hivi kuna wapenzi hapa duniani ambao wanatumia condom...kila siku nasikia watu wanapigana kavu kavu dah!! tutakufa wengi aisee...
subiri kwanza ukapime tena baada ya miezi mitatu. Upo uwezekano mkubwa kuwa nawe ni muathirika, ila titre haijafika ya kusomeka...
yesu wangu na maria.....
wewe mtoto wewe .... iyo ni alert tu mungu amekupa kwamba hayo mapenzi uliyoyaparamia kwa pupa ipo siku yatakutokea puani .... tena inabidi ukapime tena maana si ulishangonoka na alex bila condomu?
mimi nakushauri umrudie mungu .....
achana na zinaa na tamaa za dunia hii....
tulia kama mimi ...
soma kwa sasa ,mapenzi yapo nenda taratibu dunia hii....
well said Smile. sina cha kuongeza hapo
Duh!Hongera kwa uzima wa afya,jikague ujue ni kitu gani kilikufanya uachane na na mpenzi wa kwanza!Usiniambie ni upendo!
Unaonja MOTO kwa ulimi? Acha ukuunguze.....!
Wasichana wengi wanapovuka tabaka moja kwenda jingine mara nyingi hudharau wale waliowaacha nyuma au chini. Mathalani, akipata kazi na mpenzi wake akawa bado ni mtu wa mtaani, ni rahisi huyo wa mtaani kutoswa.
Hapa tumeona mfano hai wa Happy kumwacha Alex vile tu kafanikiwa kufika chuo kikuu na huko kakutana na Victor,so far kijana ambaye kielimu kamzidi Alex.
Dada Happy, inampasa asubiri baada ya muda fulani upite halafu apime tena mara mbili au zaidi ili kwa uhakika kabisa athibitishe kuwa yu mzima.
Pili, kwa heshima ya wanaume wote tafadhali Happy muache Alex aendelee na maisha yake maana awali si kwamba ulitupa tu jongoo, bali ulitupa pia na mti wake.
Mwenyewe kwa matamshi yako hapo juu umekiri kuwa "mwaka mmoja uliopita ulipofika chuoni ulitokea kumpenda kijana mmoja kwa jina Victor"...hivyo sidhani kama kweli Alex ni aina ya mwanume ambaye kwako unaona ndiye akufahaye pamoja na mambo yote mlofanya mkiwa A-Level.
"Majuto ni mjukuu"
if this is true inatakiwa tuachana na kuwalaumu wote wawili. Kinachotakiwa ni namna ya kukata hii chain isiendelee haraka. Mfano hapy akirudi kwa alex hatuko sure kama yuko salama kwani kuna vile vifaa vya mtasiwa hivyo utaendelea kusambaa. Pia akimuaacha vikta kuna vitu vingi,anaweza kuuawa na victa na ye kujiua,vikta ataanza kusambaza kwa hasira,hana uhakika kama alex yuko salama. Kinachotakiwa ni wao kuendelea kupeana psychological support ili victor asipatwe na severe post traumatic stress disorder. Kwani kitendo cha kujua tu unao unapatwa na stress,ukiongeza na kuachwa sababu hiyo na ule wasiwasi wa leaking of information ikifuatiwa na unyanyapaa hali inakuwa ngumu zaidi. Take responsibility ya kumfanya jamaa azoee situation(ni ngumu lakini kuna vitu vitapungua) huku mkiendelea kujadili mustakabali wenu. Vile unavyofikiri ungejisikia wewe ingekupata hali hiyo hata mwenzio atakuwa hivyo. Kuwa mvumilivu,achana na tamaa kwa muda huu,muombe mungu akupe nguvu.