Jamaa yuko Rumande kwa kosa gani?

Jamaa yuko Rumande kwa kosa gani?

Mkulima

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2007
Posts
1,236
Reaction score
1,546
Mbona jamaa kasema ukweli mtupu? Anafanya nini rumande?

Na Mwandishi wetu (Nipashe)



2nd September 2009
Raia wa Iraq, Anney Anney, anayedaiwa kuwakashifu viongozi, amepelekwa rumande baada ya kesi ya kuwakashifu marais wa awamu ya pili na tatu kuahirishwa tena Septemba 7 mwaka huu kutokana na upande wa mashtaka kudai upelelezi bado haujakamilika.
Kesi hiyo iliahirishwa jana na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, Samuel Maweda
Baada ya kesi hiyo kuahirisha, mshtakiwa huyo mwenye ulemavu wa mguu, aliiomba mahakama hiyo kumruhusu ajidhamini kwa madai kuwa tangu apelekwe gerezani amekosa mawasiliano na ndugu zake wanaotakiwa kufika kumwekea dhamana.
Mshtakiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo Julai 27, mwaka huu na kusomewa mashtaka ya kutoa maneno ya uchochezi na kuwakashifu marasi hao kwa kuendesha nchi kwa maslahi yao binafsi.
Inadaiwa kuwa Julai 23, mwaka huu, majira ya mchana katika eneo la Ikulu jijini Dar es Salaam, mshtakiwa huyo alitoa maneno ya uchochezi kuwa Rais wa Awamu ya Pili, Hassan Mwinyi aliua Azimio la Arusha na wa tatu Benjamin Mkapa mashirika ya umma na ardhi kwa wazungu na waarabu na utu wa utaifa wa Watanzania .
Mshtakiwa huyo pia anadaiwa kuwa baada ya kutamka maneno hayo alisema udumu ujamaa na kujitegemea , lidumu Azimio la Arusha na zidumu fikra za Mwalimu Nyerere.
Mshtakiwa huyo alikana shaka hilo na kupelekwa rumande baada ya mahakama hiyo kukataa ombi la kujidhamini kwa kukosa wadhamini.
 
Alitoa maoni yake kama raia,alichokosea ni kuingia maeneo ya ikulu hiyo ni kama kutangaza vita na jamhuri.Angesemea mahali pengine kama vyombo vya habari............aliamua kuifanya ikulu kwa babu yake sasa mwache asote kidogo ajue ikulu ni mahali patakatifu...
Mbona jamaa kasema ukweli mtupu? Anafanya nini rumande?
 
bora wamweke huko apumzike ameacha kuongelea matatizo ya kwao huko aje aongelee ya kwetu
 
Huyo keli raia wa Iraq au ni Mtanzania mwenye asili a Iraq.

Vp raia wa Iraq asifie Azimio la Arusha na Fikra za Nyerere badala ya kusifia Fikra za Saddam?
 
Huyu jamaa sio raia wa Iraq ni mtanzania wa kabila la Iraqw toka kule Arusha.Waandishi wetu ni vigumu kufuatilia masuala ya kihabari wanakurupuka kuuza habari kwa kugeuza iwe ni mtu wa Iraq.
 
Kilichokashifiwa ni kipi?

Kwani si kweli kwamba Azimio la Zanzibar liliuwa Azimio la Arusha?

Kwani kuna dhambi gani kuuwa sera iliyoshindwa na kujaribu nyingine?
 
Anney Anne sio raia wa Iraq bali ni Mwiraqw wa Endabash, Wilaya ya Karatu. Kesi yake ilipotajwa ilielezwa kuwa ni mkazi wa Mtaa wa Kilombero, Manispaa ya Arusha. Mwandishi alipotosha alipooandika ni raia wa Iraq.
 
Mkulima, kama unafuatilia magazeti madai ya kosa la Anney haya hapa:

Mlemavu kortini kwa kumkashifu Kikwete



na Datus Bornface




MLEMAVU wa miguu, Anney Anney (50), mkazi wa Arusha Kilombelo, jana alipandishwa katika Mahakama ya Wilaya Ilala, jijini Dar es Salaam, akituhumiwa kumkashifu Rais Jakaya Kitwete.

Mwendesha Mashitaka, Mrakibu wa Polisi Niama Mwanga, alidai mbele ya Hakimu Samwel Maweda kuwa, mtuhumiwa alitenda kosa hilo Julai 23, mwaka huu, eneo la Ikulu jijini Dar es Salaam.

Alidai kuwa, siku ya tukio akiwa kwenye maeneo hayo ya Ikulu, mtuhumiwa alitoa ujumbe kupitia bango aliloliandaa ambao ungehatarisha uvunjifu wa amani kwa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwanga alidai kuwa, mtuhumiwa alitoa ujumbe wenye maneno ‘Jakaya Kikwete, Ikulu ya Dar es Salaam, Nyerere alilinda ardhi yetu pia utu na uzalendo’.

Alidai kwamba, maneno mengine ni ‘Mwinyi aliua Azimio la Arusha, Mkapa aliuza mashirika yetu na nyumba za umma, wewe (Kitwete), unauza ardhi yetu kwa Wazungu na Waarabu pamoja na utu na utaifa wetu’.

Aliendelea kudai kuwa, ujumbe huo pia ulisomeka kama, ‘Udumu ujamaa na kujitegemea, lidumu Azimio la Arusha, zidumu fikra za Mwalimu Nyerere’.

Mtuhumiwa alikana shitaka hilo na kurudishwa rumande kwa kushindwa kukidhi mahitaji ya dhamana kwani alitakiwa kuwa na wadhamini wawili.

Kesi hiyo ya aina yake, imeahirishwa hadi Agosti 10 na upelelezi bado haujakamilika.

Wakati huo huo, mfanyakazi wa ndani, Idd Hassan (19), mkazi wa Buguruni, jijini Dar es Salaam, jana alipandishwa kizimbani, akituhumiwa kwa kosa la kubaka mtoto mwenye umri wa miaka miwili (jina limeahifadhiwa).

Mwendesha Mashitaka, Inspekta wa Polisi Hamis Mhellya, alidai mbele ya Hakimu wa Wilaya, Afumwisye Kibona kwamba mtuhumiwa alitenda kosa hilo Julai 20, mwaka huu, eneo la Buguruni Malapa.
 
Hiyo siasa tu. Jamaa katoa mawazo yake hivyo sioni ulazima wa kumweka rumande. Rumande zetu zinaweka mpaka wezi wa kuku. Si shangai hata hili nalo. Je angewakashifu ingekuwaje?
 
Wanaotakiwa kwenda rumande ni wakina Rostam Aziz na genge lake na sio huyu mlemavu wa Mungu!! Hivi hapa nchini haKuna wanasheria wa haki za binadamu ambao wangejitokeza kumuwekea dhamana huyu mpambanaji anaeipenda nchi yake kiasi cha kwenda na kusema maneno ya kweli ambayo yanaowahusu na kuwagusa wanaita uchochezi? Wazungu wanamsemo; YOUR TERRORIST IS MY FREEDOM FIGHTER. HUYU JAMAA NI MPAMBANAJI NA WALA SI MCHOCHEZI KUNA UMUHIMU WA KUMPIGANIA ATOKE HUKO SELO.
 
jamaa yuko sahihi kabisa nimependa maoni yake .kwani uongo!?
 
Sijaona tatizo alilofanya huyo jamaa mpaka atiwe ndani. Alichoongea ni ukweli mtupu na ametumia haki yake kikatiba kama mtanzania kudumisha demokrasia. Niko tayari kumchangia pesa ya dhamana kama inatakiwa.
 
Back
Top Bottom