Konzo Ikweta
JF-Expert Member
- Oct 3, 2013
- 735
- 1,467
Kuna wakati kwenye maisha unaweza kuona kama vile kuna watu ambao wana uwezo MDOGO kuliko wewe ila wamepewa NAFASI kubwa unayostahili wewe. Ukijipima kimoyomoyo unasema “yaani hata sielewi kwa nini watu hawanioni”.
Unaanza kujifikiria-Mbona mimi nina KIPAJI kikubwa kuliko chake ila yeye anapewa nafasi kila siku mimi hawanioni? Mbona kila siku anapewa yeye nafasi na kusemwa vizuri ila kazi yangu hakuna anayeiona? Mbona akifanya kitu kilekile ambacho mimi huwa nakifanya yeye anaonekana genius wakati mimi nikifanya kinaonekana cha kawaida. Mbona nafanya kwa BIDII kuliko wao ila HESHIMA kila siku inaenda kwao?
Nimejifunza kwenye maisha kuna kitu kinaitwa “The Law of Timing”. Hii inahusisha wakati wako SAHIHI wa KUDHIHIRISHWA. Ukifanya na watu hawasemi, hawasifii au hawakutambui haimaanishi HAWAONI na wala haimaanishi UNAPOTEZA MUDA. Usiache, endelea. Ukilazimisha kuonekana kabla ya muda wako utapotea kabla ya muda wako, ”Trust the Process”.
Kila mtu ana wakati wa KUDHIHIRISHWA kwake. Huo wakati ukifika hata wewe utashangaa jinsi kila unachofanya kinavyoleta matokeo makubwa. Usipime siku kwa MAVUNO ya kila SIKU bali ipime kwa MBEGU unazokuza kila siku. USIACHE kumwagilia kwa HASIRA za kuona mbegu HAIOTI. Muda wako UNAKUJA!
#Nanauka
Unaanza kujifikiria-Mbona mimi nina KIPAJI kikubwa kuliko chake ila yeye anapewa nafasi kila siku mimi hawanioni? Mbona kila siku anapewa yeye nafasi na kusemwa vizuri ila kazi yangu hakuna anayeiona? Mbona akifanya kitu kilekile ambacho mimi huwa nakifanya yeye anaonekana genius wakati mimi nikifanya kinaonekana cha kawaida. Mbona nafanya kwa BIDII kuliko wao ila HESHIMA kila siku inaenda kwao?
Nimejifunza kwenye maisha kuna kitu kinaitwa “The Law of Timing”. Hii inahusisha wakati wako SAHIHI wa KUDHIHIRISHWA. Ukifanya na watu hawasemi, hawasifii au hawakutambui haimaanishi HAWAONI na wala haimaanishi UNAPOTEZA MUDA. Usiache, endelea. Ukilazimisha kuonekana kabla ya muda wako utapotea kabla ya muda wako, ”Trust the Process”.
Kila mtu ana wakati wa KUDHIHIRISHWA kwake. Huo wakati ukifika hata wewe utashangaa jinsi kila unachofanya kinavyoleta matokeo makubwa. Usipime siku kwa MAVUNO ya kila SIKU bali ipime kwa MBEGU unazokuza kila siku. USIACHE kumwagilia kwa HASIRA za kuona mbegu HAIOTI. Muda wako UNAKUJA!
#Nanauka