Thread nyingine bwana! Hivi jamaa na yeye akianzisha thread akisema ana jamaa yake akataja kabila mfano mhehe halafu akaingia woga kuwa huyo rafiki yake anaweza kumlisha mbwa!
Au mchaga akasema kuwa anaweza kumchori, au mhaya akasema anaweza kum............. au akasema tu anaweza kumwambukiza DNA za kibongo za kimajungumajungu kama za mleta thread!
Nashindwa kujua mantiki ya hii thread ila mleta thread akumbuke wasomali hawakutaka wawe pirates!!!! wanasiasa ndio waliowafikisha walipo leo hii na hakuna mtu anaetaka kuwa mbaya duniani lazima kuwe na chanzo cha yeye kubadilika na kuwa mbaya. Hapa Tanzania tunao wasomali wengi na wanaheshimika mfano mmiliki wa hotel ya paradise na tansoma mzee guledi, yupo transporter anaitwa Hassan Transporter kuna mwansiasa anaitwa Aden Rage kuna mama mmoja msomi anaitwa somebody warsame. Na hapa kwetu unapotoka wewe mheshimiwa mleta mada kuna watu wa ajabu ajabu mnawajua! tunao kuanzia kaya mpaka kitaifa. Tuna mafisadi, tuna wazinifu, tuna majambazi, tuna wauza ngozi za binaadamu, tuna wauwaza viungo vya albino...............