Jamaa akutwa na n.domu ikiwa na mchuzi. Mkewe anataka kuondoka!

Jamaa akutwa na n.domu ikiwa na mchuzi. Mkewe anataka kuondoka!

mwambhe amsamehe tu mmewe kwanza anajali sana,pili amekiri kosa na kuomba msamaha,tatu ndo kwanza wanainza safari ya ndoa,huo ni upepo utapita tu.bado kuna mengi na makubwa sana atakutana nayo anapaswa kuwa mvumilivu.

Nakubaliana sana na wewe. inawezekana ni mara yake ya kwanza au kazoea lakini kwa sababu ameomba msamaha na aibu iliyompata na ushahidi usio na mashaka inawezekana kabisa ikawa adhabu tosha ya kumfanya ajirekebishe. Pia aendelee kumwombea mume wake Mungu anaweza kumbadilisha na kuwa mume mwema sana. Kwani nani ajuaye kwamba akimwacha huyo na kuolewa na mwingine atakuwa mwaminifu kwake. Asikate tamaa kwa Mungu yote yanawezekana.
 
Si unaona mambo hayo? Ukimwagiwa euro kadhaa ? mezani, gari inaletwa mpya, jamaa anabadilisha furniture zote hadi vitanda, unapelekwa serengeti kwa wiki unalala Sopa lodge unadhani utakumbuka tena we purple wewe?

dah!anipeleke na shoping dubai or france,hoja yake ya msamaha itakua imepita kwa kweli..teh teh
 
Bond post umefanya vema msaidie huyo mama ili ndoa hiyo ipone. Ila huyo rafiki yako msaidie pia ili aelewe umuhimu na uzito wa ndoa. kama hawezi kabisa kuacha pombe basi anywe kiasi kinachombakizia akili za kujitambua na kujiheshimu. Yeye ndio anatafuta pesa sio pesa zinamtafuta. Viwanda vya pombe bado vipo tu na vitaendelea kuwepo hivyo hawezi kuikomoa pombe. Ona sasa aibu iliyompata atamwangaliaje mkewe, ndugu zake, wazazi wake, washikaji zake na wale anaowaheshimu? Mwambie aokoke aachane na mapepo hayo yatampeleka bapaya.:flypig::israel:
 
Bond post umefanya vema msaidie huyo mama ili ndoa hiyo ipone. Ila huyo rafiki yako msaidie pia ili aelewe umuhimu na uzito wa ndoa. kama hawezi kabisa kuacha pombe basi anywe kiasi kinachombakizia akili za kujitambua na kujiheshimu. Yeye ndio anatafuta pesa sio pesa zinamtafuta. Viwanda vya pombe bado vipo tu na vitaendelea kuwepo hivyo hawezi kuikomoa pombe. Ona sasa aibu iliyompata atamwangaliaje mkewe, ndugu zake, wazazi wake, washikaji zake na wale anaowaheshimu? Mwambie aokoke aachane na mapepo hayo yatampeleka bapaya.:flypig::israel:

Ndossy, kwanza nashukuru kwa mchango wako, mie nipo kwenye taasisi ya ndoa kwa muda kidogo, hakika nimeshuhudia kipindi cha miaka mitano hadi saba ndoa huwa kwenye majaribu makubwa na vijana wengi hawaelewi kuwa huo ndio wakati wa mpito na kushikana zaidi. Wengi hudhani furaha haitapatikana hapo baadae, na kuishia kufarakana hadi kuachana.
Majaribu kwenye ndoa yapo, tena mengi sana, ndo maana ni vizuri kuwa na moyo wa kiutu uzima unapoingia kwenye ndoa.
Nimepata wasaa wa kukaa na jamaa yangu kwani ni dhahiri anajutia yaliyomkuta ila ndo yashatokea, mke anaujauzito unaomfanya kila akimuona mumewe anamtukana na amemuhama chumba, hapati unyumba tena, nadhani hiyo imechangia yeye kuingia mtegoni mwa yule mzambia, pombe huwa haimfanyi arukwe na akili, nina imani walipoamua kukaa na kunywa pamoja walikuwa wanatamaniana tu sema walitafuta DUTCH COURAGE! Kuokoka labda tumuombee kwa mungu ila siwezi kumshauri zaidi ya kuwa nimemsaidia kumfichia fedheha kwa kumchukua mkewe akae kwangu ili ionekane kuwa mke wangu anamsaidia coz ni mjamzito. Time will heal their marriage.
 
Nakubaliana sana na wewe. inawezekana ni mara yake ya kwanza au kazoea lakini kwa sababu ameomba msamaha na aibu iliyompata na ushahidi usio na mashaka inawezekana kabisa ikawa adhabu tosha ya kumfanya ajirekebishe. Pia aendelee kumwombea mume wake Mungu anaweza kumbadilisha na kuwa mume mwema sana. Kwani nani ajuaye kwamba akimwacha huyo na kuolewa na mwingine atakuwa mwaminifu kwake. Asikate tamaa kwa Mungu yote yanawezekana.

Its true, waweza ruka mkojo ukakanyaga mavi.
 
Imekuwa alfajiri, simu yangu inaita, naipokea na kusikia sauti ya kike, anajitambulisha kuwa ni mke wa rafiki yangu. Nahamaki kwa kudhani jamaa amepatwa na ajali au vipi kwani nae ni mlevi kwa muda sasa.

Shemeji ananiita nyumbani kwao, nafika nakuta mke analia na bwana amelala fofofo, nauliza kama rafiki yangu anaumwa au vipi shemeji ananiambia kalala ila nikae anisimulie ndipo tumuamshe mshkaji. Naamua kukaa nipate kuelewa kwa nini yule bwana kalala usingizi wa pono huku mkewe akilia alfajiri yote ile.
Mwanamke anasema jamaa amerudi kalewa, mke akamsaidia kushuka kwenye gari mpaka ndani, lakini alipofika sebuleni jamaa akawa mzito so mke akaamua amlaze kwenye kochi, sasa akamvua shati na akawa anamvua suruali ndipo akakutana na kituko cha mwaka.

Jamaa ameivaa ndomu na mchuzi upo ndani, mkewe kaishiwa nguvu, anataka kuondoka ila ndio ana mimba na hana kazi kwani ndo amemaliza masomo ya chuo kikuu anataka akijifungua ndo awe busy kusaka kazi, mjini ana ndugu mmoja ambaye hawaivi.

Nikaamua kumuamsha jamaa na kumuuliza kilichotokea, jamaa hana la kufanya kukataa hawezi ila kabaki kuomba msamaha. Naye tulipokuwa wawili nikamuuliza kwa nini kafanya hivyo? Naye anachokumbuka alikuwa kwa party ya ofisi, kuna mwanamke mzambia ni bosi wake walipiga ma-cocktail ya kumwaga wakaishia kuji-do kwenye gari. Kilichoendelea hakumbuki.

Mkewe kaomba kukaa kwangu japo apate muda wa kufikiria zaidi, nimeongea na wife wangu amekubali ili tuisevu ndoa yao. Mke wa jamaa anaingia jioni ya leo. Wandugu mnadhani kwa hili tulilofanya tupo sawa?

Mkuu, umenikumbusha mbali, zile fiction za James Hadley Chase.
 
Imekuwa alfajiri, simu yangu inaita, naipokea na kusikia sauti ya kike, anajitambulisha kuwa ni mke wa rafiki yangu. Nahamaki kwa kudhani jamaa amepatwa na ajali au vipi kwani nae ni mlevi kwa muda sasa.

Shemeji ananiita nyumbani kwao, nafika nakuta mke analia na bwana amelala fofofo, nauliza kama rafiki yangu anaumwa au vipi shemeji ananiambia kalala ila nikae anisimulie ndipo tumuamshe mshkaji. Naamua kukaa nipate kuelewa kwa nini yule bwana kalala usingizi wa pono huku mkewe akilia alfajiri yote ile.
Mwanamke anasema jamaa amerudi kalewa, mke akamsaidia kushuka kwenye gari mpaka ndani, lakini alipofika sebuleni jamaa akawa mzito so mke akaamua amlaze kwenye kochi, sasa akamvua shati na akawa anamvua suruali ndipo akakutana na kituko cha mwaka.

Jamaa ameivaa ndomu na mchuzi upo ndani, mkewe kaishiwa nguvu, anataka kuondoka ila ndio ana mimba na hana kazi kwani ndo amemaliza masomo ya chuo kikuu anataka akijifungua ndo awe busy kusaka kazi, mjini ana ndugu mmoja ambaye hawaivi.

Nikaamua kumuamsha jamaa na kumuuliza kilichotokea, jamaa hana la kufanya kukataa hawezi ila kabaki kuomba msamaha. Naye tulipokuwa wawili nikamuuliza kwa nini kafanya hivyo? Naye anachokumbuka alikuwa kwa party ya ofisi, kuna mwanamke mzambia ni bosi wake walipiga ma-cocktail ya kumwaga wakaishia kuji-do kwenye gari. Kilichoendelea hakumbuki.

Mkewe kaomba kukaa kwangu japo apate muda wa kufikiria zaidi, nimeongea na wife wangu amekubali ili tuisevu ndoa yao. Mke wa jamaa anaingia jioni ya leo. Wandugu mnadhani kwa hili tulilofanya tupo sawa?

Mtu gani anavulia nguo sebuleni acha kuturusha na uongo wako'
 
hivi tujaribu kugeuza story mwanaume ukikuta kitu kama hiko kwa mkeo ungemsamehe?
 
Huyo jamaa ni mwangalifu sana pamoja na kupombeka hivyo! Safi sana. Mke ashukuru kupata Mume mwangalifu.
 
sasa nyie msioolewa si ndo mtakua wezi wa waume za watu?

Angel msoffe, hao wasioolewa wanajiitaga 'single moms' honestly wao ndo kazi yao kuwarubuni waume za watu. Ona huyo mwanamke aliyelala na mshkaji nae ni single mom, yeye ni mtu wa outing kaishia kulala na mshkaji kwenye gari na ni bosi eti. Kweli nawaambieni adui ya mwanamke ni mwanamke mwenzie, hapo ukute kasema ' ah kwanza mkeo sa hv ananuka maziwa mshamba yule'. Mwanaume ni kiumbe dhaifu sana when it comes to sex tena ukichukulia mkewe ni mjamzito na anamnyima unyumba jamaa mimba yake ndo inavyomtuma. Kweli hawa masingle ladies wanaharibu ndoa za wanawake wenzao walioamua kutulia katika ndoa.
 
Mkuu, umenikumbusha mbali, zile fiction za James Hadley Chase.

Ha ha ha! James Hardley, ndugu yangu siwezi kumfikia yule nguli wa uandishi hata siku moja! Nway thanks for your appreciation.
 
Mtu gani anavulia nguo sebuleni acha kuturusha na uongo wako'

Shine, umeisoma story vizuri? Hawana mtoto, mke ndio anaujauzito, jamaa karudi amelewa hajiwezi, mke kamsaidia kuingia ndani amena kalewa, ameshindwa kumbeba akaamua amlaze sebuleni at least yupo ndani. Hujaelewa bado ndugu?
 
hivi tujaribu kugeuza story mwanaume ukikuta kitu kama hiko kwa mkeo ungemsamehe?

Inadepend na mtu, pia kosa likoje, binafsi nitataka kujua kwa nini kafanya vile. Is it about money, love, satisfaction au ndo alivyo! Hayo ni maswali ya msingi sana.
 
dah!!!!
Kuna ndoa zina majaribu....

Bora umejisemea wewe, hayo ni majaribu, ni sawa leo umejenga gorofa halafu nakuta limeungua na moto, watoto wamekufa, mali zote zimeungua, unafanyaje? Unajiua? Nope i guess not, there is life still, just have faith and keep on living coz u never know what tomorrow holds for your life.
 
Back
Top Bottom