Nyambala
JF-Expert Member
- Oct 10, 2007
- 4,465
- 1,171
Katika hotuba yake ya shukrani ambayo pia ilieleza mikakati ya serikali ya awamu ya nne katika kipindi kijacho cha miaka mitano, Rais Kikwete alisema kuwa atajenga makao makuu ya CCM ambayo yatakuwa ni ukumbi mkubwa utakaowawezesha kufanya vikao kwa usalama na utulivu.
Kwa sasa CCM inatumia majengo ya tawi la chama hicho mkoani Dodoma kuwa ofisi zake za makao makuu na hutumia ukumbi huomwa Kizota, ambao ulikuwa ghala la nafaka kufanyia mikutano yake mikuu.
Kikwete pia alisema kuwa katika kipindi hicho cha miaka mitano ijayo, atajenga Chuo Kikuu cha Kilimo cha Mwalimu Julius Nyerere mkoani Mara.
Awali, kabla ya Kikwete kupigiwa kura na Shein kuthibitishwa, ulisomomwa wasifu wa mgombea huyo na mwanasiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombare Mwiru alisoma mwelekeo wa sera.
Wakuu hivi hivi vyuo vikuu vinavyoahidiwa na JK ni mipango iliyofanyiwa utafiti au siasa. SUA inasua sua lakini tunaambiwa kuna chuo kikuu cha kilimo kingine kitajengwa. UDSM iko hoi mpaka wanaomba michango ya kupaka rangi majengo lakini JK anawaza chuo mpya.
Tukisema JK hajafanya lolote kwenye infrastructure tunaambiwa anaendeleza zile za awamu ya tatu......... Sasa mbona vyuo haendelezi kama ilivyokuwa imekusudiwa?????? Mbeya Tech ilikuwa ndiyo iwe chuo kikuu cha ufundi nchini lakini hiyo hapana kuendeleza I think kwa JK ni politically incorrect. Leo tunazungumzia Hikichuo kipya. Hivi huyu jamaa huwa anafikiri kabla ya maamuzi ya aina hii kweli?????