BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,165
Jaji Bomani azilipua Kampuni za madini Tuesday, 19 April 2011 09:31
Ramadhan Semtawa
Mwananchi
MWANASHERIA Mkuu Mstaafu Jaji Mark Bomani, amezitaka kampuni za madini nchini kuwekeza asilimia 50 ya mapato yao ya fedha za kigeni kwenye benki za ndani ili kunusuru shilingi.
Kauli hiyo ya Jaji Bomani ambaye aliwahi kuongoza Kamati ya Rais ya Kudurusu mikataba ya madini, inakuja kipindi ambacho maliasili hiyo imetajwa kutonufaisha nchi kichumi kutokana na Sheria ya Madini ya 1998 inayotoza mrahaba wa asilimia tatu.
Akizungumza katika mahojiano maalumu ofisini kwake wiki iliyopita, Jaji Bomani alisema tayari amefikisha hoja hiyo kwa wadau husika baada ya kuona utajiri wa madini haunufaishi nchi kwa kiasi kikubwa.
Bomani alisema thamani ya shilingi dhidi ya fedha za kigeni inazidi kushuka na kuongeza, "sasa hivi thamani ya dola moja ya Marekani ni sawa na takribani Sh1,500."
Alisisitiza kwamba fedha za kigeni zinazoingia nchini hazitoshi ikilinganishwa na mahitaji ya nchi na wananchi wake na kuweka bayana, hiyo inatokana na kuwepo kwa mianya mingi.
Mikataba ya madini
"Mojawapo ya mianya hiyo ni ruhusa iliyotolewa na serikali kwa Kampuni za madini ya dhahabu kutorejesha nchini fedha zinazotokana na mauzo ya dhahabu nje. Miaka ya 1990 serikali ilitiliana saini na kampuni kadhaa za madini, mikataba ambayo ilizipa ruksa kampuni hizo ya kutorejesha nchini fedha zao za mauzo ya kigeni," alifafanua.
Kwa mujibu wa mzee Bomani, wakati mikataba hiyo ikitiwa saini bei ya dhahabu ilikuwa chini ambayo ni dola za Marekani 260 kwa wakia lakini, leo hii bei ya dhahabu ni dola za Marekani 1,500 kwa kila wakia.
Akikazia katika eneo hilo, Jaji Bomani alisema, "Maana yake ni kwamba kampuni za madini zinapata mapato ya juu kweli kweli." (Na Tanzania inaambulia vijisenti tu!)
Mwanasheria huyo nguli, alisema sababu za masahama huo kwa kipindi hicho ilikuwa kuwahakikishia wawakezaji kwamba wakati wote wangekuwa na akiba ya fedha zao nje kwa ajili ya manunuzi kwani walikuwa na matumizi makubwa.
Bomani alihoji, "Je, msamaha huo bado unahitajika kweli katika hali ya bei ya sasa ya dhahabu ambayo ni karibu mara tano ya bei ya wakati huo, ikizingatiwa matumizi makubwa makubwa yamepungua?"
Aliongeza, "hivi karibuni kampuni ya African Barrick Gold ilitoa taarifa yake ya mwaka 2010, ikitamba mambo yalikuwa mazuri kweli kweli! Hata kama kampuni hizi bado zina msamaha huo uliotolewa zaidi ya miaka kumi iliyopita, haziwezi zenyewe kwa kuzingatia mahitaji ya nchi, zikarejesha nchini angalau sehemu ya mapato hayo, hata kama serikali inazionea huruma au haya?" (Mhhhh! Wachukuaji hawa wanachota tu!)
Mauzo ya madini mwaka 2010
Jaji Bomani alisema mwaka jana thamani ya dhahabu iliyouzwa nje ya nchi ilikuwa zaidi ya dola 1.4 bilioni za Marekani na kwamba, "kampuni hizi zingekuwa zimerejesha asilimia 50 tu ya mapato yake zingekuwa zimerejesha nchini zaidi ya dola 700. milioni za Marekani (takriban sh 1.2trilioni).
Alisema ukiongeza mapato yanayotokana na na vyanzo vingine kama utalii, uuzaji wa bidhaa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na uuzaji mazao ya kilimo na misaada mbalimbali nchi ingekuwa imejipatia dola nyingi na shilingi ingeendelea kubaki imara.
Ramadhan Semtawa
Mwananchi
MWANASHERIA Mkuu Mstaafu Jaji Mark Bomani, amezitaka kampuni za madini nchini kuwekeza asilimia 50 ya mapato yao ya fedha za kigeni kwenye benki za ndani ili kunusuru shilingi.
Kauli hiyo ya Jaji Bomani ambaye aliwahi kuongoza Kamati ya Rais ya Kudurusu mikataba ya madini, inakuja kipindi ambacho maliasili hiyo imetajwa kutonufaisha nchi kichumi kutokana na Sheria ya Madini ya 1998 inayotoza mrahaba wa asilimia tatu.
Akizungumza katika mahojiano maalumu ofisini kwake wiki iliyopita, Jaji Bomani alisema tayari amefikisha hoja hiyo kwa wadau husika baada ya kuona utajiri wa madini haunufaishi nchi kwa kiasi kikubwa.
Bomani alisema thamani ya shilingi dhidi ya fedha za kigeni inazidi kushuka na kuongeza, "sasa hivi thamani ya dola moja ya Marekani ni sawa na takribani Sh1,500."
Alisisitiza kwamba fedha za kigeni zinazoingia nchini hazitoshi ikilinganishwa na mahitaji ya nchi na wananchi wake na kuweka bayana, hiyo inatokana na kuwepo kwa mianya mingi.
Mikataba ya madini
"Mojawapo ya mianya hiyo ni ruhusa iliyotolewa na serikali kwa Kampuni za madini ya dhahabu kutorejesha nchini fedha zinazotokana na mauzo ya dhahabu nje. Miaka ya 1990 serikali ilitiliana saini na kampuni kadhaa za madini, mikataba ambayo ilizipa ruksa kampuni hizo ya kutorejesha nchini fedha zao za mauzo ya kigeni," alifafanua.
Kwa mujibu wa mzee Bomani, wakati mikataba hiyo ikitiwa saini bei ya dhahabu ilikuwa chini ambayo ni dola za Marekani 260 kwa wakia lakini, leo hii bei ya dhahabu ni dola za Marekani 1,500 kwa kila wakia.
Akikazia katika eneo hilo, Jaji Bomani alisema, "Maana yake ni kwamba kampuni za madini zinapata mapato ya juu kweli kweli." (Na Tanzania inaambulia vijisenti tu!)
Mwanasheria huyo nguli, alisema sababu za masahama huo kwa kipindi hicho ilikuwa kuwahakikishia wawakezaji kwamba wakati wote wangekuwa na akiba ya fedha zao nje kwa ajili ya manunuzi kwani walikuwa na matumizi makubwa.
Bomani alihoji, "Je, msamaha huo bado unahitajika kweli katika hali ya bei ya sasa ya dhahabu ambayo ni karibu mara tano ya bei ya wakati huo, ikizingatiwa matumizi makubwa makubwa yamepungua?"
Aliongeza, "hivi karibuni kampuni ya African Barrick Gold ilitoa taarifa yake ya mwaka 2010, ikitamba mambo yalikuwa mazuri kweli kweli! Hata kama kampuni hizi bado zina msamaha huo uliotolewa zaidi ya miaka kumi iliyopita, haziwezi zenyewe kwa kuzingatia mahitaji ya nchi, zikarejesha nchini angalau sehemu ya mapato hayo, hata kama serikali inazionea huruma au haya?" (Mhhhh! Wachukuaji hawa wanachota tu!)
Mauzo ya madini mwaka 2010
Jaji Bomani alisema mwaka jana thamani ya dhahabu iliyouzwa nje ya nchi ilikuwa zaidi ya dola 1.4 bilioni za Marekani na kwamba, "kampuni hizi zingekuwa zimerejesha asilimia 50 tu ya mapato yake zingekuwa zimerejesha nchini zaidi ya dola 700. milioni za Marekani (takriban sh 1.2trilioni).
Alisema ukiongeza mapato yanayotokana na na vyanzo vingine kama utalii, uuzaji wa bidhaa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na uuzaji mazao ya kilimo na misaada mbalimbali nchi ingekuwa imejipatia dola nyingi na shilingi ingeendelea kubaki imara.