Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Pamoja na uduni wake(IFM) katika suala la management, kuna suala moja linanikera zaidi! Na hili ni kuhusu ma-lecturer wa hapa IFM,yaan wamekuwa mabingwa wa ngono! Wanawarubuni dada zetu kwa madai ya kuwasaidia kielimu au saa nyingine kwa vitisho vya kuwafelisha! Na mtu anayeongoza kwa madhambi haya ni mkuu wa idara ya Social Protection! Kwa kweli jaman dada zetu wanateseka na hii tabia mbovu na chafu!
Mkuu heshima japo umekuwa specific kwa chuo kimoja ila unatakiwa kutazama mfumo mzima Tanzania. Suala la rushwa ya ngono ni kweli ipo na imejaa tele kwenye taasisi za elimu ya juu. Lakini si kwenye taaisis hizo tu hata serikalini watu siku hizi wanapeana vyeo kama malipo ya ngono.
Tukirudi katika taasisi za elimu ya juu. Ni dhahiri kabisa kuwa wanaosoma huko ni watu wazima wenye kujua wajibu wao na kujitambua katika jamii. Sasa mtu mzima anapolalamika kuwa amelazimishwa ngono kwa kutishwa basi huo tunauita ni ubakaji, na anastahili kumfikisha mtuhumiwa kwenye vyombo vya dola, ila kama atabakia kimya basi ni dhahiri ameridhia kitendo hicho. Ninachokiona katika post yako hii ambayo inakosa connection to the point on whether the weak management is the source of the practice or lack of ethics among academicians as well as students but no clear explanations from your post.
Mimi nimepitia pale UDSM miaka ile ya Mmari, tatizo hili lilikuwepo na ninakumbuka kuwa ilifikia hatua baadhi ya wanafunzi wenzetu wa kiume walikuwa wakigombana na baadhi ya wahadhiri kwa kuwa wapenzi wao wa kike walikuwa wakichukuliwa na wahadhiri hao. Nina hakika kabisa kuwa ingekuwa enzi hizi za utandawazi basi tungeshuhudia posts kama hizi kutoka kwa wanafunzi waliojikuta wanachangia wenza na walimu kwa kuwaanika hadharani as part of the fracas.
Tatizo la ngono kwenye mjumuiko wa watu wazima halikwepeki, nenda bungeni, nenda serikalini na maofisini, nenda shule za sekondari, nenda vyuoni. Kinachotakiwa hapa ni kuwa na miiko na kufuatiliwa ili anayeivunja apate adhabu stahili. Kama wachangiaji walivyosema njia pekee ya kuwa salama ni kufuata kilichokupeleka chuoni, yaani soma kwa bidii na fuata maelekezo mwisho wa siku utafaulu mtihani wako bila msaada wa rafiki, boyfriend, au lecturer. Ukifuata mob saikoloji ujue kuwa mitihani itafika ukiwa huna kitu kichwani ni hapo utakapojikuta unakuwa mtumwa wa ngono ili upitsihwe. Kama umeingia darasani na kujifunza mbili mara mbili ni nne, ni dhahiri ikija kwenye mtihani utajaza nne na hakuwa wa kukukosesha eti kwa kuwa umemnyima ngono.
umefika chuo wewe? kama hujui uhondo wa ngoma ingia ndani ucheze,vitu hivyo vipo sana vyuoni na kuna wengi wana masters, degree,advance diploma, diploma au certificate ZA CHUPI na inafika hatua mtu anadeclare hadharani kuwa bila kuachia utamu maisha yake chuoni yangetawaliwa na rabsharabsha za supplimentary kama sio discontinuationNaungana na wewe mkuu. umetoa maelezo mazuri sana. kwakweli mtoa maana ameeleza juujuu sana. Pia swala la msingi umeliezea vizuri, kwamba hakuna mtu wa mfelisha mwanafunzi eti kwakuwa anamtaka. HIYO HAIPO KABISA. KAMA UTAKA KUFAULU NI KUJUA NONDO TU. MTU AKIFELI NI KWAMBA HAJUI. KWAHITYO USHAURI KWA WANAFUNZI NI KUSOMA KWA BIDII NA SIVINGINEVYO.