Nimejaribu kuangalia hii clip alipokutana na wachezaji Samatta na Ulimwengu nadhani ni Airport nimegundua JK alikuwa kiongozi mtia matumaini na sio mtishaji watu.
Hakuwa mtu wa kujimwambafai, mtishaji wengine kwa kauli zisizopiwa wala mwenye dharau.
Kukutana huku ghafla na vijana hawa kuna kitu +ve alipandikiza mioyoni mwao.
Natamani viongozi wengine wangemuiga hata katika hili tuu na kuachana na yale mengine aliyo fail.
Wengine wanaamini kwenye vitisho na mikwara mikwara
Hawamini kwenye taasisi wanazoziongoza wanaamini kwenye mimi.ndo mana wanasema wasipochaguliwa hiking au kile hakitafanyika!
Kwangu mimi ukinambia jitahidi jishughulishe kwa chochote maana usipomuwa na kipato ni ngumu kumudu hata gharama za mahitaji ya msingi kama chakula na usipofanya kazi hauli zote kwangu sawa maana mwisho wa siku zote zinanitaka kujishughulisha siwezi kumchukia mtu anaeniambia kujishughulisha