Wakati Kamati ya uongozi ya chama cha wananchi CUF, inayoongozwa na mpiganaji Julius Mtatiro kama mwenyekiti na watetezi wengine wa maslahi ya chama cha wananchi CUF dhidi ya kibaraka wa CCM Profesa Ibrahim Lipumba anayeshirikiana na Msajili wa vyama vya siasa kama wakala wa serikali kuihujumu CUF na kudhoofisha upinzani nchini ikiendelea kumtuhumu Jaji Mutungi kushirikiana na Lipumba kuiba Milioni 360 za chama cha CUF.
Tayari Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa Hesabu za serikali amemtia hatiani jaji Mutungi kwa kulitia hasara serikali na ofisi yake inayoendeshwa na kodi za wananchi kwa kufanya utapeli wa zaidi ya shilingi milioni 600.
‘’Msajili wa Vyama vya Siasa alifanya Ununuzi wa Consultancy Services juu ya utoaji wa Usalama wa Anga, Usalama na Stadi za maisha kwa shilingi 668,000,000’’. Inasema ripoti ya CAG
MASWALI
1. Je Msajili wa Vyama vya siasa ni Mtaalamu wa masuala ya Anga siku hizi
2. Msajili wa vyama tangu lini amekuwa na huo ujuzi wa masuala ya anga
3. Msajili wa vyama vya siasa ni mjuzi wa mambo ya stadi za maisha
4. Kwanini Rais Magufuli anaendelea kuwakumbatia wasaidizi wanaomchafua kama huyu?
5. ONGEZEA WEWE MWENYEWE
taarifa zaidi naendelea kuzikusanya na nitazishusha humu humu SOON.