Jamani naomba ushauri wa haraka iwezekanavyo

Jamani naomba ushauri wa haraka iwezekanavyo

Joseph

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2007
Posts
3,518
Reaction score
1,089
Leo nimeamka asubuhi na mke wangu,cha kushangaza ni kukuta amechanjwa chale mapajani yaani kila paja chale mbili.
Tumejaribu kujadili ni nini hasa kimetokea tunashindwa kujua,sisi ni wacha Mungu na huwa tunasali kabla ya kulala na hata katika maisha yetu ya kila siku tunamtanguliza Mungu.
Wadau naomba ushauri wenu wa nini kinaendelea na nini cha kufanya.
 
mkuu Joseph ninahakika hayo ni majaribu tu inabidi mzidishe maombi mtashinda,kama mlikua mnasali kabla ya kulala sasa anzisha mchakato wa kulala mapema then amkeni na familia yenu yote kuanzia saa saba msali hata kwa masaa mawili then wewe na mkeo salini mara kwa mara hata mara tatu kwa usiku mzima.naamini hayo ni majarbu ukifanya kwa mfululizo utamjua nani kafanya hvyo ndani ya mwezi.mwambie Mungu sifi mpaka nimeuona utukufu wako,siogopi lolote kwakua najua upo nami wakati wote,fanya muujiza kabla hakujapambazuka....nipe feedback
 
Last edited by a moderator:
mkuu Joseph ninahakika hayo ni majaribu tu inabidi mzidishe maombi mtashinda,kama mlikua mnasali kabla ya kulala sasa anzisha mchakato wa kulala mapema then amkeni na familia yenu yote kuanzia saa saba msali hata kwa masaa mawili then wewe na mkeo salini mara kwa mara hata mara tatu kwa usiku mzima.naamini hayo ni majarbu ukifanya kwa mfululizo utamjua nani kafanya hvyo ndani ya mwezi.mwambie Mungu sifi mpaka nimeuona utukufu wako,siogopi lolote kwakua najua upo nami wakati wote,fanya muujiza kabla hakujapambazuka....nipe feedback
Nashukuru sana Ruhazwe kwa kunitia imani na nitauchukua ushauri wako na kuufanyia kazi
 
Leo nimeamka asubuhi na mke wangu,cha kushangaza ni kukuta amechanjwa chale mapajani yaani kila paja chale mbili.
Tumejaribu kujadili ni nini hasa kimetokea tunashindwa kujua,sisi ni wacha Mungu na huwa tunasali kabla ya kulala na hata katika maisha yetu ya kila siku tunamtanguliza Mungu.
Wadau naomba ushauri wenu wa nini kinaendelea na nini cha kufanya.

Ni vyema muendelee na maombi. Kuchanjwa usiku na mtu usiyemfahamu ni dalili tosha za kuwa mmechezewa na imani za kishirikiana.
 
Ni vyema muendelee na maombi. Kuchanjwa usiku na mtu usiyemfahamu ni dalili tosha za kuwa mmechezewa na imani za kishirikiana.

Tunaendelea na maombi na tunahitaji ya kwako pia maana huku nilipo hakuna kanisa wala mchungaji japo tunaweza pata ushauri wa kiimani.
 
Leo nimeamka asubuhi na mke wangu,cha kushangaza ni kukuta amechanjwa chale mapajani yaani kila paja chale mbili.
Tumejaribu kujadili ni nini hasa kimetokea tunashindwa kujua,sisi ni wacha Mungu na huwa tunasali kabla ya kulala na hata katika maisha yetu ya kila siku tunamtanguliza Mungu.
Wadau naomba ushauri wenu wa nini kinaendelea na nini cha kufanya.

Endelea tu na maombi hakuna njia nyingine sahihi zaidi ya hiyo shetani anataka kukupima imani yako tu kama ipo haba
 
Tunaendelea na maombi na tunahitaji ya kwako pia maana huku nilipo hakuna kanisa wala mchungaji japo tunaweza pata ushauri wa kiimani.
Pole sana..........inahitajika kujizatiti kiimani zaidi, kama inawezekana ufunge safari na kumleta Padre/mtumishi aombe nanyi na kuibariki nyumba yako na familia nzima
 
Leo nimeamka asubuhi na mke wangu,cha kushangaza ni kukuta amechanjwa chale mapajani yaani kila paja chale mbili.
Tumejaribu kujadili ni nini hasa kimetokea tunashindwa kujua,sisi ni wacha Mungu na huwa tunasali kabla ya kulala na hata katika maisha yetu ya kila siku tunamtanguliza Mungu.
Wadau naomba ushauri wenu wa nini kinaendelea na nini cha kufanya.
Swali ni kwamba je hizo alama mlichunguza kama zipo kipindi mnaenda kulala au mmejikuta zipo asubuhi? suala lingine inwezekana ikawa ni matatizo ya ngozi jaribu kuwaona madaktari wa ngozi kwa ushauri zaidi, na pia endeleeni kufanya maombi
 
Pole sana..........inahitajika kujizatiti kiimani zaidi, kama inawezekana ufunge safari na kumleta Padre/mtumishi aombe nanyi na kuibariki nyumba yako na familia nzima
Asante sana,nitajitahidi kufanya hivyo pia.
 
Swali ni kwamba je hizo alama mlichunguza kama zipo kipindi mnaenda kulala au mmejikuta zipo asubuhi? suala lingine inwezekana ikawa ni matatizo ya ngozi jaribu kuwaona madaktari wa ngozi kwa ushauri zaidi, na pia endeleeni kufanya maombi
Hatukuwa tumezichunguza wakati tunaenda kulala ila wakati wa kuamka asubuhi ndio mke wangu akaziona na zilikuwa bado zina damu damu ikimaanisha kuwa hazikuwa za muda mrefu sana,bahati nzuri mke wangu ni daktari na anajua vizuri kuhusu mambo ya ngozi hivyo suala la kuwa inawezekana ni matatizo ya ngozi halipo,bahati mbaya siwezi kupiga picha maeneo ya alama zilipo hizo chale ila hazifichiki hata kwa kuangalia kwa umbali wa mita moja.
Nashukuru sana na tunaendelea na maombi.
 
Pole sana mkuu!
Hayo ni majaribu ya shetani, kazana sana ktk maombi maana shetani ameona kuna kitu fulani mnakaribia kufanikiwa ambacho mmekuwa mnakiomba kwa muda mrefu, anachofanya ni kujaribu kuwakatisha tamaa ili msifikie lengo lenu. Endeleeni kuomba na kumtanguliza Mungu kwa kila jambo.
 
Aisay yani utani pembeni ningekuwa mimi ningeisha hama nyumba, poleni sana mnaishi na majini :scared:
 
Cha muhimu ni kuwa usiwe na wasiwasi. Endelea kusali kwa ratiba sawa na unavyosali sasa. Usifikirie kuhama nyumba wala kanisa unalosali. Elewa tu kuwa shetani anakujaribu, na ukiogopa anapata pa kushikilia
Kumbuka kuwa biblia imerudia mara nyingi sana neno ...USIOGOPE... Ukiogopa tu (bila kujali unasali au una imani kiasi gani), utaanza kuzama kama Petro alivyotaka kuzama alipotembea juu ya maji...
 
poleni sana,kazaneni kuomba sana na MUNGU mwaminifu atasikia maombi yenu
 
hapo mkuu,
inatakiwa uwe na imani tena imani kweli kweli kwa MUNGU. tena ukubali
kabisa kuwa MUNGU anaweza. kesheni mkiomba ila msipige kelele hata mtu wa nyumba
ya pili asikie. kwa imani yangu MUNGU wetu ni mwaminifu tena ukimwita
anasikia hasa sala za machozi, MUNGU huwa anajibu hapo hapo. simama imara
katika kuomba na hakika MUNGU wetu atakuonyesha kitu.
 
Pole sana mkuu!
Hayo ni majaribu ya shetani, kazana sana ktk maombi maana shetani ameona kuna kitu fulani mnakaribia kufanikiwa ambacho mmekuwa mnakiomba kwa muda mrefu, anachofanya ni kujaribu kuwakatisha tamaa ili msifikie lengo lenu. Endeleeni kuomba na kumtanguliza Mungu kwa kila jambo.
Asante sana mkuu na nashukuru sana kwa ushauri
 
Majaribu ni kipimo kwa mtu aliyeokoka, Msichoke kuomba, vilevile mnaweza kuongezea na kufunga hata kwa siku moja ama tatu. Hizo ni nguvu za giza hamna haja ya kuogopa, maana kushindana kwetu si kwa damu na nyama bali ni............ Mungu wa Mbinguni na aendelee kuwalinda na kuwaepusha na mabaya yote. Msome zaburi ya 127. Bwana awe nanyi daima- Amen
Leo nimeamka asubuhi na mke wangu,cha kushangaza ni kukuta amechanjwa chale mapajani yaani kila paja chale mbili.
Tumejaribu kujadili ni nini hasa kimetokea tunashindwa kujua,sisi ni wacha Mungu na huwa tunasali kabla ya kulala na hata katika maisha yetu ya kila siku tunamtanguliza Mungu.
Wadau naomba ushauri wenu wa nini kinaendelea na nini cha kufanya.
 
hapo mkuu,
inatakiwa uwe na imani tena imani kweli kweli kwa MUNGU. tena ukubali
kabisa kuwa MUNGU anaweza. kesheni mkiomba ila msipige kelele hata mtu wa nyumba
ya pili asikie. kwa imani yangu MUNGU wetu ni mwaminifu tena ukimwita
anasikia hasa sala za machozi, MUNGU huwa anajibu hapo hapo. simama imara
katika kuomba na hakiki MUNGU atakuonyesha kitu.
Nashukuru sana kwa ushauri na tutaufanyia kazi kwani tunaamini maombi pekee ndio yatakayotuvusha katika hili,naomba pia utujumuishe katika maombi yako maana kwa sasa tunahitaji msaada wa kuunganisha nguvu pamoja na wengine kama wewe ndugu.
 
Back
Top Bottom