Pre GE2025 Jaji Warioba: Kulikuwepo na dosari kubwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020

Pre GE2025 Jaji Warioba: Kulikuwepo na dosari kubwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wanabodi, kwa kauli hii ya Jaji Warioba ndio kusema kwamba CCM wanaanza kukubali mmoja mmoja kwamba walipora uchaguzi au kuna namna hatujamuelewa mzee wetu?

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Jaji Joseph Sinde Warioba wakati anaongea na wanahabari hivi karibuni amedokeza na kukubali kuwa chaguzi ndogo za serikali za mitaa za mwaka 2020 pamoja na uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 ulikuwa na dosari kubwa.

Soma pia: Nape Nnauye: Matokeo ya kura inategemea nani anahesabu na nani anatangaza, ili mradi ukimaliza unasema Mungu nisamehe!

Jaji Warioba alidokeza kuwa ni kawaida kwa uchaguzi wowote duniani kuwa na kasoro lakini kwa chaguzi za mwaka 2019 na 2020 dosari zake zilikuwa ni kubwa kupita kiasi na ziliwafanya washtuke.

"Ni kweli kwamba kila uchaguzi una dosari. Hakuna uchaguzi mahali popote duniani ambao hauna dosari. Lakini zinakuwa ni dosari za kawaida. Zinakuwa ni dosari ndogo ndogo zinashughulikiwa. Kwenye chaguzi unaofuata unakuwa ni mzuri zaidi."

Jaji Warioba aliongeza kwa kusema:

"Uchaguzi unaokuja tunauzungumza sana kwa sababu ya matukio ya 2019 na 2020. Dosari za uchaguzi wa serikali za mitaa kwa mwaka 2019 na uchaguzi wa mwaka 2020 zilikuwa ni kubwa na zilifanya tushtuke."

Source: Jambo TV
 
Wanabodi, kwa kauli hii ya Jaji Warioba ndio kusema kwamba CCM wanaanza kukubali mmoja mmoja kwamba walipora uchaguzi au kuna namna hatujamuelewa mzee wetu?

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Jaji Joseph Sinde Warioba wakati anaongea na wanahabari hivi karibuni amedokeza na kukubali kuwa chaguzi ndogo za serikali za mitaa za mwaka 2020 pamoja na uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 ulikuwa na dosari kubwa.

Soma pia: Jaji Warioba: Viongozi wengi waliochaguliwa siyo wale wanaotakiwa na Wananchi

Jaji Warioba alidokeza kuwa ni kawaida kwa uchaguzi wowote duniani kuwa na kasoro lakini kwa chaguzi za mwaka 2019 na 2020 dosari zake zilikuwa ni kubwa kupita kiasi na ziliwafanya washtuke.

"Ni kweli kwamba kila uchaguzi una dosari. Hakuna uchaguzi mahali popote duniani ambao hauna dosari. Lakini zinakuwa ni dosari za kawaida. Zinakuwa ni dosari ndogo ndogo zinashughulikiwa. Kwenye chaguzi unaofuata unakuwa ni mzuri zaidi."

Jaji Warioba aliongeza kwa kusema:

"Uchaguzi unaokuja tunauzungumza sana kwa sababu ya matukio ya 2019 na 2020. Dosari za uchaguzi wa serikali za mitaa kwa mwaka 2019 na uchaguzi wa mwaka 2020 zilikuwa ni kubwa na zilifanya tushtuke."

Source: Jambo TV
warioba ni mkabila na nani asiyejua kua kwa sasa yupo bega kwa bega na chama chao cha kaskazini
 
Kura zlikuwa zinapigwa na kuhesabiwa maporini

1000012666.jpg
 
Tanzania huwa tuna Uchafuzi hatujawahi kuwa na uchaguzi toka enzi za picha ya Jembe na Nyundo vs Mwalimu.
 
Back
Top Bottom