J. Edgar Hoover Mkurugenzi wa FBI na siri kubwa

J. Edgar Hoover Mkurugenzi wa FBI na siri kubwa

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
J. EDGAR HOOVER MKURUGENZI WA FBI NA "FILE" LA SIRI KUBWA

J. Edgar Hoover ndiye Mkurugenzi wa kwanza wa FBI na alikikalia kiti kwa nusu karne.

Lilikuwa jitu la mikasa likitisha na kuogopewa na kila mtu hadi maraisi wa Marekani wakimkalia mbali.

Alikuwa hawapendi akina Kennedy na akina Kennedy walikuwa hawampendi pia lakini wamfanye nini kwao alikuwa kidonda ndugu.

Robert Kennedy alikuwa Mwanasheria Mkuu wa serikali wakati kaka yake ndiye rais wa Marekani.

Hoover akapata fununu kuwa Robert ana mipango ya kumng'oa kwenye kiti chake.

Hoover akachukua file moja yaani jalada akampelekea Robert Kennedy akamwambia, "Soma jalada hilo na wala usipate tabu kunirudishia ukimaliza baki nalo mimi nina nakala."

Robert haraka sana alisitisha mpango wake wa kumng'oa Edgar Hoover kwenye kiti chake.

Siku moja Hoover yuko ofisini kwake anazungumza na rafiki yake mmoja akampa jalada akamwambia alisome.

Alipomaliza kulisoma akamtahadharisha vikali sana.

Akamwambia, "Eee bwana we hayo uliyosoma ala ala tafadhali usije ukamweleza mtu yeyote."

Edgar Hoover akalichukua lile file akaenda kuliweka kisha akarudia kumpa rafiki yake indhari kuhusu kutunza ile siri ndani ya lile file.

Yule jamaa akamgeukia Edgar Hoover mabega juu na mikono kamwelekezea Hoover viganja kaviweka kama anataka kupokea kitu uso umechukua sura ya mshangao mkubwa.

"File! akatamka kwa mshangao mkubwa anamtazama Hoover usoni jicho kwa jicho.

"Edgar, file gani hilo unalolizungumza?"

Kwa Kiingereza inakaa vyema.
Jamaa alisema, "File, what file?"

Edgar Hoover alibakia kucheka.
Kidagaa kabakianacho mwenyewe mfukoni.

Tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa hawa jamaa.
Screenshot_20201117-080109.jpg
 
Huyo bwege ndie aliewatesa sana blacks Marekani. Huyo bwege ndiye alifanya mipango ya kumuua Dr. Martin Luther King
Huyo bwege ndie alisimamia apartheid South Africa.

Yaani huyo bwege ana lawama kibao...hadi vita ya Vietnam. Huyo ndio mzandiki mwenyewe
 
Huyo bwege ndie aliewatesa sana black marekan. Huyo bwege ndiye alifanya mipango ya kumuua Dr. Martin Luther King
Huyo bwege ndie alisimamia apartheid South Africa.

Yaan huyo bwege ana lawama kibao, had vita ya vietnam. Huyo ndo mzandik mwenyew
Halafu inasemekana lilikuwa punga....na lilipenda kuvaa nguo za kike.

20201117_003616.jpg
 
Alikuwa gay halafu..alikuwa na bwana wake hapo hapo FBI..
Waliokuwa wanajua walimbatizw jina moja la kike..
Ingawa alikuwa anaogopwa na Marais hadi Mafia..
Huwa tunajua machoko ni watu dhaifu Sana, kwanini yeye aliogopwa sana Hadi na makundi ya Kimafia?
 
Alikuwa gay halafu..alikuwa na bwana wake hapo hapo FBI..
Waliokuwa wanajua walimbatizw jina moja la kike..
Ingawa alikuwa anaogopwa na Marais hadi Mafia..
Huyu ndie alie fanya u Gay uwe na nguvu sana USA. Maana kila alieupinga hadharani alihakikisha anamshusha chini awe mwanasiasa au mwanamziki or mtu yoyote mashuhuri.
 
Huyu ndie alie fanya u Gay uwe na nguvu sana USA. Maana kila alieupinga hadharani alihakikisha anamshusha chini awe mwanasiasa au mwanamziki or mtu yoyote mashuhuri.
Hii sijui Una link yoyote niifatilie?
 
Huwa tunajua machoko ni watu dhaifu Sana, kwanini yeye aliogopwa sana Hadi na makundi ya Kimafia?
Gayness does not mean weakness kuna watawala wengi wababe halafu walikua mapunga. Kuna tetesi pia Shaka Zulu na ubabe wake wote alikua shoga.
 
Indeed he was a powerful man. But with his flaws. It is believed, he was a homosexual who didn't want people to know.
Kwa maana hiyo basi, hilo file unalosema Lina siri nzito, ni file kama mafaili mengine. Inategemea hiyo siri inamuhusu nani.
 
Robert Kennedy anasema siku ambayo kaka yake JF Kennedy kapigwa risasi Hoover ndiye alimpigia simu kumpa taarifa. Hakuna cha salamu akaanza kumwambia "The President has been shot" akakata simu. Baada ya muda akapiga tena simu akasema "The President is dead" akakata simu bila hata kutoa pole. Robert anasema Hoover alimpa hiyo taarifa huku akionekana kama mtu mwenye furaha sana kwa yaliyomkuta J.F. Kennedy.

Yeye ndiyo muasisi wa mchezo wa kijasusi unaoitwa "Bad-Jacket" ambao ulitumika dhidi ya wanaharakati wa The Black Panthers na Civil Rights Movements. Inatengenezwa barua ambayo inaonekana ina mwandiko wa mwanaharakati moja, huku ikionesha kwamba anashirikiana na F.B.I kisha inaenda kutupwa kwenye gari la mwanaharakati mwingine ionekane aliisahau.

Barua ikashafunguliwa basi mtafaruku na kutoaminiana kunaanza. Huu mchezo alichezewa marehemu Stokley Carmichael a.k.a Kwame Toure. Baada ya kufanya hivyo The Black Panthers wakamfukuza kwasababu alionekana ni kibaraka wa wazungu kumbe ni mpango wa Hoover.
 
Back
Top Bottom