Jamani nimelogwa au!!!!!

Na mimi nilishaanza kuhisi umeniloga! jitahidi kushinda hili jaribu mana mi nimeshalishinda! lol. .
 
Una uhakika gani na yeye anataka kujiingiza kwenye uhusiano na na wewe. Mtokee kwanza ili uone, pengine unajisumbua tu kufikiri kumbe mwenzako hana mawazi hayo. Mtokee akikataa automatically ukaribu utaisha na kazi zitaendelea. Akikubali chukua karatasi mbili. Andika jedwali lenye faida na hasara za kila option. yaan ku do na kutoduu. Nenda buchani muombee muuza nyama mizani. Zipime kila moja upande wake wa mizani. Chukua option yenye uzito zaidi. Jumapili njema.
 
Kuna movie inaitwa I think I love my wife ya Chris Rock ndio kama hii sred yako.
 
 
Usijidai umerogwa hakunaanaye weza kukuroga hapa duniani isipo kuwa mungu kataka.

Kama mchawi anaweza kuroga mwambie awe mfalme kama anaweza.

Wewe unasumbuliwa na nyege hujarogwa wala nini.
 
khaaa! kwani mkeo anakasoro gani au koz anawatoto wawili na huyo madamu yuko na mmoja unafikiri kutakua na tofauti..........ebu kimbia zinaa iyooo
 
Punguza ukaribu!hata kama mnashirikiana kwnye kazi ukaribu ucvuke mipaka, onyesha mcmamo wako kama mwanaume mwenye familia!
 
Usitafute mchawi sehemu nyinge. Unaye hapo hapo. Naye ni TAMAA YA MWILI. Mkemee kwa jina la Yesu ataondoka mara moja.

Ni kweli,
"Maana mtu awaye yote
atakayeishika sheria yote, ila
akajikwaa katika neno moja,
amekosa juu ya yote." Yakobo
2:10
 
Ng'oa mzizi wa fitina! Mfanye family friend! Mkaribishe yeye na mumewe na mkeo mkutane mahali wknd mjadili mambo ya siasa na familia. Itakufunga luku hutakaa uthubutu kumtamani. Bible inasema mwanamke atamlinda mwanaume, mruhusu mkeo akulinde!
Hujalogwa ila una mpango wa kujiloga!
 
Thread yako imenikumbusha Mwl. wangu wa Biology alikua anaitwa Mwl. SITAKI NATAKA , kuna siku alituchorea ALMENTARY TAMAA huku amefumba macho! Mkuu vi-elements viko % kubwa vinaonesha kumeganaisims kumeshateki plesi. Hapa unasikilizia
how to balance your sin .
 
ukishafanya game na huyo mudada-ndo itakuwa mwanzo wako wa kutoka nje-mwisho wa siku yatakukuta zaidi ya yaliyomkuta a. malima
 
ukweli kwamba huyo dada naye ni mke wa mtu ina-complicate issue nzima... angekuwa single angekuwa fair game
 
Inawezekana vilevile kwamba umerogwa. Wanawake wa siku hizi hawaaminiki. Kama ana mipango mibaya na wewe au ana hisi kuna kitu fulani atapata kutoka kwako anaweza kila njia akuweke kwenye mikono yake. Shukuru Mungu umetambua hilo, jaribu kuwa mbali naye kwa faida ya Ndoa na familia yako.
 

Piga goti ndugu sali sana.Na mwambie huyo dada kila siku kuwa unampenda sana mkeo na yeye aendelee kumpenda mumewe.Ukiona vipi changua mkeo au kazi.Kuna kashetani kanataka kuharibu hapo.Sala iwe ndio uchawi wako.sali sana kaka.
 
Punguza ukaribu nae na muonyeshe kwamba wampenda mkeo na haupo tayari kumdanganya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…