Jamani, ashakum si matusi ila sisi Wabongo tuna mapungufu mengi ila kibaya zaidi tuko very very slow almost kwenye kila kitu

Ukiachana na hilo wabongo ni wazuri mno kwenye kusambaza taarifa ambazo hawana ukweli nazo.

Mtu anaambiwa tu jambo naye analisambaza utafikiri ana ufahamu nalo kumbe nae kaambiwa tu wala hata ukweli wenyewe haujui wala huyo nae aliyemwambia nae hana ufahamu na jambo hilo.
 
Umeandika mambo yenye uhalisia. Atakaye kushambulia atakuwa na matatizo ya akili. Mimi mwenyewe huwa ninakerwa sana na watu wanaofanya mambo yao taratibu.

Mfano unaenda kwenye ATM machine unakuta mtu anatumia zaidi ya dakika 5-10 kutoa hela! Na wakati hilo zoezi ni la dakika moja tu.
 
Wakati fulani mimi na jamaa yangu mmoja tulienda kumsikiliza motivational speaker mmoja anajiita Life Coach maeneo fulani.

Akawa anahimiza umuhimu wa kudamka alfajiri ili kuweka ratiba ya siku nzima na kuuandaa mwili na akili vizuri.

Kesho yake tukaamka alfajiri saa 10. Tukafanya mazoezi, tukaweka mambo safi kila mmoja kisha tukapigiana simu kukumbushana sisi ni jobless. Tukarudi kulala kusubiri simu za michongo ya saidia fundi.
 
Umechanganya mambo meengi kiasi ni ngumu kupata suluhisho ila naona kuna vitu vinaelezeka,
1. huyo dereva slow, huenda Bado anajifunza hajazoea

2. Watu kutembea slow, Hali ya hewa Ina mchango kiasi, Dar kuna jua Kali na humidity kubwa kwa sababu ya bahari. Na hakuna AC za kutosha kwenye majengo na vivuli njiani hakuna , huenda hii inachangia watu kulazimika kutembea pole pole Ili wasitoe jasho sana

3 uharaka wa kutembea unategemea na uhitaji, mfano wakati wa kwenda kazini cheki mbio huko barabarani makongo, mbezi ya chini kule, kilwa road..gari zinakimbizwa balaa sababu watu wanawahi kazini, kinyume chake jioni watu wanaenda sehemu za starehe au nyumbani hakuna pressure kabisa

4. U slow kwenye kufanya kazi ni mazoea
5 U slow kwenye kufanya maamuzi inachangiwa na uwezo binafsi wa kuchanganua mambo (akili)

Wengine waongezee Nini kifanyike
 
Jamani, do yaani tumefikia kukata tamaa.Lakini kweli maisha yamekugonga na ukichanganya na njaa basi akili na mwili mzima unadumaa ,hakuna haja ya kuwa sharp. kingine ufanye haraka,uchelewa hakuna motivation yeyote,sasa kwa nini niharakishe sasa
Njaa mbaya,uhakika wa kula nao very slow akili lazima idumae!
 
Watu wengi ni udumavu wa lishe, umeona milo ya wachina. Angalia mlo wa mtanzania kuanzia kifungua kinywa, hata nguvu ya kufanya kazi ngumu hawana. Watu ni goigoi
 
Hata wapiga debe wa kibongo kwenye magari wako very slow utasikia "ilala, complex, buguruni sheli mnyamaniiiiii" kwa sauti ya kiteja mdomo umelegea, nenda hata hapo kenya tu usikie "kigomba mbao mbao mbao kigombambambao mbao mbao, beba beba bebaaa!" yaani unaweza usielewe anamaanisha wapi ukabaki umesimama kama mlingoti, kumbe anakusudia kwenda sokoni gikomba ni shilingi 20 tu panda.
 
Kuna

Kuna watu watasoma huu uzi slow slow
 

Maelezo yako hayana ukweli kuhusu uwakaji wa taa!!

Inapotoka kwenye green na kuwaka red huchukua sekunde si chini ya tano kuwaka green upande mwingine!!

Thus why kuna orange kati ya green na red, ipo kitaalam kubalance hilo!! Japo kuna taa zingine hazina orange lakini set up ya ubadilikaji taa umesetiwa maalum kumruhusu gari ya mwisho kuvuka kabla nyingine hazijaruhusuwa!! Yaan ikikuruhusu wewe green light kule ilishawaka red kwa sekunde angalau kumi! Sijui kama umenielewa!!

Anayeamua kupita na red kaamua na mbaya zaidi taa za siku hizi zina sekunde kabisa!! So inakuonesha pale nawahi au laah ila madereva wa siku hizi ukaidi mwingi!! Hasa Bodaboda na bajaj!!

Kuhusu defensive driving, you right japo kuna madereva akifika kwenye taa kahamia kwenye simu!! Msipomshitua itawaka green itarudi red habari hana!! Iliwahi kutokea mataa ya Magomeni Mapipa imewaka green mpaka inaisha nipo nyuma yake na sikumpigia honi wala nini!! Ila inachange kutoka green kwenda orange ndipo anazinduka, akakurupuka speed kidogo agonge bodaboda!! Hupaswi kuchukia honi, ile ni katika kuwekana attention tu na si kukutaka uvuke sababu ya hali halisi ya udereva wa sasa japo hata mie kuna wakati huwa zinanikera!! Ukichukia honi Tanzania huwezi kuendesha gari katika jiji la Delhi nchini India (honking city) ukisimama honi ukiondoka honi ukitembea honi!!

Bado nasisitiza defensive driving ila haimaanishi uwe very slow taa ya sekunde 20 kama ya Kinondoni kanisani utavusha gari moja tuu!!
 
Okey pita mataa ya Ubungo na Kimara suka uconfirm hicho unachokieleza kwamba kuna rest period after red or green..taa zinazo count hazina orange ni green red. Zile ambazo hazicount ndo zina hiyo orange.
 
Nakubaliana na mleta mada, unapanda daladala imagine imejaza ile mbaya na watu wamekaa dirishani wamefunga vioo hawahisi hata mgandamizo wa hewa. Ukimwambia hii ni hatari anafungua kidgo anaendlea kuchezea simu au kulala. Wabongo hatuko aggresive hata kwenye fursa, mpigie jamaa jobless mwambie kuna nafasi njoo fasta utashangaa anakwambia hana elf mbili ya nauli hajala na nguo hajapasi... wtf?
 
Sio kutembea tu, hata katika huduma mbalimbali wanakuwa slow sana,
Makondakta, wapiga debe na madalali wa tiketi ndio huwa wako haraka sana kwa wateja.
 
Vipi kwenye kula Tunda kimasihara tuko slow au fast?
Ahhaaaa kwa kweli wavivu wengi, mbumbumbu wengi, masikini wengi wanapoenda vitu vyashortcut, halafu ni qapenzi wa starehe sana, hasa hasa starehe ya tunda na ndio maana tunazaliana kama nguruwe na kutengeneza viscous cycle ya poverty
 
Yaani umetoa mifano mizuri sana tuko very slow kwenye kila kitu,nina ndugu zangu fulani ni jobless, ok ila mmoja ni fundi na mwingine ni mtaalamu wa computer, huyu mtaalamu wa computer ndugu mmejichanga na mumfungulia duka la vifaa na kutengeneza computer ili achichange na kuyamudu maisha na kuendeleza. Unaambiwa jamaa anakuja kazini saa nne, na kufunga saa 10.00, jumamosi haji kazini, akiitwa kazini hatokei, kila siku anataka hela kwa mdada wa dukani. Huyu wa umeme, ukimpa dili kwa mtu atatokea siku ya kwanza tu baada ya hapo, wiki hiyo hiyo anakupiga mizinga. Yaani hayo ndiyo maisha ya kibongo, tunachukulia mzaa sana kwenye mambo serious ya maisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…