Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 128,308
- 245,426
masukuma gang kwa upumbavu wake yatapinga.Sasa hapo ndio mnashika dola kwa kupanda mlima of course chadema kilianzishwa na wanywa mbege huko migombani
USSR
Binadamu analipa zaidi kwa jambo linalokonga moyo wake,Watu huwa wanapandisha kanga(vitenge) kwenye mti wakati wa Harusi huko vijijini baadaye inaanza shughuli ya kula biriani, we umepandisha linguo mlimani unaona ajabu gani? Baadaye utalila?
Si kila mtu anaweza kufika huko , wengine wanafia njianiTanzania tunaonekana watu wa hovyo kwa mambo kama haya, kulikuwa na ulazima gani? Bendera ya Tanzania haitoshi huko? Kila chama kikiweka yake tutegemee mlima kufunikwa na vitambaa badala ya theruji. Aiseee!
Na hicho ndio kipaumbele chetu , huwa wanajaa wenyewe kwenye 18 zetuMbinu za CHADEMA ni za hali ya juu mno.. Zimefanikiwa kuifanya CHADEMA kuwa kwenye mijadala wakati wote huku CCM ikikosa kabisa cha kujadililwa
Hii alama ya ukombozi mpya wa kifikra ili kuondoa ile alama ya mwanzo iliyowekwa na mwenge katika kilele hicho cha Kibo kupitia fikra potofu za waganga wa kienyeji.
Hii ndio Taarifa ya sasa kwenda kwa jamii yote Duniani, kwamba hivi ninavyoandika hapa Bendera ya CHADEMA imepandishwa na kusimikwa rasmi kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro, yaani hivi sasa inapepea juu ya mlima huo.
Ndugu David Kilawila ndiye Shujaa aliyefanikiwa kuipandisha bendera hiyo kileleni hapo.
Sasa kwa kadiri ya maono ya Wadau hili jambo linatajwa kufanana na na lile Jambo la MAMA JUSI watatu walioona nyota iking'aa angani.
Je, kwa maoni yako Jambo hili linaashiria nini?