Is Kenya's ban on maize from Tanzania and Uganda has anything to do with this directive?

Is Kenya's ban on maize from Tanzania and Uganda has anything to do with this directive?

Sakata la shehena ya mahindi, RC Shigella asema hali ni shwari​



MONDAY MARCH 08 2021​

MAHINDI PIXC

Summary

  • Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella amesema shehena za mahindi kutoka Tanzania kwenda Kenya zinapitishwa katika mpaka wa Horohororo bila vikwazo ambapo kuanzia Machi 5 hadi 7 mwaka huu jumla ya tani 510 zimepitishwa mpakani hapo.


msuya

By Elias Msuya
More by this Author

Tanga/Dar. Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella amesema shehena za mahindi kutoka Tanzania kwenda Kenya zinapitishwa katika mpaka wa Horohororo bila vikwazo ambapo kuanzia Machi 5 hadi 7 mwaka huu jumla ya tani 510 zimepitishwa mpakani hapo.

Hata hivyo, zuio la kupeleka mahindi Kenya lilitolewa juzi na Wakala ya Kilimo na Chakula ya nchi hiyo ikidai kuwa mahindi kutoka Tanzania na Uganda yana kiwango kikubwa cha sumu kuvu ambayo ni hatari kwa usalama wa walaji.

Jipatie nakala yako ya gazeti la Mwananchi leo Machi 08, 2021 ili kujua undani wa habari hii






MY TAKE
Vp Wapuuzi wamefungua mpaka baada ya bashe kuchimba mkwara!
CC: Tony254
 
Vitunguu pia zipigwe ban,
Cheap onions za Tanzania zimefanya 50kg ishuke from 8k hadi 700-1000

Am trying kuthink vile wakulima wa Tanzania wananyanyaswa na brokers!!!!
 
Nilijua tu hili saga litawanufaisha cartels fulani
 

Tani 216 za mahindi kutoka Tanzania zazuiwa mpakani upande wa Kenya​



MONDAY MARCH 08 2021​

holili pic

Meneja wa Forodha Mkoa wa Kilimanjaro, Edwin Lwato

Summary

Magari 12 yenye shehena ya tani 216 za mahindi, yamezuiwa mpaka wa Holili, upande wa Kenya, kusubiri majibu ya vipimo vya sampuli zilizochukuliwa na mamlaka za Kenya.
ADVERTISEMENT

New Content Item (1)

By Florah Temba
More by this Author

Moshi. Magari 12 yenye shehena ya tani 216 za mahindi, yamezuiwa mpaka wa Holili, upande wa Kenya, kusubiri majibu ya vipimo vya sampuli zilizochukuliwa na mamlaka za Kenya.

Akizungumza leo Machi 8, 2021, Meneja wa Forodha Mkoa wa Kilimanjaro, Edwin Iwato amesema mahindi hayo yamezuiwa kuanzia Machi 5, mwaka huu na mpaka sasa bado wanasubiri majibu ya sampuli zilizochukuliwa.

"Katika mpaka wa Holili, kumekuwa na mkwamo wa kibiashara wa mahindi na kuanzia Machi 5 hadi 8, mwaka huu,kuna shehena ya mahindi tani 216, kutoka kwa wakulima wa Tanzania ambayo yamekwama upande wa Kenya, kusubiri taratibu za majibu ya vipimo.

"Sampuli zimechukuliwa kwa ajili ya vipimo kwenye shehena hizo za mahindi tani 216, bado tunasubiri wenzetu wa Kenya wakamilishe utaratibu huo,na ni changamoto ambayo imejitokeza na imeathiri kidogo mzunguko wa biashara hiyo ya mahindi,” aliongeza.

Aidha amsema serikali inaendelea kushughulikia suala hilo ili kuweza kukwamua mkwamo huo na kuwezesha biashara kwa pande zote kuendelea kama kawaida.

Wakizungumza baadhi ya wafanyabiashara wa mahindi katika mpaka wa Holili, wameonyesha kushangazwa na kauli ya Kenya kudai kuwa mahindi yana sumu,wakieleza kuwa wamefanya biashara hiyo zaidi ya miaka 20 bila matatizo.

Ramadhani Bakari, amesema wamekuwa wakishirikiana vizuri na wafanyabiashara wa Kenya na wamefanya biashara ya nafaka kwa muda mrefu bila matatizo lakini leo wanashangaa kusikia mahindi ya Tanzania yana sumu

"Kuna magari yamezuiwa upande wa Kenya lakini ukiangalia pia hapa katika soko la kimataifa la nafaka la Holili, kuna shehena ya mahindi ina wiki, wapo wafanyabiashara kutoka maeneo mbalimbali nchini na tunapata hasara kubwa, hatujui kama ni ishu za kisiasa au kuna mgogoro wa chini kwa chini unaendelea,” aliongeza.

"Tunaomba sana serikali hizi mbili, ziweze kukaa kwa pamoja na kuona namna ya kumaliza tatizo hili, maana tumekuwa tukishirikiana vizuri, kwa muda mrefu na hatujawahi kusikia watu hawa wamefariki Kenya au Tanzania kutokana na kula nafaka zenye sumu,” alilalamika Bakari.

 
If you wish to see geza happy, Write this phrase 'Win win situation'
 

Tule sumu na tuwalipe? Acheni masihara bana 😅
 
Back
Top Bottom