Iringa: Muda wa kuswali Misikitini wapunguzwa ili Kudhibiti Maambukizi ya Coronavirus

Iringa: Muda wa kuswali Misikitini wapunguzwa ili Kudhibiti Maambukizi ya Coronavirus

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Muda wa kuswali wapunguzwa Mkoani Iringa, kuanzia jana, muda wa kuswali katika nyumba za ibada umepunguzwa kutoka zaidi ya dakika 30 za awali hadi kati ya dakika 10 na 15 siku ya Ijumaa.

Shehe wa Mkoa wa Iringa, Abri Said alisema utekelezaji wa maelekezo hayo ulianza jana katika misikiti yote mkoani humo ikiwa ni hatua inayolenga kuunga mkono juhudi za serikali za kukabiliana na wimbi la tatu la covid-19.

“Kwa niaba ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania niwaombe waumini wetu wote mkoani Iringa kuchukua tahadhari kwa kuzingatia maelekezo ya wataalamu ili kuepukana na janga hili hatari,” alisema.

Pamoja na kupunguza muda huo wa ibada, Sheikh Abri alisema waumini watakaoenda misikitini, madrasa na watakaoshiriki shughuli nyingine za dini hiyo, watatakiwa kukaa mbalimbali ikiwa ni hatua nyingine ya kukabiliana na ugonjwa huo.

Kuhusu masuala ya misiba na ndoa, aliwaomba waumini wavumilie kwa kukubali ushiriki wa watu wachache kwa maana ya majirani na familia. “Tukijikinga na kujilinda, tukamtanguliza Mwenyezi Mungu, suala hili litakuwa la muda.

Mwenyezi Mungu atatulinda na tutavuka salama. Tuahirishe mikusanyiko na makongamano yasyo ya lazima,” alisema.
 
Virusi wanahitaji nusu sekunde tu ya kukutana viweze kusambaa. Tuachane na haya maigizo, watu wapewe chanjo haraka sana kabla maafa hayajazidi.
 
HIZI hofu ndizo zitakazovuruga ibada, itabidi wasali majumbani mwao na familia zao, inashangaza watu wa mungu nao wanawajaza hofu waumini wao
 
Muda wa kuswali wapunguzwa Mkoani Iringa, kuanzia jana, muda wa kuswali katika nyumba za ibada umepunguzwa kutoka zaidi ya dakika 30 za awali hadi kati ya dakika 10 na 15 siku ya Ijumaa.

Shehe wa Mkoa wa Iringa, Abri Said alisema utekelezaji wa maelekezo hayo ulianza jana katika misikiti yote mkoani humo ikiwa ni hatua inayolenga kuunga mkono juhudi za serikali za kukabiliana na wimbi la tatu la covid-19.

“Kwa niaba ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania niwaombe waumini wetu wote mkoani Iringa kuchukua tahadhari kwa kuzingatia maelekezo ya wataalamu ili kuepukana na janga hili hatari,” alisema.

Pamoja na kupunguza muda huo wa ibada, Sheikh Abri alisema waumini watakaoenda misikitini, madrasa na watakaoshiriki shughuli nyingine za dini hiyo, watatakiwa kukaa mbalimbali ikiwa ni hatua nyingine ya kukabiliana na ugonjwa huo.

Kuhusu masuala ya misiba na ndoa, aliwaomba waumini wavumilie kwa kukubali ushiriki wa watu wachache kwa maana ya majirani na familia. “Tukijikinga na kujilinda, tukamtanguliza Mwenyezi Mungu, suala hili litakuwa la muda.

Mwenyezi Mungu atatulinda na tutavuka salama. Tuahirishe mikusanyiko na makongamano yasyo ya lazima,” alisema.
Hii amri ya kupunguza mda wa hadi dakika15 khutba ya IJUMAA, haijakaa sawa na mda huo hauwezi kukidhi kukamilisha masharti ya ibada tukufu ambayo ni fardhi kwa muislamu. Kwa hivyo huyo Sheikh hafai!
 
Kupunguza muda wa kusali kwa hofu ya maambukizi ni sawa na kuvuruga mfumo wa ibada, maana yake hakutakuwa na ibada kadri sura ya maambukizi itakavyojitokeza. Hatima yake ni kuacha kukusanyika kuabudu kwa hofu ya maambukizi zaidi. Mungu hataabudiwa ki uhalisia, watu watajihami kuambukizwa
 
HIZI hofu ndizo zitakazovuruga ibada, itabidi wasali majumbani mwao na familia zao, inashangaza watu wa mungu nao wanawajaza hofu waumini wao
 
Back
Top Bottom