Jamani Bagia za Iringa tamu, hasa za Kalenga!

Jamani Bagia za Iringa tamu, hasa za Kalenga!

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Leo asubuhi nimeamka na hamu ya BAGIA ZA IRINGA, hasa za KALENGA!, liliko fuvu la Chifu Mkwawa aliyekuwa kiongozi wa Wahehe aliyepinga ukoloni wa Kijerumani mwishoni mwa karne ya 19 kabla ya kujiua mwaka 1898 ili kuepuka kukamatwa.
IMG_6200.jpeg

Tuachane na ishu za historia maana isije ikawa ni chenga ya maudhi kwa hawa GEN Z, acha niendelee na michapo ya hizi Bagia za Kalenga, vitafunwa vya kitamaduni, vinavyotokana na Kunde, ambapo hutiwa viungo (chumvi n.k), kisha kukaangwa hadi kuwa na rangi ya kahawia na kuwa na ukoko wa nje.
IMG_6199.jpeg

Utake mwenyewe ule bila pilipili au ule na kiungo hicho ili kuongeza ladha.
IMG_6201.jpeg

Kutokana na umaafuru wake Bagia hizi kupikwa Kalenga na kusafirishwa mapema alfajiri Iringa mjini umbali wa km 14.6, na kuwauzia wasafiri mbalimbali kwenye vituo vya mabasi.
IMG_6202.jpeg

Hii ni moja ya biashara kubwa kwa kina Mama, na wamekuwa wakitengeneza kipato kwa ajili ya familia zao.

Soma ==> Historia ya Mkwawa na Uhehe
 
Nasubiri uweke location ya sambusa za kalenga ama idodi..na ingredients!
 
Vitu vya kulakula, wanaita ubuge.

Umenikumbusha mbali huu ubuge. Wakati niko shule ya msingi, nikizikamatia hela tu, nilikua nakwenda kununua sambusa 40 au hata 50. Nakaa zangu sehemu kwenye majani nakula namaliza zote.

Mapishi ya Kitanzania matamu sana.
 
Nilisoma heading harakaharaka nikadhani "bangi za Iringa tamu"
 
Vitu vya kulakula, wanaita ubuge.

Umenikumbusha mbali huu ubuge. Wakati niko shule ya msingi, nikizikamatia hela tu, nilikua nakwenda kununua sambusa 40 au hata 50. Nakaa zangu sehemu kwenye majani nakula namaliza zote.

Mapishi ya Kitanzania matamu sana.
Huu ndiyo ustaarabu sasa, siyo Jitu linakuja na bagia au sambusa kiduchu mbele za Watu kuwatamanisha ilihali lilishavimbiwa pembeni 🤗

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
 
Hizo bagia za kunde mbona toka zamani Dar watu walikuwa wanakaanga na kuuza. Au wewe ni wa 2000, alaf ndio kwanza unaziona?
 
Leo asubuhi nimeamka na hamu ya BAGIA ZA IRINGA, hasa za KALENGA!, liliko fuvu la Chifu Mkwawa aliyekuwa kiongozi wa Wahehe aliyepinga ukoloni wa Kijerumani mwishoni mwa karne ya 19 kabla ya kujiua mwaka 1898 ili kuepuka kukamatwa.
View attachment 3087346
Tuachane na ishu za historia maana isije ikawa ni chenga ya maudhi kwa hawa GEN Z, acha niendelee na michapo ya hizi Bagia za Kalenga, vitafunwa vya kitamaduni, vinavyotokana na Kunde, ambapo hutiwa viungo (chumvi n.k), kisha kukaangwa hadi kuwa na rangi ya kahawia na kuwa na ukoko wa nje.
View attachment 3087347
Utake mwenyewe ule bila pilipili au ule na kiungo hicho ili kuongeza ladha.
View attachment 3087348
Kutokana na umaafuru wake Bagia hizi kupikwa Kalenga na kusafirishwa mapema alfajiri Iringa mjini umbali wa km 14.6, na kuwauzia wasafiri mbalimbali kwenye vituo vya mabasi.
View attachment 3087355
Hii ni moja ya biashara kubwa kwa kina Mama, na wamekuwa wakitengeneza kipato kwa ajili ya familia zao.

Soma ==> Historia ya Mkwawa na Uhehe
Kutokana na kupigia promo kubwa sana hizo Bagia, zisije zikawwa zimechanganywa na kile kilaji maarufu Cha watu wa Iringa Cha yule mnyama😁
 
Back
Top Bottom