Jakaya Kikwete aongoza Vikao vya Bodi ya Taasisi ya GPE vinavyofanyika Jijini Paris

Jakaya Kikwete aongoza Vikao vya Bodi ya Taasisi ya GPE vinavyofanyika Jijini Paris

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Rais Mstaafu Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete, ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Kimataifa inayoshughulikia Masuala ya Elimu Duniani (Global Partnership for Education (GPE) ameongoza Vikao vya Bodi ya Taasisi hiyo vinavyofanyika Jijini Paris, nchini Ufaransa kuanzia tarehe 5 hadi 7 Disemba, 2022.

Vikao hivyo ni vya kwanza vya ana kwa ana tangu dunia ilivyokumbwa na ugonjwa wa COVID-19 mwishoni mwa mwaka 2019.

Katika vikao hivyo, Taasisi ya GPE inapitia na kuazimia masuala mbalimbali yatakayolenga kuboresha mifumo ya elimu katika nchi zinazoendelea ikiwemo kuongeza idadi ya wanafunzi wanaopata elimu, wakiwemo watoto wa kike, na matumizi ya teknolojia katika utoaji wa elimu.


IMG-20221206-WA0009.jpg
IMG-20221206-WA0011.jpg
IMG-20221206-WA0010.jpg
IMG-20221206-WA0015.jpg
 
Comasava,sava bien? Komanta levu? Je mapele Jhozee, Jhabite et Kilosa.

Swaye la bienevyu de morogoro.

Hongera sana JK.
 
Safi sana mutu makini mnooo. Piga kazi
 
Watoto wa jk wamekula bataa sana

Toka miaka 30 waziri.. mpaka miaka 70 bado baba ana vitengo vikubwa tu
 
Back
Top Bottom