Jaji Manento: Rais apunguziwe mamlaka uteuzi wa Majaji

Jaji Manento: Rais apunguziwe mamlaka uteuzi wa Majaji

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Jaji Kiongozi mstaafu, Amir Manento amependekeza Katiba iweke udhibiti kwa Rais asiwe na mamlaka ya kuteua majaji nje ya mapendekezo ya Tume ya Utumishi wa Mahakama. Manento alitoa mapendekezo hayo jana kwa kwa Tume ya Haki Jinai, iliyoundwa па Rais Samia Suluhu Hassan, kuangalia jinsi ya kuboresha mfumo na taasisi zinazosimamia haki jinai, inayoongozwa na Jaji Mkuu mstaafu, Mohamed Chande.

Akizungumza па waandishi wa habari baada ya kuwasilisha mapendekezo hayo kwa Tume hiyo, Jaji Manento alisema kuwa ingawa Tume ya Utumishi wa Mahakama hupendekeza majina ya majaji, lakini Katiba inampa Rais mamlaka ya kuteua majaji hata nje ya orodha inayopendekezwa.

Ibara ya 109 ya Katiba inasema kuwa majaji watateuliwa na Rais kwa kushauriana na Tume ya Utumishi wa Mahakama.

"Rais hatakiwi kushughulikia mambo ya kitaaluma, yeye ni mwanasiasa, anaweza akateua majaji wa kisiasa. Haki haitatendeka wala haitaonekana inatendeka ingawa ni jaji. Waachiwe wataalamu wa sheria, vigezo ni vingi kwa sababu nilikuwa huko."

"Tunaangalia hukumu zako, mwonekano wako mbele ya watu, lugha unayotumia, je, unawafokea, unawatisha na heshima yako.

"Sasa leo unamwachia Rais, na washauri wake ni wanasiasa, haki haitatendeka," alisema.

Rais mstaafu wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Dk Rugemeleza Nshala alisema "Tume inashauri tu, anayeteua ni Rais. Kwa hiyo. ushauri si lazima ufuatwe.

Kwa upande mwingine, Jaji Maneno alipendekeza kuwepo na chombo kinachosimamia utekelezaji wa haki za jinai.

Pia chombo hicho kiwe chini ya Mahakama akisema kwamba kwa mfumo wa Mahakama kitakuwa huru, kwani polisi wanakiuka haki tangu kukamata watu.​
 
Katiba itamka Rais lazima afate ushauri, iwe lazima
 
 
Hivi Judge kama huyu anastaafu ili iweje....

Nafikiri majaji na madaktar hawatakiw wastaafu, offcourse na maprofessa, wanapozeeka ndipo wanakuwa na akili zaidi.

Hili la Judge Munento limeongelewa sana.
 
Kusema kweli majaji wanatakiwa kuteuliwa na jopo maalumu na kuthibitishwa na Bunge.
Majaji wa Tz wamekuwa wakiteuliwa kisiasa hivyo kuharibu tasnia heshima ya majaji duniani!
Wamekuwa wakitoa hukumu kuendana na mihemko ya kiasiasa badala ya haki na weledi.
 
Kusema kweli majaji wanatakiwa kuteuliwa na jopo maalumu na kuthibitishwa na Bunge.
Majaji wa Tz wamekuwa wakiteuliwa kisiasa hivyo kuharibu tasnia heshima ya majaji duniani!
Wamekuwa wakitoa hukumu kuendana na mihemko ya kiasiasa badala ya haki na weledi.
Jaji Mkuu Prof Ibrahim Juma

" Majaji wafanye maamuzi kulingana na mwenendo wa Serikali"

Niliposikia hivi nikasema Mbinguni Majaji na mahakimu Tanzania wataisikia tu.
 
Kipengele cha Katiba kinachompa Rais mamlaka ya kuteua majaji nje ya mapendekezo ya tume ya utumishi wa Mahakama ndiyo kilimpa Magufuli kibri cha kutujazia majaji wa mchongo wanaofanya Mahakama idharauliwe.
 
Kipengele cha Katiba kinachompa Rais mamlaka ya kuteua majaji nje ya mapendekezo ya tume ya utumishi wa Mahakama ndiyo kilimpa Magufuli kibri cha kutujazia majaji wa mchongo wanaofanya Mahakama idharauliwe.
😅😅😅kweli
 
Hakuna watu wanaokula rushwa kama mahakimu
Yaani ndugu yangu kauwawa na ushahidi upo unakuta baada ya mda muuwaji yuko mtaani kisa hakim kapewa 20m kwa roho ya mtu

Watajuana wenyewe
Wakati yule alikuwa anawapandisha vyeo kisa mtu kawaweka ndani wapinzani, wao waliufyata
 
Nashangaa nchi za Kiafrika, anateuliwa mtu kisiasa badala ya taaluma. Mf. Wazara ya afya ukiweka mwanasiasa na wizara inakufa. Weka mtu aliyebobea katika udaktari ili madokta wakiongea jambo ajue wanasema nini. Mwanasiasa anaishia kugonga mezani tu "unanijua mimi ni nani"
 
Hawa wazee wakistaafu ndio akili zinaongezeka

..Jaji Manento akiwa Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu aliingilia kati suala la kifo cha mwandishi Daudi Mwangosi na kutoa ripoti iliyobainisha ukweli kuhusu tukio lile. Serikali ilikuwa inajaribu kusema uongo.

..labda kuna wanaomfahamu zaidi, lakini ktk tukio lile na ripoti aliyotoa nadhani ni Jaji mwenye msimamo na aliyenyooka ktk haki.
 
Back
Top Bottom