Jamani, nimeokota mapesa!

Jamani, nimeokota mapesa!

Kwa nabii flora kulikuwa na shuhuda motomoto za waumini kuokota mamilioni kwenye daladala, kwenye magodolo n.k
Lakini next Sunday yule muumini sadaka anatoa buku na kuonyesha ishara kuwa asubuhi hajapata chai.
Yes.
Yesu yupo anaweza kutumia malaika kugawa pesa n.k
Mungu akubariki
 
tangazo limekaa kimkakati ukizingatia valentine iko jirani utakuwa na kazi kubwa uko pm.
 
Hongera..!! Kuna Uwezakano Kama Ikikuwia Vyema Ukaniwezesha Shilingi 10000 Ya Kitanzania?
Usimuombe mtu pesa. Muombe Mungu. Fedha na dhahabu ni mali yake.
Hii ni ahadi ya Yesu kwamba tukimuomba Mungu tutapewa. Mathayo 7:7-12
“Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtapata; bisheni nanyi mtafunguliwa mlango. Kwa kuwa kila aombaye hupewa; naye kila atafutaye hupata; na kila abishaye hufunguliwa mlango. “Au ni nani miongoni mwenu ambaye mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe? Au mwanawe akimwomba samaki atampa nyoka? Basi ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao?..."
 
ikiwa ni mwaminifu,mcha Mungu,bora apeleke polisi kama mali ya kuokota,kisha apewe RB itakayomfanya akae kwa kipindi fulani,asipopatikana mwenyewe ndipo atapewa kutumia kama pesa za kuokota zilizokosa mwenyewe.
Imeandikwa wapi hiyo, maana tunaongozwa na Maandiko Matakatifu
 
tangazo limekaa kimkakati ukizingatia valentine iko jirani utakuwa na kazi kubwa uko pm.
Sio tangazo, ni habari. Hata hivyo, upendo unapaswa kuonekana siku zote, siyo Valentine Day tu. Waebrania 13:1-8 "Upendano wa ndugu na udumu..."
 
Be blessed
Heshima zenu Wakuu! Nawaletea habari ya kweli, kweli kabisa, maana mimi nauchukia uongo kama ukoma! Nimeokota mapesa. Sasa usiniulize ni dola ngapi, usije ukashawishika kunifuata uninyang’anye!

Wewe jua tu nimeokota mapesa kama wana wa Israeli walivyookota “mana” jangwani. Mimi nafanya kazi kwa bidii ili kujipatia kipato.

Hata hivyo, pamoja na kufanya kazi ninamtegemea Mungu kila wakati, kwakuwa najua unaweza kufanya biashara usipate wateja/pesa. Unaweza kuajiriwa ukafukuzwa kazi.

Unaweza kupata pesa zikaibiwa zote! Hivyo ni muhimu kumtegemea Mungu. Kwa kufanya hivyo nimeona Mungu akinifanikisha na kunitendea miujiza mingi.

Haya, turudi kwenye mada. Ilikuwa hivi: Kuna watu watatu walikuja ofisini kwangu wiki iliyopita, kwa wakati tofauti na siku tofauti. Wote ninawafahamu na huwa ninawasiliana nao.

Niliwahudumia wakaondoka. Jana mchana, niliingia ofisini kwangu, nikachungulia chini ya viti vya wageni. Kwa mshangao mkubwa nikaona mapesa! Mimi ni mwaminifu sana kwa habari ya pesa.

Nikija dukani kwako ukinizidishia chenji nakurudishia. Nikasema moyoni mwangu haya mapesa nadhani ni wale jamaa waliokuja ofisini kwangu wameyadondosha. Siwezi kuyatumia.

Nikawapigia simu na kuwauliza kama waliona upungufu wa pesa kwenye mifuko yao baada ya kuondoka. Wote wakakataa na kunipa kibali cha kuyatumia hayo mapesa.

Jamani Mungu ni Mkuu sana! Nawasikitikia wanaosema eti Mungu hayupo. Wanakosa baraka nyingi.

Tangu nimwamini Yesu, nimeona miujiza mingi ya kupita kawaida.

Hata huo ni muujiza. Nilikuwa na shida ya pesa, nikamuomba Mungu, amenipa mapesaaa! Stay blessed!
 
sheria za nchi zinasema hivyo.
Hahaa. Nchi ipi, na mimi niko nchi ipi? In every corner of this world, kila nchi ina sheria zake. We're all living under different rules—each country brings its own flavor, its own way of governing life. So, remember: no matter where you are, each nation stands unique with its own set of laws and customs. Tuko pamoja?
 
Katika sheria ya Uislamu, mali ya kuokota, ikiwa ina thamani kubwa basi inabidi uitangaze kwa muda wa mwaka mmoja.

Baada ya hapo ikiwa hajapatikana mwenyenayo ndio inakuwa halali yako, unaweza kuitumia.
 
Usimuombe mtu pesa. Muombe Mungu. Fedha na dhahabu ni mali yake.
Hii ni ahadi ya Yesu kwamba tukimuomba Mungu tutapewa. Mathayo 7:7-12
“Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtapata; bisheni nanyi mtafunguliwa mlango. Kwa kuwa kila aombaye hupewa; naye kila atafutaye hupata; na kila abishaye hufunguliwa mlango. “Au ni nani miongoni mwenu ambaye mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe? Au mwanawe akimwomba samaki atampa nyoka? Basi ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao?..."
Haya!!Uwe Na Siku Njema
 
Umeandika ukiwa na wenge jingi sana halafu umejichanganya hata haueleweki, lengo la huu uzi ni nini?

Kuokota mapesa au kutangaza injili ya YESU? Au kujitangazia wewe ni muaminifu?

Halafu uaminifu wa mtu hautangazwi na mtu mwenyewe. Eti mimi ni muaminifu 🤣🤣🤣 hebu jishikilie basi.
Lengo la uzi umelielewa ila sema umebaki na maswali. Halafu ungejuaje mimi ni mwaminifu kama nisingesema? Hata Yesu alijitaja jinsi alivyo: "Mimi ni Nuru ya Ulimwengu... Mimi ni Njia na Kweli na Uzima. .. Mimi ni Mchungaji Mwema nk nk." Hivyo usishangae kusikia ninajiita "Mwaminifu" Ndivyo nilivyo, ni tabia yangu.
 
Lengo la uzi umelielewa ila sema umebaki na maswali. Halafu ungejuaje mimi ni mwaminifu kama nisingesema? Hata Yesu alijitaja jinsi alivyo: "Mimi ni Nuru ya Ulimwengu... Mimi ni Njia na Kweli na Uzima. .. Mimi ni Mchungaji Mwema nk nk." Hivyo usishangae kusikia ninajiita "Mwaminifu" Ndivyo nilivyo, ni tabia yangu.
Yesu alishawahi kusema yeye ni mwaminifu
 
Na mitego ya Shetani huwa inapitia kwenye shida ulizonazo.
Sidhani kama M-ungu analeta riziki kwa njia ya kuokota bali baraka za kazi uzitendazo.
Shetani haniwezi mimi. Nimepewa mamlaka ya kumkemea kwa Jina la Yesu.
Nimekuambia unaweza kufanya kazi usipate pesa/wateja. Hivyo usiweke matumaini yako yote kwenye kazi yako. By the way, hujasoma habari za wana wa Israeli jangwani? Soma 📖 Kutoka 16:14-15. Kila siku walikuwa wanaokota "mana"(chakula kitamu sana). Unashangaa mimi kuokota mapesa kwa siku moja tu? Je, ningekuambia kila siku naokota?
 
Back
Top Bottom