Pre GE2025 Itungwe sheria inayotoa adhabu dhidi ya wanaomtukana Rais

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
mtafuteni mwenyekiti wenu wa wasomi chawa PASCO MAYALA.
Ndo kiongozi wenu,kikundi Cha Kusifu na kutukuza viongozi ...
Duh...!, kwa hivyo mimi ndie Mwenyekiti wa ma chawa!, uchaguzi ulifanyika lini mimi nikachagulwa?.
Mnazionaga nyuzi zangu za kusifu tuu, lakini za kukosoa huwa hamzioni?

Kuna chawa anaweza kupandisha bandiko kama hili?.
- Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye!

- Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, 2025 Mama Akabidhi Kwanza Mwanamume, Kisha 2030 Ndipo Aje Mwanamke

- Kauli ya Rais kwa waandishi 'Wapara' kuwa wakimpara "Atawaparua", Je Rais Samia ni katili?, Soma Jinsi ya kuwabaini makatili!. Ni kutumia macho tu!.

- Uhuru wa Habari Tanzania: Kati ya Waparaji na Wakunaji Wazuri, Nani Watamsaidia Zaidi Rais Samia?. Tunakuomba Mama, Usiwaparure Waparaji!.

- Mabadiliko ya Sheria Bila Mabadiliko ya Katiba,Sawa na Kula Bila Kunawa!. Je Watanzania Tuna Haraka Sana na Uchaguzi Hadi Tukimbilie Kula Bila Kunawa?

- Kufanya kosa si kosa, kosa kurudia kosa! Sheria ya Uchaguzi ni kosa. Kwanini tunarudia kosa? Haki si hisani, ni stahiki. Bunge tutendeeni haki!

- Madudu ya ajabu ya ubatili wa Katiba yetu, mabadiliko "fake" ya sheria na Tume ya Uchaguzi. Rais Samia asilaumiwe kwasababu yeye sio mwanasheria!

- Mabadiliko ya Sheria ya Uchaguzi: Je Tupige Ndege Wawili kwa Jiwe Moja kwa Uchaguzi Serikali za Mitaa/Mkuu, Ufanyike Siku Moja au Tuendeleze Mazoea?

- "IGA ya DPW imetusaidia sana kujitambua. Tuna wanasheria wa Aina Gani!, Bunge na Serikali yetu, Ilipitishaje IGA Hii?

- Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda

Chawa anaweza kuleta hoja kama hizi?. Haya ni mabandiko 10 tuu, ukitaka 20 nakupa, ukitaka 30 nakupa.

P.
 
tusibishane bure unajua tusi ni lipi, na neno la kawaida ni lipi. Kuna maneno yanaweza kuwa ni karaha lakini siyo matusi. Au hukujifunza kiswahili ulipokuwa shuleni mwenzetu umesoma english medium?
 
acha kutetea ujinga , sidhan kama hata D mbili unazo wewe
Mkuu unanifanya nikudharau ingawa sikufahamu. D mbili ndiyo nini kwanza? Jenga hoja taratibu bila kejeli na dharau utafika mbali sana na watu watakuekewa unachomaanisha ila kwa mtindo huu inaonesha hata wewe mwenyewe unajidharau nimeona mahali umeandika "ubadilishane ngozi".

Hivi Brother hujawahi kuanbiwa kujidharau mwenyewe ni hatari sana?.Naomba nikudhauri kuwa" acha kujidharau hutawadharau wengine pia.
Una hoja nzuri ila halo kakitu kanakuharibia sana. Nikutoe wasiwasi kanaweza kutoka na ukawa vizuri kabisa.
 
Fanya kazi kwa bidii ujiongezee kipato utapunguza hasira zisizo na sababu
 
Kaka pokea chalenji😂😂😂😂
 
Si ndio hiyo sheria ya uchochezi na kuigombanisha serikali na wananchi wake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…