Iraq: Wanaharakati wapinga Sheria ya umri wa ndoa kuanzia miaka 9

Iraq: Wanaharakati wapinga Sheria ya umri wa ndoa kuanzia miaka 9

BabaMia

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2024
Posts
270
Reaction score
554
Sheria mpya inayopendekezwa nchini Iraq inayolenga kupunguza umri wa ridhaa ya Ndoa kwa Wanawake hadi miaka tisa, jambo linalolenga kuruhusu Wanaume Nchini humo kuoa Wanawake wakiwa na Umri mdogo

imepingwa vikali na Wanaharakati Nchini humo wakidai kuwa ni yenye kuhalalisha udhalilishaji wa kijinsia kwa Watoto ambapo pia inaelezwa kuwa Sheria hii inataka kufuta moja ya sheria bora zaidi za haki za Wanawake katika Mashariki ya Kati, ambayo inawapa Wanawake haki za kudai talaka, malezi ya Watoto, na urithi.

Wanaharakati na baadhi ya Wabunge wa Iraq wanapinga kwa nguvu pendekezo hili, wakisema kuwa litakuwa janga kwa haki za Wanawake na Watoto, Raya Faiq, ambaumye ni Mratibu wa Makundi ya kupinga sheria hii, alisema kuwa pendekezo hili litaruhusu Ndoa za Watoto na kuminya haki za Familia za kukataa Ndoa hizo huku akiweka wazi kwamba sheria hii ingekuwa ni njia ya kisheria ya kuruhusu udhalilishaji wa kijinsia kwa Watoto.

Pia, soma: Bunge la Iraq lajadili mpango wa kuruhusu ndoa za utotoni, kushusha umri wa mabinti kuolewa hadi miaka 9

Aidha Serikali ya Iraq, kwa upande wake, inadai kuwa mabadiliko haya yatasaidia kufuata sheria za Kiislamu, wakisema kwamba yatawalinda Wasichana kutoka kwa mahusiano yasiyofaa lakini hata hivyo, Wanaharakati wanasisitiza kwamba sheria hii itawarudisha nyuma Wanawake na Watoto kwa miaka mingi.

Sheria hii ilipitishwa kwa mara ya pili Bungeni mnamo Septemba 16, 2024, na inatarajiwa kupitishwa tena kutokana na msaada kutoka Vyama vya Shia Nchini humo lakini hata hivyo inaelezwa si Vyama vyote vya Shia vinaunga mkono sheria hii, na bado kuna juhudi kubwa za kupinga.

Mapambano haya ni muhimu kwa Wanawake wa Iraq, ambao wanapinga vikali hatua hii, wakiitaka Serikali kuepuka kurejesha nyuma haki za msingi za Wanawake na Watoto.
 
Sheria mpya inayopendekezwa nchini Iraq inayolenga kupunguza umri wa ridhaa ya Ndoa kwa Wanawake hadi miaka tisa, jambo linalolenga kuruhusu Wanaume Nchini humo kuoa Wanawake wakiwa na Umri mdogo imepingwa vikali na Wanaharakati Nchini humo wakidai kuwa ni yenye kuhalalisha udhalilishaji wa kijinsia kwa Watoto ambapo pia inaelezwa kuwa Sheria hii inataka kufuta moja ya sheria bora zaidi za haki za Wanawake katika Mashariki ya Kati, ambayo inawapa Wanawake haki za kudai talaka, malezi ya Watoto, na urithi.

Wanaharakati na baadhi ya Wabunge wa Iraq wanapinga kwa nguvu pendekezo hili, wakisema kuwa litakuwa janga kwa haki za Wanawake na Watoto, Raya Faiq, ambaumye ni Mratibu wa Makundi ya kupinga sheria hii, alisema kuwa pendekezo hili litaruhusu Ndoa za Watoto na kuminya haki za Familia za kukataa Ndoa hizo huku akiweka wazi kwamba sheria hii ingekuwa ni njia ya kisheria ya kuruhusu udhalilishaji wa kijinsia kwa Watoto.

Aidha Serikali ya Iraq, kwa upande wake, inadai kuwa mabadiliko haya yatasaidia kufuata sheria za Kiislamu, wakisema kwamba yatawalinda Wasichana kutoka kwa mahusiano yasiyofaa lakini hata hivyo, Wanaharakati wanasisitiza kwamba sheria hii itawarudisha nyuma Wanawake na Watoto kwa miaka mingi.

Sheria hii ilipitishwa kwa mara ya pili Bungeni mnamo Septemba 16, 2024, na inatarajiwa kupitishwa tena kutokana na msaada kutoka Vyama vya Shia Nchini humo lakini hata hivyo inaelezwa si Vyama vyote vya Shia vinaunga mkono sheria hii, na bado kuna juhudi kubwa za kupinga.

Mapambano haya ni muhimu kwa Wanawake wa Iraq, ambao wanapinga vikali hatua hii, wakiitaka Serikali kuepuka kurejesha nyuma haki za msingi za Wanawake na Watoto.
wAISLAMU JOONI HAPA KUNA HOJA. FaizaFoxy NA KUNDI LAKO JF MISIMAMO MIKALI
 
Ni upuuzi mkubwa kupitisha hiyo sheria ya hovyo kiasi hicho
 
Mathayo 7
15 Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?

17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.

18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.

19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.
 
Hivi ni kweli kuwa Mtume Mohamed S. A. S. Aliwahi kuoa mtoto wa miaka 9. ??

Mbona inaogopesha ??

Unaanzaje kumkalia kinenani mtoto Mdogo hivyo jamani ??

🙆‍♂️🤦‍♀️😭
 
Mathayo 7
15 Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?

17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.

18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.

19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.
Hapo bibilia ili jaribu kumhalalisha Paulo kumbe inamtukanisha kabisa. Alitaka asema yeye ni Mtume wakati hakuna aliye mpa utume sio Mungu wala sio Malaika wa Mungu kamfikishia ujumbe. Sa huo utume fake ni wake 😆
 
Hivi ni kweli kuwa Mtume Mohamed S. A. S. Aliwahi kuoa mtoto wa miaka 9. ??

Mbona inaogopesha ??

Unaanzaje kumkalia kinenani mtoto Mdogo hivyo jamani ??

🙆‍♂️🤦‍♀️😭
Hizo za miaka 9 mlipata wapi zile hadith zilizo tungwa na wakrisito na wayahudi kwa kudai ni za Bukhari na wengine, kama alivyo tunga paulo kitabu cha kwaya na kutoa tolea jipya kwani gazeti vitabu vya Mungu😄
 
Mtoto wa miaka 9 anajua kazi ya wembe ni kuchongea penseli na kunyolea kipara tu basi . Anajua mtoto ananunuliwa,anajua kuchamba ni haja kubwa tu.
 
Hizo za miaka 9 mlipata wapi zile hadith zilizo tungwa na wakrisito na wayahudi kwa kudai ni za Bukhari na wengine, kama alivyo tunga paulo kitabu cha kwaya na kutoa tolea jipya kwani gazeti vitabu vya Mungu😄
Kwani unazani hao wairani msingi wa madai hayo unatokana na nini ?
Ni sababu ni sunnah hata Mtume alafanya hivyo.
Lakini ndipo sasa Watu tunabaki na mshangao mkubwa! 🤔🤔
 
Kuna muajemi anaunga mkono hoja ila ukimwambia nataka nimuoe binti wako wa miaka hiyo hakuelewi kabisa.
 
Back
Top Bottom