Donnie Charlie
JF-Expert Member
- Sep 16, 2009
- 16,908
- 19,123
Aisee umetishaMi kipindi nakua nakumbuka ITV ilikua na maigizo ya Mizengwe ya Max na Zembwela, igizo la Mambo hayo akiwepo kina Dokii,Dr cheni Joti na mpoki kama sikosei.
Nawakumbuka kina Mlopelo, Muhogo Mchungu na Mzee Pwagu
Kukawa na Igizo la sayari mziki wake ukawa unaimbwa "Sayari yetu sayarii oooh sayarii🎶" hapo nilikua namuona Johari, Ray, Kanumba, Mzee magari, na Ben, alafu likaja igizo la Jahazi.
Maigizo tulikua tunayaangalia marudio yake siku ya jumamosi mchana yaani siku ya jumamosi inakua Kama siku ya sherehe nawahi kuoga na ninafanya usafi kwa juhudi ili saaa 9 inikute nimeshamaliza kazi zote niangalie marudio.
Alafu jumamosi saa 3 usiku maigizo yanaendelea saa 4 usiku naangalia WWE miereka ya kina DX na John Cena kabla ya igizo kuisha kunakua na matangazo matatu , kulikua na matangazo ya chai jaba na lile tangazo la jambo lotion lotion inakata kiuono balaa
Mimi naitwa jambo kubwaa🎶 na wewe jee🎶 Mimi naitwa jambo katikatii 🎶 na wewe jee ? Mimi naitwa jambo ndogoo🎶
Daaaaah Times flies, Times flies.
Saa mbili baada ya Taarifa ya Habari! Nakumbuka jumatano kulikuwa na Maisha.
Kulikuwepo pia kipindi kizuri sana cha CAPTAIN kilichokuwa kinaitwa BEYOND 2000. RENAGADE pia ya akina Rhino Ranks na Richmond Branscombe! Usisahau na VITIMBI kutoka KBC ambayo nayo pia ilikuwa inarushwa kupitia ITVKampuni ya IPP Limited mwaka 1994 inatambulisha chaneli ya Analog kwa jina ITV kupitia masafa ya mawimbi ya kawaida kipindi hiko.
Na kipindi hiko ndio mtaa mzima tumenunua TV ya PANASONIC TX iliyotoka 1993 sikumbuki model ikiwa ya rangi.
Kipindi hiko Tv inafunguliwa saa 8 au 10 sikumbuki ila inafungwa saa sita usiku.
Ndipo nilipo jua series kama:
*Family Matters
*Perfect Strangers
*fresh prince of bel air
*The V
Na matangazo kama :
*Revlon
*cocal cola
Kipindi hiko unaamka usiku kushuhudia ngumi za Mike Tyson.
Ila kuna dada mmoja ni kama mwarabu au muhindi fulani alikuwa ndo mtu wa kwanza ITV wanafungua ndo anaonekana sana. Hivi yupo wapi miaka 30 sasa.
Wenye kuijua ITV vizuri
[mention]pasco mayala [/mention] ni moja ya watu wenye kuijua ITV
Hizi zilifuata baadaye kwenye miaka ya 1996, tumezainagalia tukiwa kwenye ma-hall ya udsm. Days of Ourr Lives piaNimekumbuka the bold and the beautiful hiyo miaka ya 90, kulikuwa na tamthlia ya sunset beach, mara acapulco bay.
Alikuwa anaitwa Fauziyat Abood. Huyu ndiyo alianza kabisa halafu wakafuata akina Suzan MungiYupi huyo ni Shyrose Bhanji au yule mwenye mwanya mzuri alikuwa naitwa Neema kama sikosei?
Seki bwana yupo wapi?KWA UCHACHE NILOKAWA NACHUNGULIA DIRUSHANI NILIPENDA SANA KIPINDI CHA SEKI ENZI ZILE CHANNEL 5 ILIKUWA ANAWAHOJI WATU BEACH NA STYLE YAKE YA KUGEUZA CAP NA ALIKUWA ANATIA MBWEMBWE FLANI HIVI ZA COMEDY.
ILA NIRUDIPO HOME ILIKUWA NI KWENYE PANASONIC RADIO YA MSHUA RTD NDIO STATION MAMA NIKAWA MPENZI WA TAARIFA YA HABARI HUSUSAN REPORTER BEEN KIKO KAMA SIKOSEI AKIRIPOT HABARI ZA MUSOMA NILIPENDA SANA AINA YA UONGEAJI WAKE SIJAONA MWENYE KUKOPY KIZAZI HICHI CHA CONNECTION.
ILA RADIO ONE ILIKUWA TUNAKUSANYIKA JIONI SAA 11 NA WASHKAJI WEEKEND TUKITOKA KUFUA UNIFORM MTONI NA KUSIKILIZA RADHA 10 ZA BONGO ZIKIPOROMOSHWA NA "ABD" ABDALLAH MWAIPAYA NA KIPINDI CHA CHEMSHA BONGO NISHAMSAHAU MTANGAZAJI DAAH MZEE WA KENGELE NADGANI HII NDIO KAIKOPY D'JARO TBC PIA USIKU WA SAA 3 ILIKUWA NI CHAGUO LA DJ MIKONO YA ABOUBAKAR SADICK KWA FUIO HAPO NDIO ILIKUWA BETRI ZA VIDONGE ZINAISHIAGA.
RADIO YANGU YA MWISHO KUIFATILIA NI RFA MWANZONI KABISA MWA FM STATION SIJAJUA HAWA JANAA WALIONGEZA NINI KWENYE ILE MITAMBO YAO MAANA FREDY FEDRICK "FEDWAA" (Hayati) HUYU MWAMBA SAUTI ILIVYOKAWA INAPAFOM VIZURI KULE RFA IKAWA NI TOFAUTI KABISA NA FEDWAA ILOKAFANYA NINUNUE WORKMAN YANGU MAANA JAMAA ILIKUWA KILA KIPINDI ANACHOSIMAMA UTASEMA KISIISHE NAKUMBUKA ENZI ZILE YULE JAMAA WA SITOSAHAU NA STORY YA GAMBOSHI NDIO IKIWA MWANZONI MWANZONI KABISA KIUKWELI RFA ILIKUWA NI MOTO SIJAJUA CLOUDS KULIKUWA NA AKINA NANI MAANA TULIKUWA TUNASIMULIWA NA WALE WARUDIO DAR NA KUZIPONDA RADIO TUNAZOSIKILIZA KWA KUZIITA ZA KISHAMBA HAAAA HAAAA HAAAA DUH PANGETOKA FULSA MAISHA KUPIGA REVERSE BASI ILE MIAKA NDIO NINGERUDI ILA DUUU NINGEMISS JF MAANA NDIO KIDOOOOGO SEHEMU ILIYOBAKI RUBUDAAAAANI
Juzi nimekereka nimetune Wasafi F.M barabarani nasikia Juma Lokole kama sikosei anaeleza kwamba ile haki ya kitunguu ukikata kinakutoa machozi wale ni bacteria fulani ambao naturaly wako katika vitunguu!Enzi hizo kuna kipindi radio one kinaitwa the heat sikosei, utasikia bongo fleva zote kipindi hicho Mr 2 ndio anatoka na nyimbo zake za Yamenikuta, Utaitwaje tozi shule kama huwezi imba mistari ya sugu? Hahahhaa
Kuna ile nani zaidi, Jumapili hapo, Alipambanishwa Buju Banto na Shaba Ranks Asee kete zote za moto pambano likawa droo ikabidi lirudiwe tena Siku nyingine Mnaikumbuka hii?
Radio station za siku hzi ukifungulia stori tuuu za watangazaji hazina mvuto tena.
Baba yangu aliniita hili jina Rino Lenzi.Umeisahau Rino Lenzi mkuu, ile jingle yake wakati tamthlia inaanza inapigwa mpaka kesho Radio One
Mimi nimeikuta channel 5.Mpaka leo nikitaka kutupia jicho channel za ndan upande wa habari ni itv 😃
Wakaja na itv 2 channel 5 badae ikawa eatv
Kila Nchi ilikuwa na Frequency tufauti ya Sauti. Tanzania ni 6.0 MHz. So TV nyingi japo zilikuwa na system ya PAL sauti zilikuwa azina 6MHz so ilikuwa either uibadike cystal ya 6.0MHz au huiweke juu ya iliyokuja na TV. Henzi hizo spear korofi ya TV ilikuwa fly back transformer (FBT) na Duka kubwa la spear lilikuwa nyuma ya Jengo la Ushirika mnazi mmoja jamaa anaitwa Rushna. Tulipiga sana hela those days- na jamaa angu kuna mitaa alimwelewa Binti ikawa kila siku anatuaga workshop eti anaenda rekebisha Antenna imekaa Vibaya😂 kwenye nyumba hiyo hiyo kila siku.Si akamtia mimba Binti ya Mwenye Nyumba ! Mpaka Leo Tayari wana wajukuu- jamaa aliozwa ndoa ya MkekaMimi naikumbuka Panasonic top dome, nilinunua laki tatu na sitini mwaka ' 93 nilikuwa naangalia KBC kenya, itv ilikuja baadae, na kupata itv ilibidi ufunge kitu kinaitwa crystal!
Sent from my SM-T285 using JamiiForums mobile app
Wewe unaitwa Rino Lenzi?Baba yangu aliniita hili jina Rino Lenzi.
Alikuaga ni mpenzi wa movies sana,
Kwa sasa ni marehemu , amefariki 09 / 01 mwaka huu
Unaweza ukanijuza mengi kuhusiana na hili jina la tamthilia lakini sipati info zake kwenye Google
Mpe hii kwanza👇Mwenye video la Tangazo la Chai Jabaaa, yule jamaa na domo lake kuubwa naliomba tafadhali, nshalitafuta hollaa
Walikuwa na tamthilia moja inaitwa Beast Master nilikuwa naipenda sanaKampuni ya IPP Limited mwaka 1994 inatambulisha chaneli ya Analog kwa jina ITV kupitia masafa ya mawimbi ya kawaida kipindi hiko.
Na kipindi hiko ndio mtaa mzima tumenunua TV ya PANASONIC TX iliyotoka 1993 sikumbuki model ikiwa ya rangi.
Kipindi hiko Tv inafunguliwa saa 8 au 10 sikumbuki ila inafungwa saa sita usiku.
Ndipo nilipo jua series kama:
*Family Matters
*Perfect Strangers
*fresh prince of bel air
*The V
Na matangazo kama :
*Revlon
*cocal cola
Kipindi hiko unaamka usiku kushuhudia ngumi za Mike Tyson.
Ila kuna dada mmoja ni kama mwarabu au muhindi fulani alikuwa ndo mtu wa kwanza ITV wanafungua ndo anaonekana sana. Hivi yupo wapi miaka 30 sasa.
Wenye kuijua ITV vizuri
[mention]pasco mayala [/mention] ni moja ya watu wenye kuijua ITV
Mtu yoyote mwenye mdomo mkubwa alikuwa akiitwa Chai JabaMwenye video la Tangazo la Chai Jabaaa, yule jamaa na domo lake kuubwa naliomba tafadhali, nshalitafuta hollaa
Enzi hizo hakuna flash wala CD, video mnaangalia kwa kutumia mikanda inataka kufanana na bibliaMimi nimeikuta channel 5.
Enzi hizo tunavizia ngoma kali, then tunaicopy kwenye ile mitofali.
Na ukichelewa kusyopisha itarecord hadi matangazo halafu wimbo uishe vibaya.
Kwahiyo mnakua attention kichizi, wimbo ukiisha tu chap mnaistopisha kurecord.
Ile mitofali tulikua tunachagua zile ambazo mzee anapenda na sisi hatupendi, zile nyimbo za kina defao, pepe kale, mbutalikasu and the likes.
Channel 5 ndo lilikua ting'a la vijana, huku RFA kila asubuhi ni lazima nisikilize.
Aisee namiss sana kipindi kile, ndo kipindi nilikua nina furaha ya kweli sio saivi nafake hadi furaha kudadadeki.