Jamal Mustafa wa Wasafi Media ni moto wa kuotea mbali

Jamaa kiukweli anajua kwenye masimulizi creativity ya hali ya juu niliacha kusikiliza The Story book hasa baada ya Mtiga kuondoka ila kwa Sasa jamaa Ni Moto wa Kuotea Mbali Professor
Mtiga alikuwa mzuri kwenye sauti tu ila Jamal anaweza sana kuchimbua hoja fikirishi, anasoma mno inaonekana si mtu poa kwakweli.
 
Muda wa kipindi? Masafa yake ni ngapi kwa pande za Dom?
 
Ila wasafi Ni wehu,kwny wasafi festival watu Wana mzuka na kukata mauno ya mziki wao wakampandisha huyo dogo aje kusoma ma vitabu yake jukwaani,wahuni wakazomea mwanzo mwisho ikabidi ashuke tu.

[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
huyo mwamba anajua ila combination yake na mtiga ndo ilikipendezesha kipindi, wakati ule anaandaa content alafu mtiga anasimulia kipindi kilikua fire sana.
 
Muda wa kipindi? Masafa yake ni ngapi kwa pande za Dom?
Sana sana yuko YouTube, The Story book.
Ni moja ya vipindi vizuri sana na kuna visa vingi sana uhadithia, vya kusisimua, kuhuzunisha, kuchekesha na kutisha zaidi na zaidi vikiambatana na picha.
Kwa Dodoma, Wasafi ni 104.1 Kalpana.

Karibu Chako tule kuku siku moja mpenzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…