#COVID19 Iran yarudisha chanjo za Corona 'zilizotengenezwa Marekani'

#COVID19 Iran yarudisha chanjo za Corona 'zilizotengenezwa Marekani'

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1645606329658.png

Iran imerudisha dozi 820,000 za chanjo ya virusi vya corona iliyotolewa kama msaada na Poland kwa sababu ilitengenezwa Marekani.

Televisheni ya taifa siku ya Jumatatu ilimnukuu Mohammad Hashemi, afisa wa wizara ya afya, akisema kwamba Poland ilitoa takriban dozi milioni moja za chanjo ya AstraZeneca ya Uingereza na Uswidi kwa Iran.

"Lakini chanjo zilipofika Iran, tuligundua kuwa dozi 820,000 kati ya hizo ambazo ziliagizwa kutoka Poland zilitoka Marekani," alisema.

Waziri wa afya wa Iran, Bahram Einollahi, aliandika katika barua kwa mkuu wa mamlaka ya forodha kwamba licha ya uhakikisho wa Poland,chanjo hizo zilitoka kutoka "chanzo kisichoidhinishwa".

Alisema watoa huduma wa Poland wameahidi "kubadilisha chanjo hizo na zile kutoka kwa chanzo kilichoidhinishwa" na kurudisha chanjo zilizorejeshwa.

Mnamo 2020, Kiongozi Mkuu wa Iran Ali Hosseini Khamenei, ambaye ndiye mwenye usemi wa mwisho juu ya maswala yote ya serikali, alikataa uwezekano wowote wa chanjo za Marekani au Uingereza kuingia nchini, na kuziita "haramu".

Iran sasa inaagiza tu chanjo za Magharibi ambazo hazijazalishwa Marekani au Uingereza.
 
Iran imerudisha dozi 820,000 za chanjo ya virusi vya corona iliyotolewa kama msaada na Poland kwa sababu ilitengenezwa Marekani.

Televisheni ya taifa siku ya Jumatatu ilimnukuu Mohammad Hashemi, afisa wa wizara ya afya, akisema kwamba Poland ilitoa takriban dozi milioni moja za chanjo ya AstraZeneca ya Uingereza na Uswidi kwa Iran.

"Lakini chanjo zilipofika Iran, tuligundua kuwa dozi 820,000 kati ya hizo ambazo ziliagizwa kutoka Poland zilitoka Marekani," alisema.

Waziri wa afya wa Iran, Bahram Einollahi, aliandika katika barua kwa mkuu wa mamlaka ya forodha kwamba licha ya uhakikisho wa Poland,chanjo hizo zilitoka kutoka "chanzo kisichoidhinishwa".

Alisema watoa huduma wa Poland wameahidi "kubadilisha chanjo hizo na zile kutoka kwa chanzo kilichoidhinishwa" na kurudisha chanjo zilizorejeshwa.

Mnamo 2020, Kiongozi Mkuu wa Iran Ali Hosseini Khamenei, ambaye ndiye mwenye usemi wa mwisho juu ya maswala yote ya serikali, alikataa uwezekano wowote wa chanjo za Marekani au Uingereza kuingia nchini, na kuziita "haramu".

Iran sasa inaagiza tu chanjo za Magharibi ambazo hazijazalishwa Marekani au Uingereza.

BBC Swahili
 
Woyoooooooooo kumekucha kumekucha [emoji91][emoji91][emoji91][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]

Raha sana
 
Huu ni ujuha sasa, sidhani kama dini imefundisha hivyo,
Unaangamia kwa kukosa maarifa tu
 
Hayo Ni masuala ya kisiasa dini inahusika vipi hapo !?
Dini ni mfumo kamili wa maisha,
Siasa, michezo, kazi na kila ujualo linasimamiwa na dini,
Ukikosa dini umekosa kila kitu
Na ukiwa na dini umepata kila kitu
 
Back
Top Bottom