa bahati mbaya hesabu zimegoma then wamemkuta trump naye ni kiburi na mpenda sifa km edorgan so kazi ipo, walizoea obama walikua wakimponda sana na kumsema kila walivyotaka kila mtu alikua akiivimbia marekan ila huyu wa sasa kazi ipo maana anaanza kukuchamba tweeter, ana uwezo wa kubishana na watu mia kwa wakati mmoja halafu anapenda sifa mnoooo, leo anamsifia putin kesho anamtangazia vikwazo lukuki, hapa kwa trump wajipange
 
uturuki wa walimdaka yule pastor ili kumtumia kama kadi ya kumpata gullen ila kwa bahati mbaya hesabu zimegoma then wamemkuta trump naye ni kiburi na mpenda sifa km edorgan so kazi ipo, walizoea obama walikua wakimponda sana na kumsema kila walivyotaka kila mtu alikua akiivimbia marekan ila huyu wa sasa kazi ipo maana anaanza kukuchamba tweeter, ana uwezo wa kubishana na watu mia kwa wakati mmoja halafu anapenda sifa mnoooo, leo anamsifia putin kesho anamtangazia vikwazo lukuki, hapa kwa trump wajipange
Hahahaha eti anaanza kukuchamba Tweeter
 
Panya wakubwa wawili walionenepeana wameunganisha nguvu ili kupambana na paka mmoja mwenye njaa kali, umoja ni nguvu ngoja tusubiri labda panya watashinda maana paka hana nguvu kwa sababu ya njaa
 
Je hao panya nyuma yao kuna nani usije
Panya wakubwa wawili walionenepeana wameunganisha nguvu ili kupambana na paka mmoja mwenye njaa kali, umoja ni nguvu ngoja tusubiri labda panya watashinda maana paka hana nguvu kwa sababu ya njaa
usishangae nyuma ya hao panya kuna simba anayewambia chokonoeni nipo nyuma yenu kuwasaidia, nyie anzishie kisha niachieni menyewe
 
Kipofu na kiwete wanapoungana kumkabili mayweather..[emoji848][emoji848][emoji848][emoji57][emoji57]
 
Ataumizwa kiuchumi tu atakuwa kama Ugiriki
 
Back
Top Bottom