Jaji Warioba: Hivi tunaposema Katiba siyo kipaumbele, sababu ni nini?

Jaji Warioba: Hivi tunaposema Katiba siyo kipaumbele, sababu ni nini?

macho_mdiliko

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2008
Posts
25,191
Reaction score
48,765
Jaji Warioba ametoa mawazo mazuri sana kuhusu katiba mpya. Ameuliza tunaposema katiba siyo kipaumbele ina maana gani wakati katiba ilibakia kipengele cha kupiga kura tu?

Ameenda mbali zaidi na kusema tukiendelea na kisingizio hiki, hata ikifika mwaka 2024 au 2025 tutasema tena hivyo hivyo.

Kwa ujumla ana mawazo mazuri sana.

Msikilize:
 
Uzuri ni Kwamba wanaosema katika si kipaumbele sasa hivi wana watu wengi na kwa vyovyote vile watakuwa na maamuzi kupitia wingi wa kura za wajumbe na wananchi!

Wanaopiga kelele za kutaka katiba mpya, ambao naamini agenda yao iliyojificha ni kusaka madaraka tu, hawana chao hata ikikubaliki tuendelee na mchakato wa katiba. Tegemeo lao ni kuleta vurugu ili wapate upenyo wa kulazimisha agenda zao.

Mambo yakiwa kama kawaida, matakwa ya walio wengi yapewe njia, bado watapiga kelele tu. Sababu ukizungumza katiba mpya ni nini ambacho walio wengi wataridhia kiwemo. Na siyo wanachotaka wao kiwemo. Nawakumbusha tu mchakato wa katiba mpya uliopita. Mpaka ikapelekea wakakimbia bunge maalumu la katiba.
 
INTRODUCTION

Nimefuatilia kuhusu kuandika katiba Mpya ambalo ni takwa la watanzania wengi, nikajiridhisha kwamba, kama CCM ikiwa madarakani katiba Mpya ni haiwezekani.

MAIN BODY
Kwa sababu katika mataifa yote yalifanikiwa kuandika katiba Mpya, mambo mawili au matatu yametokea kwanza ndo Katiba mpya ikatokea!

Mosi; Msuguano wa kimawazo! Serikali ikiona suala la katiba nompya kutokuwa kipaumbele na wananchi wakiona kama kipaumbele baada ya kuridhika kwamba katiba imepoka mamlaka ya wanachi na kuyarundika katika mhimili mmoja unaoitwa serikali! Tanzania kwa Sasa iko katika hatua hii. Freeman Aikaeli Mbowe, anajaribu kusuguana na serikali kifikra! Na serikali ambayo imeshaonja utamu wa Katiba iliyopo inakuwa haionekani kujifunza wala kuchukua mawazo mbadala kuelekea katiba mpya, bali kutumia kila njama kuaminisha jamii kuwa suala hilo halina msingi kwa Sasa, na kufanya hivo ni chokochoko! Tunatakiwa kuvuka hapa twende hatua ya pili.

Pili, Kuvurugana kinguvu! Mbwai mbwai (sitamani itokee), lakini ni hatua! Kote ambako katiba Mpya imeandikwa kumetokea timbwili la Asha Ngedere kwanza ndo Katiba ikaandikwa! Fuatilia Kenya, na hata Zanzibar! Kimeumana kwanza ndo akili ya Viongozi ikakaa sawa! Siamini kama ni njia nzuri, lakini kwa uzoefu ipo katika hatua za kuitafuta na kuipata katiba Mpya! Kuna wakati mwalimu wangu wa history aliuliza why armed struggle, jibu lilikuwa rahisi tu, Failure of peaceful means! If you fail to provide the required demands of the society peacefully, they can try it through bloodshed! Tuwe makini! Kisiwa cha uvumilivu kina mipaka, kina ukomo!

Tatu, Kuondolewa chama Tawala Madarakani. Ni ngumu sana kuandika katiba Mpya Kama chama dola , ambacho kinanufaika na katiba iliyopo kikiwa Madarakani. Wakifanya hivo, ujue katiba hiyo itakuwa imepakwa rangi tu. Itakuwa ni Calorite kwenye ngozi ya mtu mweusi! Hivyo, jukumu letu kubwa ni kupigania kwanza kukiondosha chama Tawala. Maana hata katiba iliyopendekezwa si ile ya Warioba. Imechakachuliwa! Imepakwa rangi! Hivyo jambo kubwa ni box la kura, ambalo nalo halina haki ndani yake, kutokana na ukweli kwamba katiba iliyopo haitoi nafasi kwa vyama mbadala kushinda , hata kama wananachi wataamua tofauti!

HITIMISHO
Namba moja ni uchochezi na chokochoko na ugaidi. Namba mbili, kisiwa cha uvumilivu kilishajengewa hofu tangu enzi za Mwl, na kufundishwa kumuachia Mungu. Namba tatu, Mwamzi ni yule Mtoto wa chama dola! Haiwezi kumwangusha Baba, wala mama! Kwa hiyo, hata mimi sijui[emoji3]!


USHAURI!
Free Mbowe! Aendelee kutoa elimu, ili isaidie upatikanaji wa Katiba mpya kwa njia ya kwanza!

Ahsante
 
Taarifa za umbea zinasema kuwa CDM wamemkosea mama yetu na kama hawataomba RADHI kwa herufi kubwa na kumtambua yeye ni MKUU na sio "mwambie yule mama yenu kuwa wembe ule nilioutumia kumnyolea mwenzake,nitautumia kumnyolea", basi hali itaendelea namna hii;

Nafurahi hali iwe namna hii tena na vijana wa igipi 0 waendelee kuwakamata hadi wote wajae mahakamani; kwani 2025 kunaUCHAGUZI au ni kugawana majimbo na kuchukua fomu na kupita bila kupingwa ili tupate maendeleo maana MIKOA kama ARUSHA NA MOSHI ambapo hao wakora wamekuwa wanashinda wapo nyuma KIMAENDELEO kulinganisha na LINDI,SINGIDA,DODOMA au MPANDA ambapo Chama chetu hushinda ZAIDI? Yaani Dar ipo juu kiuchumi kwa sababu chama tawala kimekuwa madarakani lakini wale jamaa wakikamata majimbo maendeleo yanarudi nyuma.
 
Uzuri ni Kwamba wanaosema katika si kipaumbele sasa hivi wana watu wengi na kwa vyovyote vile watakuwa na maamuzi kupitia wingi wa kura za wajumbe na wananchi!

Wanaopiga kelele za kutaka katiba mpya, ambao naamini agenda yao iliyojificha ni kusaka madaraka tu, hawana chao hata ikikubaliki tuendelee na mchakato wa katiba. Tegemeo lao ni kuleta vurugu ili wapate upenyo wa kulazimisha agenda zao.

Mambo yakiwa kama kawaida, matakwa ya walio wengi yapewe njia, bado watapiga kelele tu. Sababu ukizungumza katiba mpya ni nini ambacho walio wengi wataridhia kiwemo. Na siyo wanachotaka wao kiwemo. Nawakumbusha tu mchakato wa katiba mpya uliopita. Mpaka ikapelekea wakakimbia bunge maalumu la katiba.

Warioba naye anataka katiba mpya, na yeye anataka madaraka gani? Hoja za maiti hai hizi.
 
Uzuri ni Kwamba wanaosema katika si kipaumbele sasa hivi wana watu wengi na kwa vyovyote vile watakuwa na maamuzi kupitia wingi wa kura za wajumbe na wananchi!

Wanaopiga kelele za kutaka katiba mpya, ambao naamini agenda yao iliyojificha ni kusaka madaraka tu, hawana chao hata ikikubaliki tuendelee na mchakato wa katiba. Tegemeo lao ni kuleta vurugu ili wapate upenyo wa kulazimisha agenda zao.

Mambo yakiwa kama kawaida, matakwa ya walio wengi yapewe njia, bado watapiga kelele tu. Sababu ukizungumza katiba mpya ni nini ambacho walio wengi wataridhia kiwemo. Na siyo wanachotaka wao kiwemo. Nawakumbusha tu mchakato wa katiba mpya uliopita. Mpaka ikapelekea wakakimbia bunge maalumu la katiba.
Katiba mpya haikwepeki. Hakuna wa kuikwamisha. Polisi wanatusaidia sana kufanya campaign. Amen
 
Back
Top Bottom