Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,336
- 4,731
MGOMBEA urais wa chama cha ADC, Queen Sendiga adai kupigwa makofi na watu wasiojulikana na kuvunjiwa kioo cha gari lake akiwa katika maeneo ya stendi kuu ya zamani ya Manispaa ya Iringa kuendelea na mikutano yake ya hadhara ya kampeni .
Akizungumza mara baada ya tukio hilo leo mgombea huyo alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 10 jioni wakati akielekea katika viwanja vya Stendi kuu ya zamani ya mabasi yaendayo mikoani eneo ambalo pia chama cha mapinduzi (CCM) walikuwa na mkutano wa kampeni za mgombea wa udiwani kata ya Kitanzini Miyomboni .
Alisema kuwa jana kwa mujibu wa ratiba alikuwa ana mikutano yake ya kampeni katika mkoa wa Iringa katika halmashauri ya Manispaa ya Iringa na asubuhi baada ya kuwasili Iringa alikutana na matangazo ya mgombea udiwani na ndipo alipotoa taarifa tume ya taifa ya uchaguzi kulalamikia suala hilo
" Mimi kabla ya kuwasilisha malalamiko mkurugenzi wa tume ya Taifa ya uchaguzi Bwana Mahela kuelezea vurugu ambazo nimekutana nazo jimbo la Iringa mjini niliendelea na ratiba zangu za kampeni za kuzunguka mitaano kama sokono na maeneo mengine kuomba kura japo tayari mgombea wangu wa nafasi ya ubunge jimbo la Iringa mjini Daud Masasi ambae pia ni kamishina wa ADC mkoa wa Iringa aliwasilisha malalamiko hayo kwa msimamizi wa uchaguzi jimbo la Iringa mjini" alisema
Kuwa ameshangazwa na kusikitishwa na tukio la vijana kuvamia gari lake la matangazo na kuvunja kioo cha mbele cha gari hilo na wengine kumzingira na kumpiga makofi yeye wakati akihoji sababu ya gari lake kuvunjwa kioo wakati akielekea eneo hilo katika mkutano.
Hata hivyo alisema kuwa katika vurugu hizo gari la matangazo na vijana waliokuwepo katika gari hilo ndio ambao wameshambuliwa sana na yeye wameishia kumsukuma na kumzaba makofi wakati wa mvutano huo .
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Juma Bwire alipotafutwa na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu alisema hajapata taarifa hizo zaidi ya kusikia kutoka kwa mwandishi hivyo anafuatilia
Akizungumza mara baada ya tukio hilo leo mgombea huyo alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 10 jioni wakati akielekea katika viwanja vya Stendi kuu ya zamani ya mabasi yaendayo mikoani eneo ambalo pia chama cha mapinduzi (CCM) walikuwa na mkutano wa kampeni za mgombea wa udiwani kata ya Kitanzini Miyomboni .
Alisema kuwa jana kwa mujibu wa ratiba alikuwa ana mikutano yake ya kampeni katika mkoa wa Iringa katika halmashauri ya Manispaa ya Iringa na asubuhi baada ya kuwasili Iringa alikutana na matangazo ya mgombea udiwani na ndipo alipotoa taarifa tume ya taifa ya uchaguzi kulalamikia suala hilo
" Mimi kabla ya kuwasilisha malalamiko mkurugenzi wa tume ya Taifa ya uchaguzi Bwana Mahela kuelezea vurugu ambazo nimekutana nazo jimbo la Iringa mjini niliendelea na ratiba zangu za kampeni za kuzunguka mitaano kama sokono na maeneo mengine kuomba kura japo tayari mgombea wangu wa nafasi ya ubunge jimbo la Iringa mjini Daud Masasi ambae pia ni kamishina wa ADC mkoa wa Iringa aliwasilisha malalamiko hayo kwa msimamizi wa uchaguzi jimbo la Iringa mjini" alisema
Kuwa ameshangazwa na kusikitishwa na tukio la vijana kuvamia gari lake la matangazo na kuvunja kioo cha mbele cha gari hilo na wengine kumzingira na kumpiga makofi yeye wakati akihoji sababu ya gari lake kuvunjwa kioo wakati akielekea eneo hilo katika mkutano.
Hata hivyo alisema kuwa katika vurugu hizo gari la matangazo na vijana waliokuwepo katika gari hilo ndio ambao wameshambuliwa sana na yeye wameishia kumsukuma na kumzaba makofi wakati wa mvutano huo .
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Juma Bwire alipotafutwa na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu alisema hajapata taarifa hizo zaidi ya kusikia kutoka kwa mwandishi hivyo anafuatilia