Israel imepokea ndege za kijeshi kutoka USA

Wakristo mnachekesha sana. Aliye andika bibilia alisha waroga mana alikuwa Muisael yani mkisikia
Israel mnachanganyikiwa wakati wao ndio walimua Yesu kama mnavyo dai ni Mungu wenu.
andika vizur au edit ueleweke mkuu.
 
Mungu ni muweza wa yote mkuu, hako unakokaita kakipande ka ardhi ndiko ambako Mungu alikuja akaishi hapa duniani miaka 33. Jifunze kutowekea uwezo wa Bwana Mungu wako mipaka. Wekea mipaka ya uwezo wa akili yako kama mwanadamu.

Na washawasha!


 
Bila ya USA hakuna Israel. Wanaitegemea sana USA na inawalinda.


The opposite is true. Hata Obama alikuwa na mawazo kama yako, kamuulize sasa. Vichwa vinavyo endesha USA na hata Urusi ni vya kiyahudi. Urusi na USA wanapiganishwa vita syria bila kijijua wanachopigania.

Na washawasha!
 
Kama hayo ndo mawazo yako, basi ni yako tu wala Mungu hahusiki nimekwambia kasome Ezekiel sura 38 na 39 kisha uje hapa na hoja kamili au kamuulize Mchungaji wako kuhusu Israel na siku za mwisho, nenda kasome Daniel yale majuma sita ya Israel na lile juma la saba linalojumlisha mataifa nje na Israel. Tafuta kujua ndoto ile ya sanamu ya mfalme
Nebukadreza ambayo Danile alitoa fasri yake, linganisha wanyama wanne aliwaona Daniel, tafuta kuijua pembe yenye macho na mdomo iliyoota juu ya mnyama wa nne.

Nenda mnyama juu ya nchi na yule mwingine aliyetoka ndani ya bahari, tafuta kujua sana habari ya Babeli nawanamke aliyepanda juu ya mnyama, haya utayapa kwenye Ufunuo wa Yohana.

Nenda tena soma Injili ya Mathayo sura yote ya 25, Mariko sura yote ya 13, Luka sura yote ya 21, malizia na Wathesalonike wa pili sura yota 2. Sasa jiulize Kristo atakapikuja ayakuta mataifa yanafanya nini huko Yisrael?

Kama unachuki na Wayahudi eti kwakuwa walimuua Yesu Kristo bado tena hujajua kunanini kati ya Mungu na Wayahudi hebu rudia tena kusoma Warumi 11:12-36 uone nini Mtume Paulo anasema juu ya Israel, halafu jiulize baada ya Kristo kuimaluza vita ya Amargedonia Israel itakuwa wapi na Kanisa litakuwa wapi.

Ndugu yangu haya mambo kwa lugha yetu yanaitwa eschatology, kwa mtu yeyote ambaye hii lugha bado kwake ni shida ni vigumu mno kuweza kuyachambua maana yamesemwa na kuandikwa kipoetic na ecalyptici hasa kwenye vitabu vya Ufunuo, Daniel, Ezekiel, 2Thessalonians, Mathayo 25,
Mataifa yote yataufikia mwisho wao bali Israel itabaki pamoja na wale wamtumainio BWANA katika dunia hii ya sasa ndo watadumu milele.
 

Hakuna kitu kibaya duniani na kwa mwanadamu kama mtu kuwa Braiwashed! Yaani umejieleza sana lakini point yako ya reference ni Biblia tu na ndiyo inakufanya uyaamini yote hayo unayoyaelezea kuhusu Israel as if na wewe ni muisrael!
Kikubwa nilichokiona kwako ni kwamba una ugonjwa wa kuelewa Jews ni nani na Christians ni nani! Alafu bado una ushabiki wa kutoelewa mambo..yaani umelishwa madesa ya hovyo kuhusu Israel.
Ujinga ni kitu kibaya sana haswa unapokuwa kwenye level ya juu.
 
Kama wewe ni mmoja wao waichukiao Bibilia Nenda kayaamini ya Charles Darwin na sura ya nyani ndani ya mwanadamu lakini mimi nitaamini ya Biblia na mfano wa Mungu ndani ya mwanadamu japo mwanadamu alianguka dhambini lakini bado Mungu akaleta mpango wa pili wa wokovu.
 
Nachokifahamu mim mambo karibu yote yanayotokea zama hizi yalikuwepo zamani ila sasa yanafanyika kulingana na mabadiliko ya vitu mbalimbali ikiwemo Technology.
Na kama hayakufanyika basi ni yalitabiriwa na sasa wakati wake umefika na unabii unatimia

Suala la mapigano kuitwaa ardhi ni jambo la miaka mingi tangu kuumbwa kwa misingi ya Dunia. Kwa mfano DAUD alikuwa mtumishi wa Mungu mzuri sana na ndiye ambaye Mungu alikuwa anamtumia katika mapigano/Vita (kumbuka ktk mapigano hayo damu zilimwagika). Na mara zote kabla hajaenda kupigana vita alikuwa lazima amuulize MUNGU aende au laah.. na mara zote Mungu akimruhusu atamwambi "Shuka upiganenao kwa maaana nitautia mji huo mikononi mwako" na mara nyingi waliposhinda vita na mji huo (aridhi hiyo) waliichukua wao na kuikaa...Pia kumbuka safari yao kutoka misri kwenda Kaanan (Nchi ya Ahadi) japo kuwa waliahidiwa kuikaa nchi hiyo lakini ilibidi wapigane vita vikali iliwaitwae kuimiliki ile Ardhi.
Kama ni msomaji wa Bible kumbuka Joshua, Kalebu na wenzao walitumwa kuipeleleza nchi ya kaanan kabla ya kwenda kuikalia, waliporudi wenzao wote walisema hawawezi kwenda kuitwaa ile nchi kwakuwa wanaoishi ndaniyake ni WANEFELI (Majitu makubwa) tena huwala watu hivyo wao wakajiona kama mapanzi mbele yao.. lakini Joshua na Kalebu wakamwambia Haruni na waisrael wote kuwa wasiogope ile nchi wamepewa kuitwaa wapande kupigana nao nahao watu watakua chakula yao.

Sasa kwa mfano huo pata picha hiyo vita ya kupigana na majitu ilikuwa ya namna gani. Na waliposhinda ndipo wakaitwaa Ardhi ya kanani.

So ndugu yangu mapigano ya Ardhi na ya mataifa kwa mataifa yalianza miaka mingi sana sema kwa sasa kutokana na technology zana za kivita zimeboreshwa..

Niongezee jambo hapo...kuna wazazi waliokulia dini sana wanawakataza vijana wao wasiingie jeshini kisa watapigana vita, watafanya matukio ya uuaji nk... binafsi naona hawapo sahihi. Tena kama ni mwanangu au ndugu yangu namwambi umechagua fungu lililobora sana. Nenda ukalitumikie Taifa ila usimwache MUNGU na kuisimamia haki. Chunguza historia ya Israel waliokuwa makamanda wakuu na waongoza mapambano wote walikuwa wachamungu hasa (Soma kitabu cha waamuzi ktk Bible ), Mfno mzuri Gideon, Jehu, Ehud, Joshua, Kalebu, DAUD nk wote hao waliongoza majeshi ya Israel ktk vita na walishinda kwakuwa Mungu alikuwa ndani yao.
 
Eti wakikosea? wanakosea wapi wao wanataka nchi yao na mipaka kama Mungu alivyombaia Musa, wala washabiki wa wafilisti na humanikwa hili itakula kwenu hata mkiunganisha arabic na uislam wote kupambana na Israel hamna kitu mtakacjoambulia Israel mbelekwambele hadi unabii utimie, wakristo bandia hawa wasiojua hata unabii unasema nini juu ya Israel na mataifa siku za mwisho.

Ushabiki wa human right haumzuii Mungu kutimiza mpango wake; hauwezi kuugawanya mji wa Yerusalemu eti ipande mwingine uwe wa wafilist kisa haki za binadamu? yaani Mungu afuate ya haki za binadamu;

Nimejaribu kwaonyesha hata vifungu ndani ya Biblia kuhusu Israel na siku za mwisho badala ya kuvisoma na kuja hapa na hoja ubakia kuilaumu Israel nchi inayochukiwa na kila muislam mdogo na mkubwa eti inawanyanyasa wafilisiti.

Chuki zidi ya Israel ni kujisumbua tu maana linapifika swala la kutimia yale Mungu aliyosema na manabii huwa haliangalii ni nani atapiteza au nani atapa bali kile Mungu anataka kifanyike ndo kitafanikiwa. Nimeuliza maswali nilizani utakuja kujibu?


Je pindi Yesu akirudi ataikuta dunia inafsnya nini? na je ni nini kitakuwa chanzo cha vita ya gogu na magogu hadi kubadilishwa kuitwa armagedonia?

Ni lazima msikiti wa al aqsa na lile dome viwe chini kwanza kisha hekalu lijengwe tena. upende usipende ni lazima unabii utimie. Hivi jiulize miaka zaidi ya 1896 Waisrael hawapo nchini mwao, lakini 1945 wakajikusanya na kulejea je unadhani ni kwanini 1968 nchi 9 za kiarabu
zilipigwa na kushindwa na taifa la Israel lisilozid raia 300000? Israel itawashinda wote maadui na mipaka yake itairejesha kama inavyotajwa katika Bibilia.
 
Wewe si mkristo au hufaham historia ya ukristo na uyahudi. Mashariki ya kati hakutakuwa na aman mpaka manandiko yatimie

 
Umenena vyema mkuu!! kuna watu humu eti nao wanajiita wakristo huku wakishindwa hata kujua tu Israel ilitokea wapi, na imepitia nyakati zipi tangu kuanzishwa kwake; eti wao wanailaumu kisa tu inataka kuirejesha mipaka yake na ardhi yote iliyochukuliwa na wapalestina ukiwemo mji wa Yerusalemu mashariki. Eti wao wanataka mji ugawanywe vipande viwili sehemu ya mashariki iwe ya wafilisti na magharibi iwe ya Israel kisa eti kule mashariki kuns mskiti wa al aqsa na lile dome lao.

Wakati Bibilia inaweka wazi kabisa kuwa mashariki mwa Israel ndiko huko mlima Moria upo na hapo ndipo Ibrahim alitaka kumtoa sadaka mwanae Isaka, vilevile ndo huko huko Sulemani alianza kujinga nyumba ya BWANA 2Nyakati 3:1. swali wakati Suleman analijenga Hekalu la BWANA huko Mlima Moria je waislamu walikuwa wapi? Bibilia haionyeshi uwepo wao enzi hizo wala enzi za Agano Jipya na na ndiyo masna neno uislam halipo keenye Bibilia.

586 B.C Yeremia yule nabii alishuhudia kubomolewa kwa mji wa Israel kisha kuvunjwa Hekalu lote na Nebukadreza mfalme wa Babeli Yeremia 39:1-18, baada ya miaka wakarudi tena na kuujenga Yerusalemu pamoja na Hekalu nalo likajengwa upya na akina Zerubabel na Nehemia tazama Neh. 2:1-20.

Hili ndo hekalu alilolikuta Yesu Kristo ambalo nalo lilibomolewa na Warumi mwaka ule wa 70 A.D na Wayahudi wote wakakimbia kwakuwa Rumi ilitoa amri kuwa myahudi yeyote atakayeonekana Yerusalem atauawa. Toka mwaka huo mpaka 1945 ndo tena Wayahudi wakaanza taaratibu kurudi kwenye nchi yao na kuwakuta waarabu wameshajenga mskiti mahali pa hekalu, mskiti huu ulijengwa takriban miaka ya 705 A.D
 
Wakristo mnachekesha sana. Aliye andika bibilia alisha waroga mana alikuwa Muisael yani mkisikia
Israel mnachanganyikiwa wakati wao ndio walimua Yesu kama mnavyo dai ni Mungu wenu.
una elements za misimamo mikali ww
 
mkuu hizo F-35 ziko overeted,hazina tofauti na ndege zingine,
halafu sikuhizi wale jamaa washakomaa na vita,ndege sio tishio tena,

ila kuhusu hilo hekalu,hivi unafikiri waisrael wanashindwa kulibomoa?,
tatizo lilipo ni matokeo ya huo ubomoaji,
kwanza kuna unabii fake waliosema utatimia ndo hekalu lijengwa,hautatimia kwahiyo itaonekana kumbe zilikuwa ni hekaya tu za abunuwasi na hivyo uwepo wa taifa la israel utaonekana kuwa umebase katika uongo,
pili vita itakayotokea baada ya hapo,inabidi kwanza wajiulize sana kabla hawajabomoa pale.

Kitu kingine,ni kuwa hapajawahi kuwepo sinagogi pale kabla mfalme wa iran,cryrus hajawajengea wayahudi baada ya kuwatimua wababel.
Palikuwa na kibanda tu cha mita 20x20,msingi unaonekana pale ni mabaki ya jengo lililojengwa na wairan miaka 3000 iliyopita
 
Wewe tayari uko brainwashed sasa siwezi endelea mjadala na wewe. You need to wake up!
 
mkuu ukitaka ujue hasa wenyeji wa Jerusaleam,hebu seach mtawala alieitwa Abdul Heba,
miaka 4000 iliyopita kabla hata abrahamu bado yuko chekechea kule kwao iraq
 
Samahani mkuu hivi hawa wajudaism wa Israel wanatumia biblia kama hii tunayotumia sisi? na ni wakristo kama sisi? , manake nimeona kanisani kwetu hata mchungaji anawapigania
 
Hivi mkuu mbona data zinaonesha Israel kuna waislamu wengi kuliko wakristo wenzetu halafu hawa jews kumbe ni wakristo wenzetu?
 
The opposite is true. Hata Obama alikuwa na mawazo kama yako, kamuulize sasa. Vichwa vinavyo endesha USA na hata Urusi ni vya kiyahudi. Urusi na USA wanapiganishwa vita syria bila kijijua wanachopigania.

Na washawasha!
achana na story za utotoni eti kwa kuwa ni gifted land ndo iwe na watu waelevu.... nitajie top ten ya wanasayans wakubwa au jamii yoyote muhimu... km waisrael watafika hata wa 4... tusidanganyane
 
Hongera! Ni wachache sana wamefikia hatua ya kujitambua na kuwa na fikra huru kama ww. Wakristo wengi na waislam wengi wamejivika udini na kusahau kuwa dini ya Mwenyezi MUNGU ni unyenyekevu na upendo tu basi. Ngoja niwapeni siri; Yeyote atakayetenda mema na akamcha mwenyezi MUNGU haitakuwa hofu juu yake na atalipwa mema siku ya kiyama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…