Jaji Warioba: Mawaziri wasitokane na Wabunge

Jaji Warioba: Mawaziri wasitokane na Wabunge

Papaa Mobimba

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2018
Posts
882
Reaction score
3,337
Jaji Warioba akihojiwa na Mwananchi Digital Aprili 7, 2024. amesema kuwa Mawaziri wasitokane na wabunge,

"Bunge liwe ni bunge, serikali isiingiliane na bunge, na vizuri mawaziri wasiwe kwenye bunge, mbunge asiwe waziri. Wakati tulipopata uhuru na hasa tulipobadili katiba tukawa Jamhuri, Rais alipewa madaraka mengi sana, Rais wakati ule alikuwa na madaraka makubwa kwanza kulikuwa na sheria ambazo zinampa madaraka ya kuwatia watu kizuizini bila kupitia utaratibu wa Mahakama, alikuwa na uwezo wa kuwahamisha watu kutoka sehemu moja kwenda nyingine na ikatungwa sheria ambayo ilimpa madaraka hayo ya kuwatia watu kizuizini"

"Kwa upande wa uteuzi, Rais mwenyewe alisema kwamba anateua watu wengi mno ambao hawafahamu wala hawasimamii nidhamu yao haisimamii, akaona kwa utaratibu ule kulikuwa na hatari ya kuteua watu ambao hawana sifa au uwezo, zikawa zinaingia hata dalili za rushwa kwamba kwa kuwa ni Rais ndiye anayeteua na kuletewa mapendekezo na watu wengi inawezekana mtu akaenda akamhonga kiongozi fulani ili apigiwe debe ateuliwe ama mtu ana jamaa yake anaona amsaidie anakwenda kumpigia debe akasema hapana"
 
Hili hata mm nililiona, how comez waziri awe mbunge.
Na sifa za mbunge ni ajue kusoma na kuandika, huyu anaejua kusoma na kuandika uende kumpa uwaziri wa fedha, mtu wa kubwabwaja.

Kuna nafasi ambazo wasingewekwa wanasiasa ila watu wenye taaluma hiyo.
 
Ana mapendekezo gani sasa namna ya kuwapata mawaziri na viongozi wengine ngazi za uteuzi?
 
Sio dawa, majaji hawatokani na chama na serekali lkn unaona zaidi.muulize Mbowe. Kikubwa ni kuwapata wacha Mungu wanaojua baada ya maisha kuna kufa na kuna kulipwa

Jaji Warioba akihojiwa na Mwananchi Digital Aprili 7, 2024. amesema kuwa Mawaziri wasitokane na wabunge,

"Bunge liwe ni bunge, serikali isiingiliane na bunge, na vizuri mawaziri wasiwe kwenye bunge, mbunge asiwe waziri. Wakati tulipopata uhuru na hasa tulipobadili katiba tukawa Jamhuri, Rais alipewa madaraka mengi sana, Rais wakati ule alikuwa na madaraka makubwa kwanza kulikuwa na sheria ambazo zinampa madaraka ya kuwatia watu kizuizini bila kupitia utaratibu wa Mahakama, alikuwa na uwezo wa kuwahamisha watu kutoka sehemu moja kwenda nyingine na ikatungwa sheria ambayo ilimpa madaraka hayo ya kuwatia watu kizuizini"

"Kwa upande wa uteuzi, Rais mwenyewe alisema kwamba anateua watu wengi mno ambao hawafahamu wala hawasimamii nidhamu yao haisimamii, akaona kwa utaratibu ule kulikuwa na hatari ya kuteua watu ambao hawana sifa au uwezo, zikawa zinaingia hata dalili za rushwa kwamba kwa kuwa ni Rais ndiye anayeteua na kuletewa mapendekezo na watu wengi inawezekana mtu akaenda akamhonga kiongozi fulani ili apigiwe debe ateuliwe ama mtu ana jamaa yake anaona amsaidie anakwenda kumpigia debe akasema hapana"
 
Kama "the state" mnasoma komenti hii!

mtambue ya kuwa Mzee warioba,Butiku na wengineo siku zao zinamiminika sana hawana muda tena !muda sio mrefu watatuacha !

nawaombeni kabla hawajafa Hawa wazee wapewe kiu yao waache legacy wasije wakafa kabla ya katiba mpya kupatikana !maiti zao zitagoma kututiii wakati wa maziko!

tutimize kiu yao kabla hawajaondoka Duniani

fanyeni hima kabla hawajaitwa,wameshaona makosa waliyoyafanya Kwa kupitisha katiba hii wanataka wafanye masahihisho!!!

someni mtambue wakati ni ukuta!
 
Subiri ile misukule, chawa, mapopoma, wachawi, na wasiokuwa wazalendo ije hapa utasikia wanasema "huyu mzee akae kimya, ashawahi kuwa waziri nk nk" ndo mtajua wa Tz wengi bado ni wapumbavu sana na ndio mtaji wa CCM
 
Sio dawa, majaji hawatokani na chama na serekali lkn unaona zaidi.muulize Mbowe. Kikubwa ni kuwapata wacha Mungu wanaojua baada ya maisha kuna kufa na kuna kulipwa
Kenya wameweza iwepo Tume ya kuteua majaji na sio Raisi
 
Jaji Warioba akihojiwa na Mwananchi Digital Aprili 7, 2024. amesema kuwa Mawaziri wasitokane na wabunge,

"Bunge liwe ni bunge, serikali isiingiliane na bunge, na vizuri mawaziri wasiwe kwenye bunge, mbunge asiwe waziri. Wakati tulipopata uhuru na hasa tulipobadili katiba tukawa Jamhuri, Rais alipewa madaraka mengi sana, Rais wakati ule alikuwa na madaraka makubwa kwanza kulikuwa na sheria ambazo zinampa madaraka ya kuwatia watu kizuizini bila kupitia utaratibu wa Mahakama, alikuwa na uwezo wa kuwahamisha watu kutoka sehemu moja kwenda nyingine na ikatungwa sheria ambayo ilimpa madaraka hayo ya kuwatia watu kizuizini"

"Kwa upande wa uteuzi, Rais mwenyewe alisema kwamba anateua watu wengi mno ambao hawafahamu wala hawasimamii nidhamu yao haisimamii, akaona kwa utaratibu ule kulikuwa na hatari ya kuteua watu ambao hawana sifa au uwezo, zikawa zinaingia hata dalili za rushwa kwamba kwa kuwa ni Rais ndiye anayeteua na kuletewa mapendekezo na watu wengi inawezekana mtu akaenda akamhonga kiongozi fulani ili apigiwe debe ateuliwe ama mtu ana jamaa yake anaona amsaidie anakwenda kumpigia debe akasema hapana"

Yaani sasa hivi katika nafasi zile za juu tungekuwa na mtu hata mmoja mwenye akili, upeo na uzalendo, japo nusu ya huyu mheshimiwa sana Jaji Warioba, nchi tayari tungekuwa na katiba nzuri ya kupigiwa mfano Afrika nzima.
 
Ngoja chawa na viroboto waje...si ajabu wakamhusisha na Chadema

Haitashamgaza. Maana siku hizi kila mwenye akili kubwa au mwenye mawazo ya kizalendo, hata awe mwanaCCM mwasisi, machawa yatahusisha na CHADEMA, kama vile kuwa mwanaCCM hustahili kuwa na akili wala uzalendo kwa nchi yako.
 
Jaji Warioba akihojiwa na Mwananchi Digital Aprili 7, 2024. amesema kuwa Mawaziri wasitokane na wabunge,

"Bunge liwe ni bunge, serikali isiingiliane na bunge, na vizuri mawaziri wasiwe kwenye bunge, mbunge asiwe waziri. Wakati tulipopata uhuru na hasa tulipobadili katiba tukawa Jamhuri, Rais alipewa madaraka mengi sana, Rais wakati ule alikuwa na madaraka makubwa kwanza kulikuwa na sheria ambazo zinampa madaraka ya kuwatia watu kizuizini bila kupitia utaratibu wa Mahakama, alikuwa na uwezo wa kuwahamisha watu kutoka sehemu moja kwenda nyingine na ikatungwa sheria ambayo ilimpa madaraka hayo ya kuwatia watu kizuizini"

"Kwa upande wa uteuzi, Rais mwenyewe alisema kwamba anateua watu wengi mno ambao hawafahamu wala hawasimamii nidhamu yao haisimamii, akaona kwa utaratibu ule kulikuwa na hatari ya kuteua watu ambao hawana sifa au uwezo, zikawa zinaingia hata dalili za rushwa kwamba kwa kuwa ni Rais ndiye anayeteua na kuletewa mapendekezo na watu wengi inawezekana mtu akaenda akamhonga kiongozi fulani ili apigiwe debe ateuliwe ama mtu ana jamaa yake anaona amsaidie anakwenda kumpigia debe akasema hapana"
Naafikiana na Warioba
  1. Hawa mawaziri wetu wanaiba fedha nyingi sana na hizo ndizo wanazitumia kutoa rushwa wakati wa uchaguzi
  2. Mawaziri waombe kazi kwa uwazi na wapigiwe kura na wananchi digitally kwa vitambulisho vya NIDA
  3. Makatibu wakuu nao waombe kazi na kupigiwa kura, kadhalika RCs DEDs na DCs wasiwepo vyeo vifutwe
Wote kwa ujumla wao waondolewe na wananchi kwa underperformance kwenye maeneo watakayotumikia
Mfumo wa sasa ni wa kubembelezana na kuleana sana
 
Ana mapendekezo gani sasa namna ya kuwapata mawaziri na viongozi wengine ngazi za uteuzi?
Siyo lazima yeye pekee ndo aje na suluhisho lote; hapo ni kutaka kufifisha hii hoja muhimu. Kama kawaida CHAWA huanza kuwasha taratiibu ili baadaye akunyonye damu. Wewe ni CHAWA unayetafuta pa kuanzia UCHAWA
 
Ana mapendekezo gani sasa namna ya kuwapata mawaziri na viongozi wengine ngazi za uteuzi?
Wenzetu Raisi anapendekeza majina , majina hayo nanapelekwa bungeni kwenye kamati Kamati inawaita au inamwta kwa mahojiano ya kweli. Ndipo kura inapigwa. Bunge linakuwa bunge kweli siyo mchongo. Kwa wakuu wa mashirika na taasisi nafasi zinatangazwa na bunge kazi yake ndiyo kuwahoji na kumtafuta mtu sahihi.
 
Naunga mkono HOJA,

Jimbo la bumburi halitamaniki, huwezi Amini Jimbo Hilo mbunge wake ni Waziri.
 
Back
Top Bottom