Iringa: Ajinyonga baada ya kuachana na mkewe

Iringa: Ajinyonga baada ya kuachana na mkewe

Boran Jakutay

Senior Member
Joined
Apr 8, 2023
Posts
110
Reaction score
259
Kijana Carlos Mwamilinga aliyekuwa na miaka 37, amekutwa amejinyonga kwa kamba katika chumba alichokuwa akiishi eneo la Njiapanda ya Mtwivila kwa kile kinachodhaniwa kuwa ni kutingwa na mawazo kupita kiasi kutokana na kuachana na mkewe mwezi mmoja uliopita.

Marafiki na majirani wa marehemu, wamebainisha kwamba, kijana huyo baada ya kuachana na mkewe, akaanza kunywa pombe kali huku akionekana mwenye mawazo sana.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Idunda, Elisius Mbilinyi, amesema sababu ya moja kwa moja ya kijana huyo kujinyonga haijafahamika, huku akibainisha kwamba marehemu alikuwa akiishi peke yake baada ya kuachaba na mkewe.

Chanzo: Azam TV
 
Sasa anajinyonga vipi tenaa huyu nae akati alikua anafanya mapenzi ambayo nature inataka?? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Na watajinyongaa sanaa, mbna badooo. Lol
 
Batu batajimilikisha kihalali sasa bila hofu ya revenge..mpeni maua yake bizinenga ikaa hiyo jomba
 
Mmmh curses still marinates in Iringa kwani watu bado wanawaza mapenzi kiasi hicho.
 
Sasa anajinyonga vipi tenaa huyu nae akati alikua anafanya mapenzi ambayo nature inataka?? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Na watajinyongaa sanaa, mbna badooo. Lol
Geita wameshatoa mfano wa kushughulika vizuri na watu kama ninyi. Zamu yako itafika.
 
Tuwe na akiba ya maneno kwa wenzetu wanaopatwa na Visanga vya hivi.

Binafsi namshukuru tu Mungu kuwepo mpk leo, mara kadhaa nimepitishwa ktk nyakati ngumu km hz na Mke.

Sio mara zote ni rahisi kuacha!
Sio mara zote ni rahisi kuanza upya!
 
Sasa anajinyonga vipi tenaa huyu nae akati alikua anafanya mapenzi ambayo nature inataka?? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Na watajinyongaa sanaa, mbna badooo. Lol
Inawezekana huyo ndiyo mpenzi wake wa kwanza,na ndiyo mara yake ya kwanza kuumia kimapenzi

Ova
 
Inawezekana huyo ndiyo mpenzi wake wa kwanza,na ndiyo mara yake ya kwanza kuumia kimapenzi

Ova
Na hilo ndo tatizo liliompa mawazo ,mambo ya kuwa na mwanamke mmoja akikutia tu stress huna pa kwenda kupumzika Kwa haraka
 
Kijana Carlos Mwamilinga aliyekuwa na miaka 37, amekutwa amejinyonga kwa kamba katika chumba alichokuwa akiishi eneo la Njiapanda ya Mtwivila kwa kile kinachodhaniwa kuwa ni kutingwa na mawazo kupita kiasi kutokana na kuachana na mkewe mwezi mmoja uliopita.

Marafiki na majirani wa marehemu, wamebainisha kwamba, kijana huyo baada ya kuachana na mkewe, akaanza kunywa pombe kali huku akionekana mwenye mawazo sana.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Idunda, Elisius Mbilinyi, amesema sababu ya moja kwa moja ya kijana huyo kujinyonga haijafahamika, huku akibainisha kwamba marehemu alikuwa akiishi peke yake baada ya kuachaba na mkewe.

Chanzo: Azam TV
Hiyo mitaa si ndio ya kujinyongea?
 
Geita wameshatoa mfano wa kushughulika vizuri na watu kama ninyi. Zamu yako itafika.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] watekelezaji wenyewe ndo hawa wanaanza kujiua wao wenyewe, watanifikia mie lini hiyooo??? Poleeeee weee
 
Inawezekana huyo ndiyo mpenzi wake wa kwanza,na ndiyo mara yake ya kwanza kuumia kimapenzi

Ova
Na badoo watajinyongaa mnooo tena na tena.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ukiona mwanaume hataki kuachwa,jua huyo anamtegemea mke wake kiuchumi asilimia Mia moja.Japo hawezi kuacha tabia zinazomkera mke wake lakini bado anamgang'ania mke wake asiondoke.Mke akitaka kuondoka anamtishia akiondoka atamuua.Mwanaume lazima uwe mwanaume ambaye anaweza kuishi katika hali zote za ndoa. I mean married or divorced.
 
Back
Top Bottom