Jakaya Mrisho Kikwete, Raisi Mstaafu aliyejaaliwa hekima nyingi

MIXOLOGIST

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2016
Posts
14,311
Reaction score
36,056
Wasalamu wana JF,

Wakati tukimaliza matanga ya bibi yetu Elizabeth, nimetafakari sana mienendo ya viongozi wetu hapa Tanzania. Hakika, Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na madhaifu yake ni mtu mwenye hekima nyingi.

Huyu mzee alitufumbua kuhusu kuchanganya akili za kuambiwa na za kwetu. Hali kadhalika alituasa tunapoenda sehemu kwa minajili ya kuwa viongozi basi tusirithi maadui wa watangulizi wetu.

Hekima ya huyu mzee iko praticlal na mengi aliyo yasema au anayo yasema yana mafunzo makubwa, japo wengi wetu tunamchukulia poa. Kwangu mimi video hii hapa chini ni moja ya maneno yake yanayonitafakarisha sana.
Your browser is not able to display this video.

"Siyo kwamba sisikii, wala siyo kwamba siambiwi yanayosemwa, au sijui kusema, au sina la kusema, la hasha! Sijafanya hivyo kwasababu sioni faida yake."

Tuendelee kumuenzi mzee wetu huyu, na Mungu amjaalie maisha marefu.
 
Ni kweli, mbali na madhaifu aliyonayo kama mwanadamu, amejaliwa hekima. Lakini nadhani exposure aliyonayo imejenga sana.
 
Hii ni kipindi alipohutubia bunge,na hapa alikuwa anajibu vitisho vya kagame,kagame alitoa povu,aliposhauliwa akutane na wapinzani wake wa vita,hizi busara zake laiti angezitumia vzr tungepata faida,charity begins at home,tatizo mfumo ccm wa wizi umemnufaisha yeye na familia yake,kwanza atuambie gesi yetu iliishia wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…