Israel kabla ilikuwa inajulikanaje?

Israel kabla ilikuwa inajulikanaje?

Je Musa hana historia pia ya kuishi misri na kuhusu Farao na wa Israel.
story ya wayahudi kuwepo utumwani ni fabricated story
hakuna rekodi yoyote misri inayoonyesha waliwahi kuwepo kule utumwani
hata hiyo wanayoita exodus haina ushahidi wowote
haiwezekani watu milioni 3 au zaidi wasafiri kwamiaka 40 kutoka misri hadi israel halafu wasiache ushahidi wowote mahala walipopita!!!!
kwa ufupi hiyo stori ipo kwenye biblia tu na sio kwenye kitabu chochote cha historia
 
MSINICHOKE WAUNGWANA..
NAENDELEA KUULIZA ILI NINOE ZAIDI UJUZI..
ETI NI KWELI KWAMBA CHEMBE CHEMBE ZA HAWA NEPHILS BADO ZIPO DUNIAN? KWENYE DUNIA YA LEO! KWASABABU HAWA JAMAA NDIO WALIKUWA MABINGWA WA UCHAWI NA UWEZO WA KISHETANI.. NA KAMA WALITEKETEZWA WOTE, MBONA MAMBO YA KICHAWI NDO YANASHAMILI SANA.. NA WATU NI WACHAWI SANA?. .. NA MAWAKALA WENGI WA UGANGA NA UCHAWI, WANGA, NK. + HAO FREEMASONS AND ILLUMINATS.. . JE! KUNA UWEZEKANO WA CHEMBE CHEMBE ZA DNA KU SURVIVE KWA WATU DUNIANI? NAWASILISHA NDUGUZE
Cc: Eiyer lifecoded Kudo
 
Hawakutekwa walienda mwenyewe. Yusufu aliuzwa na kaka zake kwa wamidian ambao walienda kumuuza Misri. Akapanda cheo akawa wapili kwa madaraka kutoka kwa Pharaoh. Njaa ikaikumba dunia. Kaka zake wakaenda kununua chakula akawatambua wakakaribishwa na Mzee Yakobo akaenda wakawa wamehamia huko. Alipokufa Yusufu ndiyo wakawa watumwa mpaka Mussa alipo watoa.
je, wamisri waliwatekaje hawa jamaa adi kuwafanya wawe watumwa wao.. /QUOTE]
 
zitto junior ,jonathan2018
Ngoja nijibu kwa kutumia maandiko matakatifu ili kuondoa mchanganyiko na baadhi ya matukio ya kileo kama vile masonry na Illuminati

Nitasamaraizi kuanzia kwenye garika hadi leo na ninaweka vifungu ili mtu ukasome mwenyew kuongeza ufahamu zaidi na kama kuna pahali nukuu haipo sawa basi nirekebishwe ili sote tujifunze..


Wanefili ("walio anguka, majitu") walikuwa watoto wa mahusiano ya kimapenzi kati ya wana wa Mungu na binti wa binadamu katika Mwanzo 6:1-4. Kuna mjadala kama utambulisho wa "wana wa Mungu." Ni ubishi wetu kwamba "wana wa Mungu" walikuwa malaika walioanguka (mapepo) ambao walijunziana na wanawake binadamu na / au wanaume binadamu waliopagagwa na kisha wakajumbiana na wanawake binadamu. Uhusiano huu ulisababisha watoto Wanefili, kwamba walikuwa "mashujaa wa zamani, watu wenye sifa" (Mwanzo 6:4).

Kwa nini mapepo wafanye jambo kama hilo? Biblia haitupi jibu hasa. Mapepo ni maovu, viumbe-ivilvyo geuzwa kwa hivyo hakuna kitu wanachokitenda kinafaa kutushangaza. Kama motisha ya kipekee, uvumi bora zaidi ni kwamba mapepo walikuwa wanajaribu kuchafua damu ya binadamu ili kuzuia ujio wa Masihi, Yesu Kristo. Mungu aliahidi kwamba Masihi atakuja kutoka uzao wa Hawa (Mwanzo 3:15) ambaye ataponda kichwa cha joka hilo, Shetani. Hivyo, mapepo walikuwa uwezekano wa kujaribu kuzuia hili na kuchafua ukoo wa binadamu, na kuifanya vigumu kwa ajili ya Masihi asiye na dhambi siku moja kuzaliwa. Tena, hili si jibu hasa la kibiblia, lakini ni uwezakano na si katika utata na kitu chochote Biblia inafundisha.

Wanefili walikuwa nani? Kwa mujibu wa Hebraic na hadithi zingine (kitabu cha Henoko na nyinginezo za maandiko yasiyo ya kibiblia), walikuwa kizazi kikubwa cha mashujaa maarufu ambao walifanya vitendo vya uovu mkubwa. Kawaida ukubwa na nguvu zao zilitokana na mchanganyiko wa “chembe cha za damu” ya mapepo na zile za binadamu. Yote ambayo Biblia moja kwa moja inasema kuhusu wao ni kwamba walikuwa "mashujaa wa zamani, watu wenye sifa" (Mwanzo 6:4). Wanefili walikuwa si wageni, walikuwa halisi, viumbe wa kimwili zinazozalishwa kutoka muungano wa wana wa Mungu na binti wa watu (Mwanzo 6:1-4).

Ni nini kilichotokea kwa Wanefili? Wanefili walikuwa moja ya sababu za msingi kwa ajili ya mafuriko kubwa katika wakati wa Nuhu. Pindi tu baada ya Wanefili wametajwa, neno la Mungu linatuambia hivi: "Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote. BWANA akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo. BWANA akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba niewafanya" (Mwanzo 6:5-7). Hivyo, Mungu aliendelea na mafuriko kwa dunia nzima, na kuua kila mtu na kila kitu (ikiwa ni pamoja na Wanefili) zaidi ya Nuhu na familia yake na wanyama waliokuwemo ndani ya safina (Mwanzo 6:11-22).

kulikuwa na Wanefili baada ya mafuriko? Mwanzo 6:4 inatuambia, "Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena, baad ya hayo wan wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu, wakazaa nao wana; hao ndio waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa." Inaonekana kwamba mapepo walirudia tendo la dhambi wakati mwingine baada ya mafuriko. Hata hivyo, ilifanyika kwa kiasi kidogo kuliko ilivyokuwa kabla ya mafuriko. Wakati wana wa Israeli walipeleleza nchi ya Kanaani wao walimpasa Musa taarifa: "Kisha huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona"(Hesabu 13:33). Basi, kifungu hiki hakisemi hasa kwamba Wanefili walikuwapo, ila wapelelezi waliwaza kuwa waliona Wanefili. Kuna uwezekano zaidi kuwa wapelelezi walishuhudia watu wakubwa sana katika Kanaani na kimakosa wakaamini kuwa wao ni Wanefili. Au, inawezekana kwamba baada ya mafuriko mapepo tena walijumbiana na wanawake binadamu, na kuzalisha zaidi Wanefili. Kwa hali yoyote ile, hawa "majitu" waliharibiwa na wana wa Israeli wakati wa uvamizi wao kwa Kanaani (Yoshua 11:21-22) na baadaye katika historia yao (Kumbukumbu 3:11; 1 Samweli 17).

Ni nini inazuia mapepo kutoka kuzalisha Wanefili Zaidi hii leo? Inaonekana kwamba Mungu alikomesha mapepo kuchumbiana na binadamu kwa kuweka mapepo yote waliofanya kitendo kama hicho katika lindi kuu. Yuda mstari wa 6 inatuambia, "Na, malaika walioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu." Ni wazi, si mapepo yamewekwa katika "gerezani" hii leo, hivyo lazima kuna kundi la mapepo wamekuwa wakifanya dhambi chungu zaidi ile ya awali ya kuanguka. Takribani, mapepo ambayo yalichumbina na wanawake binadamu ni wale ambao "wamefungwa minyororo ya milele." Hii itazuia mapepo yoyote zaidi kujaribu kitendo kama hicho.
 
Hii leo nimeelewa kwanini Alshababu, wanauwa jamii watu kwa madai wanatekeleza agizo la Mungu.

Kumbe Mungu tangu zamani, aliagiza minadamu, wangamizane wenyewe.
Kumbe sisi ni bustani yake
Kabla ya taifa la Israel kuwa na kuitwa Israel, lilikuwa linakaliwa na makabila ya uzao wa nduguye Esau, Mungu akaagiza popote watakapokuwa wanapita wawaangamize na wajitwalie wao ardhi iwe yao maana amewaruhusu
Hii leo nimeelewa kwanini Alshababu, wanauwa jamii watu kwa madai wanatekeleza agizo la Mungu.

Kumbe Mungu tangu zamani, aliagiza minadamu, wangamizane wenyewe.
Kumbe sisi ni bustani yake
Hii leo nimeelewa kwanini Alshababu, wanauwa jamii watu kwa madai wanatekeleza agizo la Mungu.

Kumbe Mungu tangu zamani, aliagiza minadamu, wangamizane wenyewe.
Alafu anatucheki tu, tunakouana sio.
 
zitto junior ,jonathan2018
Ngoja nijibu kwa kutumia maandiko matakatifu ili kuondoa mchanganyiko na baadhi ya matukio ya kileo kama vile masonry na Illuminati

Nitasamaraizi kuanzia kwenye garika hadi leo na ninaweka vifungu ili mtu ukasome mwenyew kuongeza ufahamu zaidi na kama kuna pahali nukuu haipo sawa basi nirekebishwe ili sote tujifunze..


Wanefili ("walio anguka, majitu") walikuwa watoto wa mahusiano ya kimapenzi kati ya wana wa Mungu na binti wa binadamu katika Mwanzo 6:1-4. Kuna mjadala kama utambulisho wa "wana wa Mungu." Ni ubishi wetu kwamba "wana wa Mungu" walikuwa malaika walioanguka (mapepo) ambao walijunziana na wanawake binadamu na / au wanaume binadamu waliopagagwa na kisha wakajumbiana na wanawake binadamu. Uhusiano huu ulisababisha watoto Wanefili, kwamba walikuwa "mashujaa wa zamani, watu wenye sifa" (Mwanzo 6:4).

Kwa nini mapepo wafanye jambo kama hilo? Biblia haitupi jibu hasa. Mapepo ni maovu, viumbe-ivilvyo geuzwa kwa hivyo hakuna kitu wanachokitenda kinafaa kutushangaza. Kama motisha ya kipekee, uvumi bora zaidi ni kwamba mapepo walikuwa wanajaribu kuchafua damu ya binadamu ili kuzuia ujio wa Masihi, Yesu Kristo. Mungu aliahidi kwamba Masihi atakuja kutoka uzao wa Hawa (Mwanzo 3:15) ambaye ataponda kichwa cha joka hilo, Shetani. Hivyo, mapepo walikuwa uwezekano wa kujaribu kuzuia hili na kuchafua ukoo wa binadamu, na kuifanya vigumu kwa ajili ya Masihi asiye na dhambi siku moja kuzaliwa. Tena, hili si jibu hasa la kibiblia, lakini ni uwezakano na si katika utata na kitu chochote Biblia inafundisha.

Wanefili walikuwa nani? Kwa mujibu wa Hebraic na hadithi zingine (kitabu cha Henoko na nyinginezo za maandiko yasiyo ya kibiblia), walikuwa kizazi kikubwa cha mashujaa maarufu ambao walifanya vitendo vya uovu mkubwa. Kawaida ukubwa na nguvu zao zilitokana na mchanganyiko wa “chembe cha za damu” ya mapepo na zile za binadamu. Yote ambayo Biblia moja kwa moja inasema kuhusu wao ni kwamba walikuwa "mashujaa wa zamani, watu wenye sifa" (Mwanzo 6:4). Wanefili walikuwa si wageni, walikuwa halisi, viumbe wa kimwili zinazozalishwa kutoka muungano wa wana wa Mungu na binti wa watu (Mwanzo 6:1-4).

Ni nini kilichotokea kwa Wanefili? Wanefili walikuwa moja ya sababu za msingi kwa ajili ya mafuriko kubwa katika wakati wa Nuhu. Pindi tu baada ya Wanefili wametajwa, neno la Mungu linatuambia hivi: "Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote. BWANA akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo. BWANA akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba niewafanya" (Mwanzo 6:5-7). Hivyo, Mungu aliendelea na mafuriko kwa dunia nzima, na kuua kila mtu na kila kitu (ikiwa ni pamoja na Wanefili) zaidi ya Nuhu na familia yake na wanyama waliokuwemo ndani ya safina (Mwanzo 6:11-22).

kulikuwa na Wanefili baada ya mafuriko? Mwanzo 6:4 inatuambia, "Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena, baad ya hayo wan wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu, wakazaa nao wana; hao ndio waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa." Inaonekana kwamba mapepo walirudia tendo la dhambi wakati mwingine baada ya mafuriko. Hata hivyo, ilifanyika kwa kiasi kidogo kuliko ilivyokuwa kabla ya mafuriko. Wakati wana wa Israeli walipeleleza nchi ya Kanaani wao walimpasa Musa taarifa: "Kisha huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona"(Hesabu 13:33). Basi, kifungu hiki hakisemi hasa kwamba Wanefili walikuwapo, ila wapelelezi waliwaza kuwa waliona Wanefili. Kuna uwezekano zaidi kuwa wapelelezi walishuhudia watu wakubwa sana katika Kanaani na kimakosa wakaamini kuwa wao ni Wanefili. Au, inawezekana kwamba baada ya mafuriko mapepo tena walijumbiana na wanawake binadamu, na kuzalisha zaidi Wanefili. Kwa hali yoyote ile, hawa "majitu" waliharibiwa na wana wa Israeli wakati wa uvamizi wao kwa Kanaani (Yoshua 11:21-22) na baadaye katika historia yao (Kumbukumbu 3:11; 1 Samweli 17).

Ni nini inazuia mapepo kutoka kuzalisha Wanefili Zaidi hii leo? Inaonekana kwamba Mungu alikomesha mapepo kuchumbiana na binadamu kwa kuweka mapepo yote waliofanya kitendo kama hicho katika lindi kuu. Yuda mstari wa 6 inatuambia, "Na, malaika walioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu." Ni wazi, si mapepo yamewekwa katika "gerezani" hii leo, hivyo lazima kuna kundi la mapepo wamekuwa wakifanya dhambi chungu zaidi ile ya awali ya kuanguka. Takribani, mapepo ambayo yalichumbina na wanawake binadamu ni wale ambao "wamefungwa minyororo ya milele." Hii itazuia mapepo yoyote zaidi kujaribu kitendo kama hicho.
MBONA KAMA UMERUKA MADA UMEJIKITA KWENYE "WANEFIL"I TU
 
Asili ya uchawi imetoka wapi?. nadhani jibu ni kutoka kwa wanefili kwakuwa walikuwa na uwezo mkubwa wa miujiza ya kishetani yaani uchawi.. sidhani kabla ya hao fallen angels kuingiliana na binti za wanadamu kulikuwa na uchawi.... so, gharika ilitokea na kuangamiza hawa jamaa wa ajabu.. then still leo wachawi, vinyamkera, na mawakala wao wapo kwa kiasi kikubwa.. au labda tuseme kwa kuwa shetani yupo na jamii yake.... means kwa namna moja au ingine analeta mambo hayo ya giza
 
Judea = Jodan
Judea (Yudea) ni Yuda au Jude...

Hii inatokana na mgawanyiko wa nchi ya Israeli miaka 800 kabla ya kuzaliwa Kristo ambapo makabila 10 yaliishi kaskazini mwa Israeli na nchi yao iliitwa Israeli na makabila mawili ya Benjamin na Yuda yaliishi kusini mwa Israeli na nchi yao iliitwa Judea au Yuda...

Makabila haya 10 hayajulikani yalipo leo hata hayo mawili nayo ni kitendawili. Makabila 10 yalisambaa hata kabla ya ujio wa Yesu na ndio maana alisema alikuja kuwatafuta kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli....

Walitawanyika baada ya kumuasi Mungu na kushiriki katika ibada za miungu mingine...
 
Upotoshaji ni mwingi sana mitandaoni, na hii ni kwa sababu wajuaji ni wengi kuliko wajuzi wa mambo.

Kila mtu anakuja na mawazo kwa sababu tu eti naye amesoma maandiko na makaratasi ya kihistoria.

Vijana tulieni historia ina watu wake.
 
Mkuu nitasummarise tu.... Abraham alikuwa anaishi huko Ur katika nchi ya mesopotamia ila baada ya vuta nkuvute na mfalme Nimrod /Amraphel mwisho wa akahamia nchi inaitwa canaan (Israel ya sasa) ambayo iliitwa canaana sababu ndipo waliishi mjukuu wa Nuhu aliyeitwa canaan na vikapita vizazi na mjukuu wake aliitwa Yakobo nickname yake akaitwa Israel na ndipo nchi walioishi ikachukua hilo jina. Baadae hao waisrael walienda utumwani huko misri kwa miaka 400 hivyo watoto wa Canaan sasa kina Amori,Hivi,Hiti,yebusi,amaleki,Rapha n.k waliishi huko hivyo waisrael waliporudi walikuta tayari sehemu kubwa ya hiyo ardhi ya canaan inakaliwa na hayo makabila ya watoto wa canaan.

Hivyo vita ikapiganwa kwa miaka kadhaa kati ya hao waisrael vs canaanites na mwisho wa siku canaan wakaporwa ardhi yao na wakakimbilia ilipo gaza ya sasa huko palestina hivyo kubadilisha jina la nchi hiyo kutoka kuitwa CANAAN hadi kuitwa ISRAEL/JUDEA and the rest is history.

NB: Israel sio nchi ya ahadi kwa Israel pekee bali ni nchi aliyoahidiwa Abraham na Mungu wake na wote tunafahamu Abraham alikuwa baba wa mataifa mengi ila kama kawaida ujanja ujanja wa Yakobo akaiba uzao wa kwanza na kujipa umiliki huo na hata baraka za Abraham akajimilikisha hivyo tusiseme nchi yao ya ahadi bali nchi aliyoahidiwa ABRAHAM.

Ni hayo tu
Mkuu zitto junior, Ibrahim alipotoka Mesapotania kwwnda kwenye nchi aliyoambiwa na Mungu, alipofika alikuta watu wanaishi pale. Ni kina nani walikuwa wanaishi pale?
 
Mkuu zitto junior, Ibrahim alipotoka Mesapotania kwwnda kwenye nchi aliyoambiwa na Mungu, alipofika alikuta watu wanaishi pale. Ni kina nani walikuwa wanaishi pale?
Biblia iko wazi kabisa na wakati Mungu anampa alijua kuna watu wanaishi.

Tusome......
Mwanzo 15:18-21
18 Siku ile BWANA akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati,
19 Mkeni, na Mkenizi, na Mkadmoni,
20 na Mhiti, na Mperizi, na Mrefai,
21 na Mwamori, na Mkanaani, na Mgirgashi, na Myebusi.


Hivyo kwa mstari huu Walikuwa wanaishi watoto wa CANAAN ambalo ndio jina halisi ya hiyo nchi aliyoenda Abraham..... Makabila yaliyokuwa yanaishi hapo ni Hivi,Hiti,Amori,warefai,myebusi,mgirgashi

Na nimesema hapo juu Mungu alimpa hii ardhi ya CANAAN ili kutimiza laana ya Nuhu juu ya Canaan kwa sababu ya dhambi ya baba yake tusome hapa

Mwanzo 9
24 Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.
25 Akasema,Na alaaniwe Kanaani;Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.
26 Akasema,Na atukuzwe BWANA Mungu wa Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake.
27 Mungu akamnafisishe Yafethi.Na akae katika hema za Shemu;Na Kanaani awe mtumwa wake.


Hivyo kwa kuhitimisha Abraham alikuta watu wanaishi Caanan ila chanzo cha kwanini Nuhu alimlaani Canaan kwa dhambi ambayo hajafanya niliwahi kuhoji humu ila sikupata jibu.

Kwanini Canaan alilaaniwa na sio Ham?! - JamiiForums
Shukrani
 
Hasa kilichowatoa kaanani kuja Misri ni njaa, kwa kweli usifanye mchezo na njaa , haina baunsa mkuu, kuna ndugu yao mmoja alikuwa na fursa misri ndio aliwavuta ndugu zake wote kuja kustiri matumbo misri, lakini kama unavyojua uongozi ni kupokezana vijiti, sasa mda ukaenda akaja kiongozi mwengine mithili ya jiwe huyo aelewi aliwafanya kama vijakazi mkuu walikuwa dhariri kweli kweli
Kwa jicho la kibinadamu utaona ni njaa ndio iliwapeleka kule, ila kwa jicho la kiroho utaona ndoto aliyoota Yusuph inatimia.
 
Spiritual ni vip?
kibinadamu ni vip?
Spiritual alishachaguliwa kuwa mkuu kwa wenzake, na alionyeshwa kwenye ndoto, maana ndoto ni njia mojawapo ya mawasiliano ya kiroho kwa binadamu, sasa baada kuchaguliwa katika ulimwengu wa roho, kilicho baki ni kujizihirisha katika ulimwengu wa mwili au kibadamu.
Sasa kibadamu ndio unaona yusuph anauzwa na ndugu zake baada kughairi kumuua, tena baada ya miaka njaa inawapeleka kule aliko ndugu yao.
 
Back
Top Bottom