Jamaa aliyeniibia kuku mwaka jana leo amefariki, mtaa unahisi nimemroga

Itakuwa nafsi yako nyingine imemuadhibu. Wengine huwa wana nguvu. Kidini wanasema malaika mlinzi wako. So your guardian angel amefanya yake kulipa kisasi baada ya wewe kusema unamwachia Mungu. Usipoangalia hata huyo mama aliyenunua kuku anaenda kupigwa
 
Usijali, kilicholipiza kisasi ni walinzi wako. Hawawezi kukubali uguswe. Wana nguvu sana. Trust me
 
Ntume Muhammad (SAW) anasema , watu watatu Dua zao hazirejeshwi ( zinakubaliwa moja kwa moja) . Wa kwanza Kiongozi muadilifu , wa pili Aliyefunga mpaka afuruturu na Maangamizo ya aliyezulumiwa .Sasa hapo ndo pamemuondosha uyo jamaa .
 
Mkuu hilo tayari limeshakujengea heshima mtaani.
Hata ukiacha hela nje ya nyumba hakuna atakayezigusa.
Kwa kuwa hukumdhuru kwa lo lote endelea na maisha yako.
 
Nipatie namba ya mganga wako tafadhali
 
Ulishamuachia Mungu.Mungu ndie anaejua kama anatekeleza ulichomuachia au anatimiza wajibu wake.
Ila mwizi siyo kumuonea huruma
 
Mambo ya kwa msisi, handeni, Tanga
 
Acha woga hakuna mtu atakudhuru.
Huwezi kuzuia hisia na maneno ya watu.
 
Kwamba hta wake zake walishindwa kuja kumsaidia
 
Hapo ndo vizuri unatakiwa uvimbe ili wajinga wajinga waache kukuzoea kitaani, watakuwa wanakuita MZEE WA BUSARA 😹

Na msibani usiende achana nao waache wazike mwizi wao..!!!
Hapo wewe fungua kilinge upige pesa za wajinga sasa.!! Chuma majani ya muarobaini yakaushe kazi ianze, si umesema msikitini huwa unaenda enda so kiarabu unakijua cha kunywea maji?? 😹

Wapandishie majini ya uongo na kweli, watume wakuletee kuku ukazie zile zilizoibiwa..!!
 
Shusha na huyo mnunuzi wa mali za wizi udongoni.

Madalali na wanunuzi wa mali za wizi ndo chanzo cha uhalifu mwingi mtaani
 
Kama ni mwizi basi kuna mtaalam mmoja aliiba kwake akaamua amle kichwa.
Kama hujahusika huna haja ya kuwaza. Kama una mawazo sana, Hama huo mtaa uwe huru. Usije kufa kwa stress
 
Binadamu wakikuchoka ni hatari, jamaa wa shimoni akakosa msaada
 
Hakuanga kisasi katika shikri kinachofanya kazi kama wewe hujahusika mkuu! Nilichokiona kwako ni hofu kuwa vipi kama ndugu wa familia wakiamua kukufanyia na wewe shirki kama malipizi.

Laana isiyo na sababu haimpati mtu! ... Kuwa na amani ... Kuwa mtu wa ibada! Unawezaje kuwa unamtegemea Mungu na kumwabudu then uogopa wachawi? This mean Mungu wako unamuona Hana nguvu na huamini kuwa anaweza kukulinda dhidi ya ushirikina.

Usirihusu hofu kukutawala maana hofu ndio mlango mkubwa sana ambao adui anaweza kuutumia kukumaliza.

Kile walichohofia na kukiogopa ndicho kilichowapata ... Siku zote hofu Ina adhabu.

Usikubali hofu
 
Hii Kuna jamaa alisota mahabusu Kwa miaka 3,yeye alienda kutishia bibi kizee mchawi wa mtaani kuwa atampiga mapanga akiendelea kumroga,,,issue ya vitisho vya jamaa ilienda viral mtaani sasa Kuna miamba ambayo ilisharogwa kitambo na huyo bibi ikatumia fursa ya vitisho vya jamaa kumaliza kazi Kwa kumkata kata panga bibi kizee,,, suspect wa kwanza aliye toa vitisho na alisota mahabusu miaka Hadi kutoka,,,hata wewe kinachokugharimu ni vitisho vyako Kwa huyo marehemu mwizi.

Cha kufanya jikinge vizuri maana next move ni kurogwa pia na ndugu za marehemu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…