Jamani, nimeokota mapesa!

Jamani, nimeokota mapesa!

Ubarikiwe sana mtumishi. Kweli kila asemaye Mungu hayupo ni mpumbavu
 
Heshima zenu Wakuu! Nawaletea habari ya kweli, kweli kabisa, maana mimi nauchukia uongo kama ukoma! Nimeokota mapesa. Sasa usiniulize ni dola ngapi, usije ukashawishika kunifuata uninyang’anye! Wewe jua tu nimeokota mapesa kama wana wa Israeli walivyookota “mana” jangwani. Mimi nafanya kazi kwa bidii ili kujipatia kipato. Hata hivyo, pamoja na kufanya kazi ninamtegemea Mungu kila wakati, kwakuwa najua unaweza kufanya biashara usipate wateja/pesa. Unaweza kuajiriwa ukafukuzwa kazi. Unaweza kupata pesa zikaibiwa zote! Hivyo ni muhimu kumtegemea Mungu. Kwa kufanya hivyo nimeona Mungu akinifanikisha na kunitendea miujiza mingi.

Haya, turudi kwenye mada. Ilikuwa hivi: Kuna watu watatu walikuja ofisini kwangu wiki iliyopita, kwa wakati tofauti na siku tofauti. Wote ninawafahamu na huwa ninawasiliana nao. Niliwahudumia wakaondoka. Jana mchana, niliingia ofisini kwangu, nikachungulia chini ya viti vya wageni. Kwa mshangao mkubwa nikaona mapesa! Mimi ni mwaminifu sana kwa habari ya pesa. Nikija dukani kwako ukinizidishia chenji nakurudishia. Nikasema moyoni mwangu haya mapesa nadhani ni wale jamaa waliokuja ofisini kwangu wameyadondosha. Siwezi kuyatumia. Nikawapigia simu na kuwauliza kama waliona upungufu wa pesa kwenye mifuko yao baada ya kuondoka. Wote wakakataa na kunipa kibali cha kuyatumia hayo mapesa.

Jamani Mungu ni Mkuu sana! Nawasikitikia wanaosema eti Mungu hayupo. Wanakosa baraka nyingi. Tangu nimwamini Yesu, nimeona miujiza mingi ya kupita kawaida. Hata huo ni muujiza. Nilikuwa na shida ya pesa, nikamuomba Mungu, amenipa mapesaaa! Stay blessed!
Lete tupicha picha
 
kwa masikitiko makubwa naona bado mpaka sasa bado hujatoa sadaka ya shukrani madhabahuni naona maneno matupu ya kushukuru mitandaoni,

hata hivyo,
Neema, Baraka na Upendo wa bwana Yesu Kristo wa Nazareth viwe nanyi nyote sasa na hata milele,

na wenye pumzi wote na wasema Aimen 🙏
Mimi nikitoa sadaka, sipigi tarumbeta🎺kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu. Mt 6:2
 
Mimi nikitoa sadaka, sipigi tarumbeta🎺kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu. Mt 6:2
ni muhimu zaidi sifa na utukufu wa Mungu kwenye maisha yetu, vikaambatana na ushuhuda wa shukrani madhabahuni, kuliko kujisifu kwa wema mitandaoni :MODS:
 
Heshima zenu Wakuu! Nawaletea habari ya kweli, kweli kabisa, maana mimi nauchukia uongo kama ukoma! Nimeokota mapesa. Sasa usiniulize ni dola ngapi, usije ukashawishika kunifuata uninyang’anye! Wewe jua tu nimeokota mapesa kama wana wa Israeli walivyookota “mana” jangwani. Mimi nafanya kazi kwa bidii ili kujipatia kipato. Hata hivyo, pamoja na kufanya kazi ninamtegemea Mungu kila wakati, kwakuwa najua unaweza kufanya biashara usipate wateja/pesa. Unaweza kuajiriwa ukafukuzwa kazi. Unaweza kupata pesa zikaibiwa zote! Hivyo ni muhimu kumtegemea Mungu. Kwa kufanya hivyo nimeona Mungu akinifanikisha na kunitendea miujiza mingi.

Haya, turudi kwenye mada. Ilikuwa hivi: Kuna watu watatu walikuja ofisini kwangu wiki iliyopita, kwa wakati tofauti na siku tofauti. Wote ninawafahamu na huwa ninawasiliana nao. Niliwahudumia wakaondoka. Jana mchana, niliingia ofisini kwangu, nikachungulia chini ya viti vya wageni. Kwa mshangao mkubwa nikaona mapesa! Mimi ni mwaminifu sana kwa habari ya pesa. Nikija dukani kwako ukinizidishia chenji nakurudishia. Nikasema moyoni mwangu haya mapesa nadhani ni wale jamaa waliokuja ofisini kwangu wameyadondosha. Siwezi kuyatumia. Nikawapigia simu na kuwauliza kama waliona upungufu wa pesa kwenye mifuko yao baada ya kuondoka. Wote wakakataa na kunipa kibali cha kuyatumia hayo mapesa.

Jamani Mungu ni Mkuu sana! Nawasikitikia wanaosema eti Mungu hayupo. Wanakosa baraka nyingi. Tangu nimwamini Yesu, nimeona miujiza mingi ya kupita kawaida. Hata huo ni muujiza. Nilikuwa na shida ya pesa, nikamuomba Mungu, amenipa mapesaaa! Stay blessed!
Niumie Fungu la Kumi nikubariki uendelee kupokea miujiza.
 
shukrani madhabahuni,
Kumbuka kisa cha wale wenye ukoma kumi. Baada ya kutendewa muujiza wa uponyaji, waliambiwa wakajionyeshe kwa makuhani, sio wakatoe sadaka ya shukrani kwa makuhani. Katika wale kumi mmoja tu ndiye aliyetambua shukrani anapaswa kupewa Yesu, akarudi kutoa shukrani kwa Yesu, na Yesu akamsifia.
Lk 17:11-18
Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya. Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali, wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu! Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika. Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu; akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria. Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi? Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?

Yesu ni Mungu. Yupo mahali pote. Shukrani zinazotolewa hata kwa njia ya mitandao anaziona na anazipokea.
 
Niumie Fungu la Kumi nikubariki uendelee kupokea miujiza.
Mtu habarikiwi kwa kutoa fungu la kumi tu bali kwa kusikia na kutenda kila neno aliloliagiza Mungu. Soma uzi huu ujue vigezo na masharti ya kubarikiwa
 
Kumbuka kisa cha wale wenye ukoma kumi. Baada ya kutendewa muujiza wa uponyaji, waliambiwa wakajionyeshe kwa makuhani, sio wakatoe sadaka ya shukrani kwa makuhani. Katika wale kumi mmoja tu ndiye aliyetambua shukrani anapaswa kupewa Yesu, akarudi kutoa shukrani kwa Yesu, na Yesu akamsifia.
Lk 17:11-18
Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya. Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali, wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu! Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika. Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu; akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria. Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi? Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?

Yesu ni Mungu. Yupo mahali pote. Shukrani zinazotolewa hata kwa njia ya mitandao anaziona na anazipokea.
napendekeza sifa, utukufu na shukrani zielekezwe kwa Mungu muweza wa yote,

na sio kujisifia wenyewe binafsi ya kwamba tu watu wema mitandaoni, baada ya neema na baraka za Mungu kutamalaki katika maisha yetu. Tumrudishie Mungu shukrani hadharani :NoGodNo:
 
na sio kujisifia wenyewe binafsi ya kwamba tu watu wema mitandaoni
Mkuu, soma vizuri uzi wangu. Mwishoni nimesema hivi: "Jamani Mungu ni Mkuu sana! Nawasikitikia wanaosema eti Mungu hayupo. Wanakosa baraka nyingi. Tangu nimwamini Yesu, nimeona miujiza mingi ya kupita kawaida. Hata huo ni muujiza. Nilikuwa na shida ya pesa, nikamuomba Mungu, amenipa mapesaaa!"

Hayo maneno yananisifu mimi au yanamsifu Mungu.
 
Back
Top Bottom