Israel mambo yamewafika hapa. Watishia kuipiga Lebanon kama dunia itashindwa kuwaondoa Hizbullah mpakani. Je, wataweza?

Binafsi hua napenda kufuatilia vita ya Ukraine kupitia Aljazeera among others ila nimeacha kabisa kuangalia tokea October 07 kwasababu 24/7 wanaongelea Gaza tuu.

Hata hapa huu uzi unaboa kwasababu inakua ngumu sana kupata taarifa yoyote ya maana kwenye military aspects za vita kwasababu kila anae comment anatanguliza udini whether anawatetea Israel ama Waarabu.

Sent from my SM-A135F using JamiiForums mobile app
 
Tafsiri yakupigana siku nyingi uwanja wa vita kua ndio kushindwa haikuanza leo
Tunakukumbusha tu ilianza tokea pale ukraine kwa kauli mbiu yako wachuuzi wagesi wana mwaka watatu sasa wanahangaika na ukraine
Tunakukumbusha tu kama wewe ndio ulikua unasema hayo
 
Sasa assad kutumia gesi ya sarin ambayo haikuthinitishwa ukweli wakutumika kwake ila tuseme alitumia kweli kama usemavyo kuna tofauti gani na israhell kutumia white phosphorus
Yaani israhell anatumia mpaka white phosphorus ambayo imepigwa marufuku ila bado tu unasema haijabanwa
Ukiona unapigana na mtu halaf umeambiwa usitumie vichwa ukaja ukatumia vichwa ujue umezidiwa mzee
Israhell hapo labda faida kubwa anayoipata hapigani kwake ila kitendo chakutumia mpaka white phosphorus ambayo imekatazwa inaonesha kama jamaa kazidiwa mpaka kutumia hio
Yaani wanajeshi wako wanakufa halaf useme hujazidiwa hakuna jeshi linalopenda wanajeshi wake wafe kama uwezekano wakutokufa upo ila tu hua wanazidiwa
Israhell hapendi hii vita iendelee mpaka sasa ila hajaweza kuimaliza kama angeweza angekua kaishamaliza zamani sana
Israhell mpaka anaomba mapigano kusimamishwa ili akomboe mateka kama angeweza si angewakomboa kwani kuna ulazima wakusimamisha mapigano wakat uwezo wakuwaokoa unao
Kushindwa kwa israhell kupo wazi hakuhitaji tochi faida pekee kwake nikua vita haipiganwi kwake hapa naungana nawewe
 
Hizbullah haihitaji kuingia israhell kufanya mashambulizi
Nandio maana inapiga israhell ikiwa Lebanon na inaua majeshi ya israhell na kuchoma vituo vyake vya kijeshi vizuri tu
Sasa ni kazi kwa israhell kwenda kuwazuia ili wasipige ndani ya israhell kama walivyo fanya kwa hamas
 
sure mkuu kuanzia mleta uzi ni ananuka udini tu
 
Brigedia ya golani imerejeshwa baada ya kuona wanakufa sana wakaona wataisha
Hakuna Anaelalamika masacre kama mungekua hamuui watoto na wanawake
Mnasema hamas wapo chini ila ajabu mnapiga hospital
Sasa shida yenu hamas au shida yenu hospital
Kama mnataka hamas wafateni huko walipo uone kama kuna mtu atasema neno
 
Huyo jamaa niishamzarau kitambo sana. Hezbollah ni Wagner2. Wana silaha za kisasa mpaka air defense.
wana kombora la kuzamisha meli la Hornet sio kama yale ya Houth madogo madogo na droni kibao
 
Unajichanganya bure.Haya sema kama una vyanzo vyengine vizuri vya kupatia hizo habari na sisi tukufuate huko.
 
israel anaingia na kupiga lebanon, anaingia na kupiga syria, anaingia na kupiga palestina kila anapotaka na hakuna anayemzuia au hujui hilo mzee?
 
israel anaingia na kupiga lebanon, anaingia na kupiga syria, anaingia na kupiga palestina kila anapotaka na hakuna anayemzuia au hujui hilo mzee?
Huko kwengine anaingia na kupiga naungana na wewe ila Lebanon hua haingii na kupiga
Israhell akimpiga Lebanon tokea baada ya vita ya mwaka 2006 hakuna siku israhell kapiga Lebanon halaf ikapita bila kujibiwa
Kubwa tu hua hasara na maafa yanazidiana ila israhell akiigusa Lebanon Hizbullah hua wanajibu hawajawahi kukaa kimya kama ipo siku israhell kapiga Lebanon halaf Hizbullah wakakaa kimya nikumbushe labda nimesahau
 
Huko chini Hamas wanafanya nini? Yaani wanawake na watoto wamelekezwa juu halafu wao wanajificha chini wanategemea hao watoto na wanawake walindwe na Nani?
 
Huko chini Hamas wanafanya nini? Yaani wanawake na watoto wamelekezwa juu halafu wao wanajificha chini wanategemea hao watoto na wanawake walindwe na Nani?
Kwani hao israhell huko juu na kule baharini wanafanya nini?
 
Sasa assad kutumia gesi ya sarin ambayo haikuthinitishwa ukweli wakutumika kwake ila tuseme alitumia kweli kama usemavyo
Kama haikudhibotishwa, ilikuaje Assad akasaini mkataba wa kuharibu shehena ya tani za Sarin gas?

kuna tofauti gani na israhell kutumia white phosphorus
White phosphorus sio chemical weapon kiuhalisia, chemical weapon gani inaweza tumika kama cover ya advancement ya jeshi, yani iwe chemical weapon alafu muitumie wenyewe kujifichia?
Cha msingi isitumike kwenye makazi ya watu ili wasiungue, sasa pale North Gaza kwenye magofu ndio unakata white phosphorus isitumike.
Yaani israhell anatumia mpaka white phosphorus ambayo imepigwa marufuku ila bado tu unasema haijabanwa
Kumbe kuna kufuata sheria za kimataifa. Sasa mbona ulishangilia Hamas kuvamia raia na kuwaua. Wakati huo sheria za kimataifa hukuwa unazijua?
 
Sasa kama unaona kutumia white phosphorus kulipo katazwa sio shida kwanini ulimgusia assad
Hapa kilichoongelewa ni kwamba zimetumika silaha zilizopigwa marufuku haijalishi zilitumika wapi wala wapi
Hao walozipiga marufuku hawakuyajua haya unayoyasema wewe
Israhell washatishia mpaka kutumia nyuklia kwa hamas tu sijui unataka kutwambia nn 🤔
 
Acha kuandika kwa mihemko na kuandika upuuzi we jamaa , vita haipiganwi kwa mdomo ,vita sio movies kama wajinga ninyi mnavyofikiri
Wewe unayedhani una akili kwanini usiwaambie hao Hezbollah waivamie Israel. Si wako wanapakana kabisa. Unadai vita haipiganwi kwa mdomo wakati hao Hezbollah wako wanatoa matamko kila siku, na mkuu wao Nasrallah alibwabwaja hamna kitu alilenga, akajiondoa kuhusika na mashambulizi na hakutoa support. Si waache kuchonga midomo waingie vitani uone kama hawapukutiki.
Vita ni ngumu siku hizi ,mbinu zimeevolve na watu wamekuja na strategies tofauti , acheni story za abunuwasi hizo za Israel sijui kumpiga nani
Ni lini vita ilikuwa rahisi mpaka useme imekuwa ngumu siku hizi?
Alafu unalinganishaje vita ya zamani na ya sasa kisha unasema ya sasa ni ngumu. Yani unachukua kama Battle of Somme au Stalingrad au Battle of Hurtgen forest unalinganisha na battle uchwara hizi za Bakhmut na Gaza? Au umetokea kwenye kutazama katuni hii ndio vita yako ya kwanza kufuatilia.
Israel kawashindwa Hamas ndio unadhani itakuwa mterezo kwa battle proven and toughened Hezbollah
Hezbollah mpaka tunakaribia Christmas ilikuwa imetangaza wapiganaji wake 117 wamekwishauwawa na Israel. Na hapo hawapo vitani, sasa kwanini usiwaombe Hezbollah waingie vitani na Israel tena kwa kutumia kisingizio cha wapiganaji wake 117 kuuwawa?

Battle proven wako 117+ wamefariki vita haijaanza, ikianze je!
Unajua Hezbollah wamepigana vita ngapi tangia 2006 ?
Unajua Israel imepigana vita ngapi tangu 1948?
Hujui mchango wa Hezbollah kwenye ile Syrian war na kuulinda uongozi na serikali ya Asad WA Syria kuendelea kuexist ?
Assad alikuwa na jeshi lake mwenyewe, Russia, Iran, makundi ya Wakurdi, Yazidi, Houthi na wengine hao Hezbollah. Mpaka sasa Assad hana umiliki wa nchi nzima. Sasa ajabu walilofanya Hezbollah ni nini?

Nami nikuulize unaujua mchango wa mashambulizi ya Israel dhidi ya majeshi ya Iran hapohapo Syria?
Unamjua marehemu Brigadier General Mosuavi wewe?
Unajua vita walizopigana na ISIS na waasi kule Syria na kufanikiwa kulisaidia jeshi lililokuwa karibuni kushindwa la Assad
Kwahiyo leo hii mnasema aliyeisaidia Syria dhidi ya ISIS ni Hezbollah. Sio Iran na Russia tena? Msimamo huu mtaendelea nao au ikitokea Iran inapigana na Israel mtaubadili mseme Iran ndio ilipigana na ISIS.

Syria ni nchi weak na ndio hiyo bado mnataka ijilipue ipigane na Israel. Sasa nchi weak kutekwa na waasi na wanamgambo wa Kiislamu ni ajabu?
 
Hamas hawana hadhi ya kupigwa nyuklia, hao ni vikojozi wanatakiwa wachapwe viboko tu.
Israel sio kama Russia, Israel haijawahi tishia yeyote wala kufanya maonyesho ya silaha zake za nyuklia.

Swali: Ni lini serikali ya Israel iliwahi sema ina silaha za nyuklia?

Huwezi tishia kitu unachokataa kuwa nacho, sasa Israel itatishiaje nukes na wakati haijawahi kubali kuwa nazo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…