Jakaya Kikwete: Mikopo zaidi itachochea ukuaji wa Uchumi

Jakaya Kikwete: Mikopo zaidi itachochea ukuaji wa Uchumi

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dkt Jakaya Kikwete amesema utoaji mikopo zaidi kutoka taasisi za kifedha zikiwemo benki, utachochea uwekezaji na ukuaji wa uchumi kupitia sekta mbalimbali zikiwemo biashara na kilimo nchini.

Kikwete alisema uimara wa taasisi za fedha nchini kwa sasa utasaidia zaidi ukuaji wa uchumi kwa kuwa wawekezaji kwenye sekta za biashara na kilimo wanategemea zaidi taasisi hizo ili kufanikisha uendeshai. wa miradi yao.

Akizungumza kwenye hafla ya futari iliyondaliwa na Benki ya NBC kwa wateja wake mwishoni mwa wiki, Kikwete alieleza kuridhishwa na uimara wa taasisi za fedha nchini akitolea mfano benki hiyo inayomiliki mali zenye thamani ya Shi.52 trilioni na amana zenye thamani ya Shl.96 trilioni.

"Hakuna uchumi bila uwekezaji kama ambavyo hakuna uwekezaji bila mikopo ya uhakika kutoka taasisi za kifedha. Pamoja na taasisi nyingine za kifedha ninawasihi mwendelee kuwa karibu na wawekezaji kwa faida ya ukuaji wenu kama wakopeshaji, pia na kwa faida ya wawekezaji wenyewe, jamii pamoja na Serikali kwa ujumla," aliongeza Kikwete.
 
Mikopo inatolewa tatizo haiwasaidii walengwa, inaishia mikononi mwa wachache matokeo yake kundi kubwa la vijana linaendelea kuteseka, bahati mbaya zaidi hao wanufaika wachache hawairudishi ili wapewe wengine, na wala hawachukuliwi hatua zozote kisheria.
 
Mikopo inatolewa tatizo haiwasaidii walengwa, inaishia mikononi mwa wachache matokeo yake kundi kubwa la vijana linaendelea kuteseka, bahati mbaya zaidi hao wanufaika wachache hawairudishi ili wapewe wengine, na wala hawachukuliwi hatua zozote kisheria.
CCM ni tatizo kubwa ndani ya nchi hii.

Imejaa viongozi walafi wanaojali matumbo yao ndugu,na jamaa zao.

Mikopo inayochukuliwa ingekuwa inakwenda kwenye miradi lengwa kwa asilimia mia tungekuwa mbali sana.

Lakini mafisadi yaliyojaa serikalini yanatafuna pesa za nchi na kufanya miradi mingi iende kwa kusuasua.

Hii nchi kupata maendeleo chini ya utawala wa CCM ni zaidi ya ndoto.
 
Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dkt Jakaya Kikwete amesema utoaji mikopo zaidi kutoka taasisi za kifedha zikiwemo benki, utachochea uwekezaji na ukuaji wa uchumi kupitia sekta mbalimbali zikiwemo biashara na kilimo nchini.

Kikwete alisema uimara wa taasisi za fedha nchini kwa sasa utasaidia zaidi ukuaji wa uchumi kwa kuwa wawekezaji kwenye sekta za biashara na kilimo wanategemea zaidi taasisi hizo ili kufanikisha uendeshai. wa miradi yao.

Akizungumza kwenye hafla ya futari iliyondaliwa na Benki ya NBC kwa wateja wake mwishoni mwa wiki, Kikwete alieleza kuridhishwa na uimara wa taasisi za fedha nchini akitolea mfano benki hiyo inayomiliki mali zenye thamani ya Shi.52 trilioni na amana zenye thamani ya Shl.96 trilioni.

"Hakuna uchumi bila uwekezaji kama ambavyo hakuna uwekezaji bila mikopo ya uhakika kutoka taasisi za kifedha. Pamoja na taasisi nyingine za kifedha ninawasihi mwendelee kuwa karibu na wawekezaji kwa faida ya ukuaji wenu kama wakopeshaji, pia na kwa faida ya wawekezaji wenyewe, jamii pamoja na Serikali kwa ujumla," aliongeza Kikwete.
Wanakopa halafu wanazipiga, kama zile za covid 19
 
Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dkt Jakaya Kikwete amesema utoaji mikopo zaidi kutoka taasisi za kifedha zikiwemo benki, utachochea uwekezaji na ukuaji wa uchumi kupitia sekta mbalimbali zikiwemo biashara na kilimo nchini.

Kikwete alisema uimara wa taasisi za fedha nchini kwa sasa utasaidia zaidi ukuaji wa uchumi kwa kuwa wawekezaji kwenye sekta za biashara na kilimo wanategemea zaidi taasisi hizo ili kufanikisha uendeshai. wa miradi yao.

Akizungumza kwenye hafla ya futari iliyondaliwa na Benki ya NBC kwa wateja wake mwishoni mwa wiki, Kikwete alieleza kuridhishwa na uimara wa taasisi za fedha nchini akitolea mfano benki hiyo inayomiliki mali zenye thamani ya Shi.52 trilioni na amana zenye thamani ya Shl.96 trilioni.

"Hakuna uchumi bila uwekezaji kama ambavyo hakuna uwekezaji bila mikopo ya uhakika kutoka taasisi za kifedha. Pamoja na taasisi nyingine za kifedha ninawasihi mwendelee kuwa karibu na wawekezaji kwa faida ya ukuaji wenu kama wakopeshaji, pia na kwa faida ya wawekezaji wenyewe, jamii pamoja na Serikali kwa ujumla," aliongeza Kikwete.
Ukiangalia kwa jirani zetu ambako serikali liyopita ilikopa sana na ya sasa hata uwezo wa kulipa mishahara watumishi wake inasuasua, ukizingatia ufisadi uliovuka mipaka uliopo nchini,........tuna mifumo imara ya kuhakikisha mikopo hiyo inafanya kazi iliyokusudiwa? ikiwa pesa za ugonjwa (uviko) watu wamezitafuna?
 
Kweli kabisa Mikopo inachochea Uchumi wa nchi, that’s pure fact but not in this Country, ikitolewa tu wajanja wachache ndiyo wanafaidika nawanalindwa yaani hata ikijurikana Pesa zimeliwa hawagusiki.
 
Yaani ukishasikia "vijana changamkieni fursa" mjue tayari filimbi ishapigwa, hapo ndio unaanza kuona hizooo sarakasi huko kwenye makorido, 'wee' halafu kakitoka kale ka-gazette tu ujue tayari ishapigwa sehemu kilaini, yani ikifikia muda taarifa inapofika kwa waandishi wa Habari na maelezo lukuki, ujue tayari ishapigwa maradufu, ukiiona taarifa kwenye vyombo vya habari, watu wanakula vacation, ishatoka hio na majeruhi wanahesabiwa... Sie walalahoi twaja ambiwa waliokopa hawajulikani, hakuna atakayelipa kati ya waliochukua "mikopo" "fursa" halafu linatokea bonge la taarifa la tawkimu. za uchumi kuwa...'kila mtanzania ana deni' la kiasi hiki na kile na hichi.....kwanini nisichoke!

Tutafika...2025 siyo mbali wakuu.

J.M.K yupo sahihi kabisa, hususani kwa Watanzania tunaoingia kwenye uchumi huu wa kibepari.
 
^NHIF fedha zake hazikufanya kazi iliyokusudiwa, bali watumishi walikopeshana kwa ajili ya shughuli zao binafsi.^ CAG.
 
Mikopo inatolewa tatizo haiwasaidii walengwa, inaishia mikononi mwa wachache matokeo yake kundi kubwa la vijana linaendelea kuteseka, bahati mbaya zaidi hao wanufaika wachache hawairudishi ili wapewe wengine, na wala hawachukuliwi hatua zozote kisheria.
Unazungumzia commercial loan au kitu gani ..?

Au zile za halmashauri ..??
 
JK na Uchumi wapi na wapi banaaa !!.

Mtu mwenyewe alipata GPA kiduchuuuuu Tena ya Sanaa yaan Sanaa yenyewe ya Siasa na Mahusiano lkn bado akapata GPA kiduchuuuuu .
Kuna elimu ya darasani na ya mtaani.
Katika maisha baada ya shule, ya darasani hutumika less than 5% na ya mtaani above 95%.
 
Mikopo inatolewa tatizo haiwasaidii walengwa, inaishia mikononi mwa wachache matokeo yake kundi kubwa la vijana linaendelea kuteseka, bahati mbaya zaidi hao wanufaika wachache hawairudishi ili wapewe wengine, na wala hawachukuliwi hatua zozote kisheria.
Vijana hawafuati hiyo mikopo,Wacha kuwa na mode ya ulalamishi kila dakika,nipo nao nimeawa-organise wapate mkopo,wanazunguka tu hawajui kwenye vikao
 
Mikopo inatolewa tatizo haiwasaidii walengwa, inaishia mikononi mwa wachache matokeo yake kundi kubwa la vijana linaendelea kuteseka, bahati mbaya zaidi hao wanufaika wachache hawairudishi ili wapewe wengine, na wala hawachukuliwi hatua zozote kisheria.

Yeye mwenyewe alitoa mikopo ya billioni 20 kila mkoa Wakati wa utawala wake ; zilisaidia nini zaidi ya kuwa hongo kwa vijana ili waipigie debe ccm!! Ile benki amabyo Samia amekwenda kuikopea fedha ADB ili isaidie wakulima , Bashe amefanya ndio kichaka chake cha hujuma na sasa wameanza kuchoma nyaraka ili kuficha ushahidi wa wizi wanaoufanya pale!!! Huyo Mkuu wa benki hiyo TADB wamemtoa Lake oil; sasa tafuteni mjue operations za owners wa hiyo Lake oil hapo ndio mtajua kama huyo mkurugenzi Mkuu wa TADB ana hadhi ya kulinda hicho kihenge!!
 
Hivi kwa nini huyu fisadi asikae kimya tu kuliko kuendelea kutuchefua na maneno yasiyokuwa na tija kwa ustawi wa taifa letu? Yeye ameshastaafu, he should shut up.
 
JK na Uchumi wapi na wapi banaaa !!.

Mtu mwenyewe alipata GPA kiduchuuuuu Tena ya Sanaa yaan Sanaa yenyewe ya Siasa na Mahusiano lkn bado akapata GPA kiduchuuuuu .
Yaani wewe ndo boya kwel , Bado unakariri kua GPA Zina positive effects kwenye maendeleo ya nchi yetu , Bongo kua na GPA kubwa ni kuonyesha uwezo mkubwa wa kukariri tu sio kuchanganua mambo , Kwa sababu wasomi wa bongo wengi hawana msaada wowote kwenye jamii , wenyewe tu hawawezi kujisimamia kwenye mambo yao zaidi ya kuhangaika na vibahasha , acha ujinga

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom