Mwabhleja
JF-Expert Member
- Jan 27, 2016
- 1,351
- 2,061
Ndugu,
Kama utakuwa mfuatiliaji wa mpira wa miguu nchini basi si ajabu kwamba katika kichwa chako utakuwa unamkumbuka vema ombwe la uongozi lililofinyanga utendaji wa shirikisho la soka nchini (TFF) tangu Jamal Malinzi madarakani.
Pamoja na mambo mengine, juzi juzi kulikuwa na kashfa ya upangwaji matokeo kwa ligi kuu daraja la kwanza ambapo baadhi ya timu ikiwemo Geita Gold Sports Club kupokonywa ushindi na kushushwa daraja licha ya ushahidi kutokuwa yakinifu ambapo haingii akilini kumfungia mchezaji na kocha msaidizi kwa kudai wamehusika kupanga matokeo pasi na uongozi mzima kuwajibishwa.
Kifupi, utagundua maamuzi ya TFF yalifanyika kwa mhemko uliochagizwa sana na baadhi ya watangazaji wa Cloudz lakini hakuna uchunguzi wa kina uliofanyika.
Pamoja na hayo, ulitolewa muda wa timu zilizoadhibiwa kukata rufaa lakini kabla ya hearing ya rufani, TFF ya Jamal Malinzi imepanga timu kibonde ya Mbao FC ambayo hata kuwasafirisha wachezaji 15 kutoka Mwanza kwenda Geita ilikuwa inapata tabu.
Swali; Rufani Zimepuuzwa?
Kama utakuwa mfuatiliaji wa mpira wa miguu nchini basi si ajabu kwamba katika kichwa chako utakuwa unamkumbuka vema ombwe la uongozi lililofinyanga utendaji wa shirikisho la soka nchini (TFF) tangu Jamal Malinzi madarakani.
Pamoja na mambo mengine, juzi juzi kulikuwa na kashfa ya upangwaji matokeo kwa ligi kuu daraja la kwanza ambapo baadhi ya timu ikiwemo Geita Gold Sports Club kupokonywa ushindi na kushushwa daraja licha ya ushahidi kutokuwa yakinifu ambapo haingii akilini kumfungia mchezaji na kocha msaidizi kwa kudai wamehusika kupanga matokeo pasi na uongozi mzima kuwajibishwa.
Kifupi, utagundua maamuzi ya TFF yalifanyika kwa mhemko uliochagizwa sana na baadhi ya watangazaji wa Cloudz lakini hakuna uchunguzi wa kina uliofanyika.
Pamoja na hayo, ulitolewa muda wa timu zilizoadhibiwa kukata rufaa lakini kabla ya hearing ya rufani, TFF ya Jamal Malinzi imepanga timu kibonde ya Mbao FC ambayo hata kuwasafirisha wachezaji 15 kutoka Mwanza kwenda Geita ilikuwa inapata tabu.
Swali; Rufani Zimepuuzwa?